Jumatatu, 12 Muharram 1447 | 2025/07/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Majeshi: Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chache

Enyi Majeshi katika ardhi za Waislamu, hasa zile zinazoizunguka Palestina: Je, kuna udhuru wowote uliobaki kwa wanaoomba msamaha? Je, kuna hoja yoyote iliyobaki kwa wanaolaani? Vipi mnaweza kuona na kusikia uvamizi na mauaji ya Mayahudi hali mmekaa katika sehemu zenu, bila kutikisika, badala ya kuelekea katika ardhi ya Al-Ribat, Palestine Ardhi Iliyobarikiwa, ili kurudisha uvamizi wa Mayahudi na kuliondoa umbile lao?

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Mjini Gaza, Mashahidi 400 ndani ya Masaa 5!

Maneno yanashindwa kuelezea uhalifu huu wa kutisha katika mwezi huu mtukufu. Mayahudi wa Netanyahu na Marekani ya Trump wanawaonea watu wasio na hatia huku wakiwa wamelala, wakitumia ndege 100, zikiwemo ndege za kivita za Marekani, kulenga mahema yaliyojaa raia, kwa kisingizio kwamba wapiganaji wachache wa upinzani wapo. Waliwafuatiulia huku kukiwa na udanganyifu waliouita "usitisha mapigano"!

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kweli Mpaka Siku ya Mwisho ni kwa Umma wa Kiislamu Pekee

Hata leo, katikati ya misiba isiyohesabika na isiyoweza kuvumilika, Ummah huu umethibitika kuwa thabiti katika kitambulisho chake na hivyo hauwezi kuangamizwa. Imethibitika kuwa unastahiki vyeo ulivyotunukiwa na Mola wa walimwengu, Mwenyezi Mungu Azza wa Jall! Angalia Kashmir, India, Afghanistan... Angalia Waislamu wa Syria, Turkestan Mashariki, Myanmar, katika nchi za Afrika, duniani kote, na mwisho kabisa Waislamu wa Palestina na hasa Gaza! Magaidi hao wa Kizayuni wameshindwa katika kila lengo lao kuhusu Gaza. Ummah huu umethibitisha mara kwa mara, kwamba uwepo wake hauzimiki! Hata adui zake wawe wakatili kiasi gani!

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali za Usiku “Mutachukua Hatua Lini kwa ajili ya Gaza?!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili ya halaiki ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi 17, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu zaidi ya 170,000, wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa amali kubwa za usiku katika idadi kadhaa ya miji Uturuki kufuatia umbile halifu la Kiyahudi kukiuka makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano alfajiri ya Jumanne tarehe 18/03/2025.

Soma zaidi...

Doria ya Pamoja ya 'CORPAT' na Adui India na Zoezi la Pande Mbili 'Bangosagar' Inathibitisha kuwa Vibaraka wa Marekani-India Wanacheza na Ubwana wa Nchi kwa Maslahi ya Mabwana zao Wakoloni

Moja ya sababu zilizomfanya msaliti Hasina kupinduliwa na watu ni kwamba alitekeleza njama ya India kule Pilkhana na mara kwa mara alifanya majaribio mabaya yote ya kuweka udhibiti wa India juu ya jeshi la nchi hiyo. Wakati ambapo wananchi wanapaza sauti kudai haki kwa mkasa wa Pilkhana, doria ya pamoja 'CORPAT' na zoezi la pande mbili 'Bangosagar' lililofanyika katika Ghuba ya Bengal kwa kushirikisha jeshi la wanamaji la Bangladesh na India imewashtua watu. Kwa kweli, vibaraka wa Marekani-India wamedhamiria kulinda maslahi ya kijiografia ya wakoloni wao hata kwa gharama ya ubwana wa nchi. Inafaa kutaja kwamba wakati matabaka ya kisiasa ya kisekula ya nchi hayakupaza sauti yake dhidi ya njama hiyo ya Pilkhana, ni Hizb ut Tahrir pekee ndiyo iliyofichua njama hiyo mbele ya taifa hilo kwa ushujaa na kupinga njama hiyo dhidi ya ubwana wa nchi hii.

Soma zaidi...

Wanawake Waliofaulu katika Uislamu wana Sifa hizi

Katika Uislamu, hakuna fahamu ya kuingia Jannat kulingana na nani unamjua na hadhi yako ya kidunia ni ipi. Wote walisifiwa na Mwenyezi Mungu (swt) kwa sababu ya sifa zao za pamoja za kuwa karibu katika utendaji wao wa kuwa kama mfano wa Mtume (saw). Ikiwa tunataka hadhi sawa ya kuingia Jannat lazima basi tufuate mfano wao wa kufanikiwa. Sifa zifuatazo basi zinahitajika.

Soma zaidi...

Vipi Tunaweza Kuwa Miongoni Mwa Wenye Mafanikio hapa Duniani na Akhera?

Mafanikio yanazunguka ulimwengu huu na Akhera, anayemcha Mwenyezi Mungu (swt) humsahilishia mambo yake, hubariki matendo yake, huitengenezea nafsi yake, mke wake na watoto wake, humpa njia ya kutokea katika matatizo, humruzuku kutoka katika vyanzo asivyotarajia, na humtosheleza. Zaidi ya hayo, Yeye (swt) humlipa sana subira yake wakati wa matatizo. Wengine wamesema: "Mafanikio ni kupata ushindi na kufikia lengo la mtu. Katika dunia hii, maana yake ni kupata furaha inayoleta kutosheka katika maisha. Katika Akhera, ina jumuisha mambo manne: uwepo milele usio na mwisho, heshima bila fedheha, mali bila umasikini, na elimu bila ya ujinga."

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu