Mashirika ya Mamlaka ya Palestina na Majambazi Wao Yamkamata Mwanafunzi Saif Abu Al-Hawa
- Imepeperushwa katika Palestina
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mamlaka ya Palestina (PA), ambayo ni tiifu kwa Mayahudi, ilimkamata mwanafunzi Saif Abu al-Hawa alipokuwa akiondoka Chuo Kikuu cha Bethlehem mnamo Jumanne, 9 Disemba 2025. Kwa kutumia majambazi wasaliti na kisha kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama vya PA, katika tukio linaloakisi mbinu za ujambazi na vitisho vya PA dhidi ya watu wa Palestina, hawazuiwi na Dini wala sheria, wala hata utakatifu wa chuo kikuu ambacho Saif alitoka. Kisha alifikishwa mbele ya mahakama mnamo Alhamisi, ambapo jaji aliongeza kifungo chake kwa siku kumi na tano, licha ya kwamba hakufanya uhalifu wowote. Kosa lake pekee lilikuwa kutaja Hukm Shari’ kwamba Waislamu hawaruhusiwi kushiriki katika sherehe za sikukuu za Kikristo!



