Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chahitimisha Kampeni yake ya Kimataifa: “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kimeendesha kampeni ya kimataifa ya kuinua ufahamu wa kimataifa na kuleta muanga wa kimataifa kuhusu mgogoro wa kutisha wa kibinadamu uliosababishwa na mzozo nchini Sudan ambao umekuwa ukiendelea kwa miaka mitatu na nusu sasa. Mzozo huu usio na maana, kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) vinavyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (“Hemedti”), umesifiwa kama “Vita Vilivyosahaulika” kutokana na kutopokea uangaziaji wa vyombo vya habari na uangalizi wa kimataifa unaostahili.