Ijumaa, 06 Rajab 1447 | 2025/12/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Taarifa ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari Wenye Kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan Unazidisha Majeraha na Kugawanya Nchi”

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Muawiya Othman, kufuatia ziara ya Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Utawala na Kamanda wa Jeshi, Luteni Jenerali Burhan, nchini Saudi Arabia, Muawiya alisema mnamo Jumatatu jioni, 15/12/2025: “Rais alielezea shukrani zake kamili kwa azimio la Rais wa Marekani Donald Trump la kushiriki katika juhudi za kufikia amani na kukomesha vita nchini humo, kwa ushiriki wa Ufalme wa Saudi Arabia. Mheshimiwa alithibitisha nia ya Sudan kufanya kazi na Rais Trump, Waziri wake wa Mambo ya Nje, na Mjumbe wake Maalum wa Amani nchini Sudan, ili kufikia lengo hili zuri bila shaka.”

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Kiongozi wa Al-Ikhwan Al-Muslimina Hassan Abdel Hamid

Jana, Ijumaa 19/12/2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Ustadh AbduAllah, Mratibu wa Kamati hiyo, ulikutana na Ustadh Hassan Abd Al-Hameed kiongozi katika Al-Ikhwan Al-Muslimina nchini Sudan.

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama Vyawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir kwa Kutoa Wito wa Kutibua Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama kiliwakamata Mashababu watano (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Shawak, ambao ni: Othman Al-Amin Kanda, Hassan Al-Amin Kanda, Muhammad Thamin Adam, Ahmad Babikr, na Al-Amin Abdullah. Hili lilikuja kufuatia Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan kufanya kisimamo mbele ya Msikiti wa Kale huko Al-Shawak, ambapo Sheikh Othman Al-Amin Kanda, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alihutubia hudhuri ya watu mashuhuri wa eneo hilo na umma kwa jumla. Katika hotuba yake, alielezea hatari ya mpango wa Marekani unaotaka kuigawanya Sudan kwa kuikata Darfur, akiwapa wale waliohudhuria jukumu la Kisharia linalofanya umoja wa Ummah na umoja wa dola kuwa suala nyeti. Baadhi ya watu mashuhuri walishiriki kwa kutoa kauli zinazothibitisha msimamo wao na pamoja na hizb ili kuzuia mpango wa kujitenga.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza chini ya kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan: Kuongeza Majeraha na Kugawanya Nchi”

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Mji wa Wad Madani

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ulitembelea Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Jimbo la Al-Jazirah jana, Jumamosi, 13/12/2025. Ujumbe huo uliongozwa na Ustadh Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Abdulaziz Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na mhandisi Walid Kamil.

Soma zaidi...

Je, Vituo vya Mafuta Vina Thamani Zaidi na Hadhi Kubwa Zaidi kuliko Watu?!

Imeripotiwa katika habari kwamba Vikosi vya Ulinzi vya Wananchi wa Sudan Kusini vilianza kupeleka vikosi vyake kulinda Uwanja wa Mafuta wa Heglig kufuatia makubaliano ya pande tatu kati ya Mwenyekiti wa Baraza la Uhuru la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir Mayardit, na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo. Mkuu wa Majeshi ya Wananchi wa Sudan Kusini, Paul Nang, alielezea katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka ndani ya uwanja wa mafuta wa Heglig kwamba makubaliano hayo yalibainisha kuondolewa kwa jeshi na kuondoka kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka kutoka eneo hilo, na alithibitisha kwamba lengo la makubaliano hayo lilikuwa kuhakikisha kwamba hakuna hujuma yoyote inayotokea kwenye vituo vya mafuta!!

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Dkt. Muhammad Al-Umda Hammad

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kwa nyoyo zilizoridhika na amri ya Mwenyezi Mungu, macho yanayobubujika machozi, na huzuni kubwa, inaomboleza mmoja wa mashababu wake aliyebeba ulinganizi wa kuregesha maisha kamili ya Kiislamu; kupitia kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume, Mwenyezi Mungu amsamehe: Dkt. Muhammad Al-Umda Hammad

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Katibu Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Al-Jazirah

Mnamo Jumanne, 2 Disemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Mhandisi Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na akifuatana na Ustadh Omar Ibrahim, pia mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na Mhandisi Walid Kamil, walimtembelea Ustadh Imad Ismail Muhammad Ahmad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Al-Jazirah, afisini kwake Wad Madani.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu

Mnamo Jumatatu, 1 Disemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, walimtembelea Dkt. Imad al-Din Muhammad Hamdallah, mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu, afisini kwake Port Sudan.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu