Pongezi kutoka kwa Amiri wa Hizb ut Tahrir, Mwanachuoni Mkubwa, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, kwa Wanaozuru Kurasa zake kwa Mnasaba wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan wa Mwaka 1447 H sawia na 2026 M
- Imepeperushwa katika Hotuba
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Enyi Waislamu, nawakumbusha haya yote katika siku hizi ambapo uvamizi wa kikatili wa Mayahudi dhidi ya Ukingo wa Magharibi pamoja na Gaza unaendelea, kisha uvamizi wa Mayahudi ukaenea hadi Lebanon na Syria… ambapo waliranda wakiwa huru katika nchi za Kiislamu bila kukutana na upinzani wowote wa kweli. Badala ya watawala kuhamasisha majeshi ya Waislamu kupigana na umbile la Kiyahudi, kuwafukuza wale walio nyuma yake na kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa... badala yake, tunawaona watawala hawa wakisaini makubaliano baada ya makubaliano nalo, na hata mtawala dhalimu Trump anawakusanya pamoja ili kuwadhalilisha, bila aibu yoyote mbele ya Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, au waumini!



