Jumanne, 14 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pongezi kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan Kwa Mnasaba wa Idd Al-Adha 1446 H

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tunafuraha kuwapongeza watu wetu nchini Sudan na Umma wote wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd Al-Adha. Mwenyezi Mungu airudishe kwetu, tukiwa Ummah ulioungana chini ya bendera ya Al-Uqab, bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), chini ya kivuli cha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yahuisha Ibada ya Takbira Katika Mwezi wa Dhul-Hijjah kwa Matembezi ya Kishindo katika Soko Kuu la Port Sudan

Baada ya swala ya Alasiri mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 6 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na tarehe 2 Juni 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan walihuisha ibada ya takbira katika mwezi wa Dhul-Hijjah. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alihutubia waumini katika Msikiti wa Ibn Mas’ud katika soko kuu la Port Sudan baada ya Swalah ya Alasiri, akiwakumbusha juu ya ubora wa siku hizi zilizobarikiwa za Dhul-Hijjah, na jinsi Maswahaba – Mwenyezi Mungu awe radhi nao – walivyozitukuza siku hizi kwa takbira na tahleel. Kisha akaanza kupiga takbira, ikifuatiwa na dua. Baadaye wote wakatoka kwa matembezi ya kishindo wakiwa wamebeba Rayah (bendera) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), na alama kubwa isemayo: "Kuhuisha Ibada ya Takbira katika Mwezi wa Dhul-Hijjah."

Soma zaidi...

Ugonjwa wa Kipindupindu Waangamiza Sudan, na Serikali, kwa Uzembe wake, Inaomba Msaada kwa Mashirika ya Kimataifa!

Shirika la Afya Duniani (WHO) limefichua kuwa takriban wagonjwa 60,000 wa kipindupindu wamerekodiwa nchini Sudan, na kusababisha vifo vya zaidi ya 1640, likionya madhara ya kuporomoka kwa mfumo wa afya nchini humu. Ufichuzi huu unakuja wakati kipindupindu kikienea kwa kasi katika Jimbo la Khartoum, ambapo maambukizi mapya yanazidi 90% ya jumla ya nchi, haswa huko Karari, Omdurman, na Ombada. Mnamo Jumanne, 27/5/2025, Wizara ya Afya ya Sudan ilitangaza kurekodi kesi 2729, pamoja na vifo 172, katika wiki moja. Waziri wa Afya wa Sudan Dkt. Haitham Mohamed Ibrahim alisema kuwa kuenea kwa kipindupindu jijini Khartoum kunatokana na kuzorota kwa hali ya mazingira na matatizo ya vyanzo vya maji ya kunywa. Wakati huo huo, Waziri Mkuu mpya Kamil Idriss anatoa wito kwa WHO, huku ripoti za vyombo vya habari zikisema kuwa anawasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom ili kujadili kusaidia juhudi za kudhibiti kipindupindu nchini humu.

Soma zaidi...

Wanasiasa wa Sudan Wanatekeleza Njama za Amerika Kuichana Nchi!

Mnamo Alhamisi, 13 Februari 2025, Al-Sharq iliripoti kwamba Osama Saeed, kiongozi wa Chama cha Mapinduzi, alisema: “Kundi letu linapanga kutangaza serikali kufikia mwisho wa Februari.” Alikuwa anakusudia serikali sambamba na ile iliyopo Port Sudan kwa sasa. Alifafanua zaidi: “Ngazi za utawala katika serikali ya kiraia ndani ya maeneo yanayodhibitiwa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) zitajumuisha rais wa Baraza Kuu, wajumbe, na Baraza la Mawaziri.”

Soma zaidi...

Al-Burhan Anatafuta Kuiga Mfumo Ule Ule wa Kisekula Uliopita

Katika hotuba iliyotolewa leo na Jenerali Al-Burhan, Mwenyekiti wa Baraza la Utawala na Amiri Jeshi Mkuu, alisema: "Kipindi kijacho kitashuhudia kuundwa kwa serikali ili kukamilisha kazi za mpito. Inaweza kuitwa serikali ya muda. Baada ya kuidhinishwa kwa waraka wa katiba, serikali itaundwa, na waziri mkuu atachaguliwa kutekeleza majukumu yake katika kusimamia baraza la mawaziri la serikali bila kuingiliwa."

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Komesheni Mambo Matatu ya Marekani ambayo Yanahusisha Uhalifu Mkali: Vita, Kuitenga Darfur, na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi

Kila mtu anashangaa juu ya siri iliyoko nyuma ya kuongezeka kwa kasi hii katika operesheni za kijeshi za jeshi hivi karibuni, kama vile vita vilivyokuwa hapo awali, na kwa zaidi ya mwaka mmoja, vimekuwa vikifanyika ndani ya duara lililofungwa, huku kukiwa na kusonga mbele na kurudi nyuma, bila ya kuwepo na uamuzi wa kijeshi kutoka upande wowote.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu