Kilio cha Wafungwa Kinasikika Nyoyoni mwa Waislamu Baada ya Uamuzi wa Umbile la Kiyahudi wa Kutekeleza Taratibu za Unyongaji
- Imepeperushwa katika Palestina
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Waziri wa Vita na anayeitwa Waziri wa Usalama wa Kitaifa katika umbile la Kiyahudi walitangaza kuanza kwa utekelezaji wa sheria ya adhabu ya kifo kwa wafungwa wanaotuhumiwa kutekeleza mauaji. Hili lilikuja “baada ya kamanda wa Kamandi Kuu katika jeshi la uvamizi, Avi Bluth, kusaini marekebisho ya amri ya kijeshi inayohusiana na Ukingo wa Magharibi” (Raya Network). Idhini ya Knesset ya uamuzi huo haikutosha kutumia sheria hiyo kwa Ukingo wa Magharibi, ambayo haiko chini ya sheria za kiraia moja kwa moja. Marekebisho haya, yaliyotolewa chini ya amri ya kijeshi, yanaruhusu sheria hiyo kutumika ndani ya mahakama za kijeshi zinazofanya kazi katika Ukingo wa Magharibi.



