Urusi Yajaribu Kubandika Shtaka la Ugaidi kwa Chama Kinachoheshimika zaidi cha Kisiasa ili Kuhalalisha Ukandamizaji na Kufilisika kwake!
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Chini ya kichwa cha habari: "Huduma ya Usalama ya Urusi yakamata seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir," Russia Today ilichapisha ripoti mnamo 5 Februari 2025, ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir huko Crimea na kuwakamata watu watano ambao walikuwa wakisajili wafuasi wa chama hicho, ambacho kimepigwa marufuku nchini Urusi." Video ilionyeshwa inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba.