Jumanne, 14 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wewe Ndiye Uliyewaletea Waislamu Njaa, Masoud Pezeshkian!

Iran ilitangaza kufilisika kwa benki yake kubwa zaidi ya kibinafsi, Benki ya Ayandeh, ambayo ina matawi 270 nchini Iran, baada ya madeni yake kupanda zaidi ya dolari bilioni tano, na kinachoshangaza ni ukosoaji wa rais wa Iran Masoud Pezeshkian kuhusu kushindwa kwa utawala akisema: “Tuna mafuta na gesi lakini tuna njaa”!

Soma zaidi...

Watawala wa Waislamu Hawana Sifa za Kulinda Heshima ya Waislamu!

Vyombo vya habari viliripoti kwamba Rais wa Marekani Donald Trump alicheza densi kwenye zulia jekundu kwenye uwanja wa ndege nchini Malaysia mnamo Jumapili, 26/10/2025, alipopokewa na Waziri Mkuu wa Malaysia. Idadi ya Wamalaysia, wanaume na wanawake, walipunga bendera za Marekani na kucheza muziki wa kienyeji ili kumkaribisha mhalifu huyo muuaji ambaye mikono yake imejaa damu ya Waislamu wa Gaza.

Soma zaidi...

“Vita vya Burqa” vya Wananchi Ni Mwangwi wa Kisasa wa Ukoloni wa Ulaya, Uliotumika Kupuuza Mauaji ya Halaiki mjini Gaza na Kumvua Mwanamke wa Kiislamu Kitambulisho Chake cha Kiislamu

Vita vya hivi karibuni vya watu wengi kutoka kwa vyama vya kidemokrasia na serikali za mrengo wa kulia vinavyotaka kupigwa marufuku kwa burqa sasa vinajumuisha Australia, Italia na Ureno. Mataifa haya ni sehemu ya kundi kubwa la nchi adui za Ulaya ambazo tayari zimepiga marufuku burqa. Ufaransa, Ubelgiji, Denmark, na Uswizi zinatekeleza marufuku ya kitaifa katika maeneo yote ya umma, huku Uholanzi na Ujerumani, zikiwa na marufuku ya sehemu inayolenga muktadha maalum kama vile shule au afisi za serikali. Nchini Uingereza, mjadala unalenga wafanyikazi, ambapo chama cha mrengo wa kulia cha Mageuzi cha Uingereza kinasema kwamba burqa kama hizo zinazuia uoanishwaji, mawasiliano, na usalama, zikiziita “nembo za mgawanyiko.”

Soma zaidi...

Mayahudi Hawaheshimu Maagano Wala Hawawezi Kuaminiwa, Na Wapatanishi Si Waaminifu

Umbile la Kiyahudi limekiuka makubaliano ya kusitisha mapigano dhidi ya Gaza zaidi ya mara 80, na kusababisha mashahidi wengi na majeraha, pamoja na kubomolewa kwa nyumba na uharibifu wa mali. Waziri mkuu wa umbile la Kiyahudi hata alijisifu kwamba aliangusha tani 153 za mabomu kwenye Ukanda wa Gaza kwa siku moja.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chahitimisha Kampeni yake ya Kimataifa: “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kimeendesha kampeni ya kimataifa ya kuinua ufahamu wa kimataifa na kuleta muanga wa kimataifa kuhusu mgogoro wa kutisha wa kibinadamu uliosababishwa na mzozo nchini Sudan ambao umekuwa ukiendelea kwa miaka mitatu na nusu sasa. Mzozo huu usio na maana, kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) vinavyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (“Hemedti”), umesifiwa kama “Vita Vilivyosahaulika” kutokana na kutopokea uangaziaji wa vyombo vya habari na uangalizi wa kimataifa unaostahili.

Soma zaidi...

Wanawake wa Kashmiri Walibakwa na Kuteswa na Uvamizi wa Dola ya India Tangu 1947

Wakati wa Kikao cha 60 cha Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) mwaka huu, Kikao cha Kimataifa kisicho cha Kiserikali kilifanyika kuhusu Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kitamaduni za Wanawake, kilichoandaliwa na OCAPROCE International chini ya kichwa, “Wanawake kwa ajili ya Kukuuza na Kulinda Turathi ya Kitamaduni na Ujenzi wa Amani Endelevu ifikapo 2030,” ambapo mwakilishi wa wanawake wa Kashmir Dkt. Shugufta, aliangazia masaibu ya wanawake wa Kashmir mikononi mwa gaidi amvamizi, vikosi vya jeshi la India. Alisema, “Ninasimama mbele yenu leo ​​kwa sauti inayobeba maumivu ya wanawake wengi walionyamazishwa kutoka bonde la Jammu na Kashmir Inayokaliwa Kimabavu Kinyume cha Sheria.

Soma zaidi...

Maadhimisho ya Mwaka wa Pili wa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Matunda Yaliyonyunyiziwa kwa Damu Safi

Tarehe 7 Oktoba iliadhimisha mwaka wa pili wa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa. Miaka miwili kamili imepita tangu umbile nyakuzi kulenga watu wetu mjini Gaza, likiwafungulia mpangilio wa kuua, kuhamisha, na njaa, na kutumia viwango vya juu vya ushenzi na ukatili dhidi yao. Kwa hivyo ni nini kimebadilika kwa vita hivi vya dhulma?!

Soma zaidi...

Mauaji na Njaa ya Watoto wa Gaza Havitakwisha Kupitia Mipango ya Wale Waliohusika na Mauaji ya Halaiki Bali Kupitia Uhamasishaji wa Majeshi ya Waislamu Pekee

Katika kipindi cha miaka 2 iliyopita, watu wa Gaza wamekuwa wakikabiliwa na mashambulizi ya mabomu, mzingiro wa kikatili na jinai za kutisha zaidi za umbile la mauaji la Kiyahudi, ambapo wanawake na watoto wamekuwa wahanga wakuu. 65,000 wameuwawa, wakiwemo zaidi ya watoto 20,000 – sawa na watoto 30 wanaouawa kila siku. Watoto wamepigwa risasi kimakusudi na wavamizi wa Kiyahudi au mashambulizi ya droni barabarani, au hata wanapotafuta chakula kwenye vituo vya misaada ambavyo vimekuwa ‘mitego ya kifo’ kwa wanaokabiliwa na njaa. Kulingana na ‘Save the Children’, watoto waliuawa au kujeruhiwa katika zaidi ya nusu ya mashambulizi mabaya katika maeneo ya usambazaji wa chakula mjini Gaza ndani ya wiki nne baada ya Wakfu wa Kibinadamu wa Gaza kuanza shughuli zake.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Chukueni Hatua na Msiache Masuala Yenu Yawe Mikononi mwa Maadui Zenu

Mazungumzo ya awamu ya kwanza ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kusimamisha vita dhidi ya Gaza yalianza mjini Sharm El-Sheikh nchini Misri, kwa kuhudhuriwa na wajumbe wa Marekani Steve Witkoff na Jared Kushner, Waziri Mkuu wa Qatar, na wakuu wa kijasusi wa Uturuki na Misri.

Soma zaidi...

Machozi ya Furaha kwa Maadui wa Mwenyezi Mungu, Kushindwa na Kukata Tamaa kwa Waislamu nchini Cyprus

Aprili iliyopita, Baraza la Mawaziri la Cyprus Kaskazini lilitoa “amri ya kiserikali” ambayo inaruhusu wanafunzi kuvaa hijabu za Kiislamu katika shule za sekondari. Hata hivyo, Muungano wa Walimu wa Sekondari wa Cyprus na Uturuki (KTOEOS), ulianza migomo, ukakataa kufundisha watoto waliofika shuleni wakiwa wamevalia mavazi ya kidini, na hatimaye wakaiomba Mahakama Upeo. Wiki iliyopita (mwisho wa Septemba), Mahakama ya Upeo ya Cyprus Kaskazini ilibatilisha “amri ya kiserikali”, ikiamua kuwa ilikuwa kinyume na katiba. Viongozi wa Muungano huo wa Walimu, ambao waliomba kubatilishwa kwa amri hiyo, walisherehekea kuregea kwa marufuku ya hijabu kama “ushindi kwa usekula” kwa kububujika “machozi ya furaha”. Wakati huo huo serikali imetangaza kuanza mara moja “kufanyia kazi sheria mpya”.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu