Jumatatu, 12 Muharram 1447 | 2025/07/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Aqida ya Kiislamu Pekee ndiyo Msingi wa Dola, Katiba, na Sheria Lengo ni Uislamu Uingie Madarakani na sio Kutosheka na Muislamu Kuingia Madarakani

Uislamu umetuwajibisha kuifanya Aqiyah (itikadi) ya Kiislamu kuwa msingi wa dola, na wakati huo huo, msingi wa katiba na sheria. Yaani, chanzo pekee cha sheria. Haupaswi kuambatanishwa na vyanzo vyengine vya sheria, kama ilivyo katika katiba zilizotungwa na mwanadamu; baadhi yazo zinadai kwamba Uislamu ndio chanzo kikuu au chanzo msingi cha sheria, huku kiuhalisia wanaazima sheria ngeni kwetu kutoka Magharibi.

Soma zaidi...

Mkutano wa Cairo, kama Watangulizi wake, Unadhihirisha Usaliti wa Watawala wa Kiarabu na Kuitelekeza kwao Gaza na Watu wake!

Gaza haihitaji mipango zaidi inayoiweka chini ya ukaliwaji kimabavu na udhibiti wa Mayahudi. Kinachohitaji kwa hakika ni hatua ya dhati kutoka kwa Ummah na majeshi yake ili kuinusuru na kuikomboa kutokana na mitego ya Mayahudi na Marekani. Bila haya, tutaendelea kuwahesabu mashahidi na majeruhi, tukishuhudia unajisi na kiburi cha Mayahudi—wakati wote huku watawala wa Waislamu wakiendelea kuusaliti Umma na utumwa wao kwa Amerika.

Soma zaidi...

Amerika Yala Sanamu Lake Yenyewe!

Katika Arabuni ya kabla ya Uislamu, baadhi ya Waarabu walikuwa wakitengeneza masanamu yao kutokana na tende; walipohisi njaa, wangekula miungu yao! Leo, historia inajirudia yenyewe, lakini kwa umbo gumu zaidi. Mfumo wa Kimagharibi ambao hapo awali uliinyanyua fahamu ya uhuru hadi kwenye hadhi takatifu—uhuru wa fikra, dhamiri, na dini; uhuru wa kuzungumza na kujieleza; uhuru wa kukongamana kwa amani; ushiriki wa kisiasa; ulinzi wa haki za walio wachache; na kukataza utesaji na kutendewa kikatili – sasa unasaliti maadili haya haya yanapokinzana na maslahi ya mabepari na kipote cha watawala.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wamefichua Udanganyifu wa Ubwana wa Kitaifa na Maslahi ya Kitaifa. Ni Hoja Gani iliyopo ya Kuzuia Kukomeshwa kwa Mfumo wa uliopo Sasa?

Mnamo tarehe 11 Februari 2025, taarifa kwa vyombo vya habari ilitolewa kwenye tovuti ya Mahakama ya Upeo ya Pakistan, ambayo ilifichua mabaki ya udanganyifu wa ubwana wa kitaifa. Taarifa hiyo kwa vyombo vya habari ilisema kuwa Jaji Mkuu na maafisa wengine wa mahakama walikutana na ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na kuwaeleza kuhusu masuala ya Mahakama ya Upeo. Katika taarifa hiyo, Jaji Mkuu alithibitisha kuwa Mahakama ya Upeo inakamilisha ajenda ya kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Mahakama ya Utungaji Sera (NJPMC) katika wiki ya mwisho ya Februari. Hata aliwaalika wajumbe wa wakoloni pia kutoa mapendekezo yao katika suala hili.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu