Unafiki wa Magharibi; Kati ya Kulaani Tukio la Sydney, na Kimya Juu ya Mauaji katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Bado hakuna kiongozi hata mmoja wa nchi au kiongozi wa Magharibi au wa Kiarabu ambaye hajashutumu tukio la Sydney, ambapo watu kumi na tano waliuawa kwa kupigwa risasi kufuatia shambulizi lililolenga tamasha la Mayahudi la Hanukkah jijini Sydney. Hata hivyo hatujaona azma mithili ya hiyo katika kulaani jinai za umbile la Kiyahudi katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Kama kawaida, rai jumla ya umma imepotoshwa, na kupuuzwa kabisa nia ya tukio hilo, kwani kila mtu alijikita kukemea kitendo hicho, bila kujali sababu iliyowafanya washambuliaji hao wawili kuwafyatulia risasi washerehekaji.



