Jumapili, 08 Rajab 1447 | 2025/12/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mashirika ya Mamlaka ya Palestina na Majambazi Wao Yamkamata Mwanafunzi Saif Abu Al-Hawa

Mamlaka ya Palestina (PA), ambayo ni tiifu kwa Mayahudi, ilimkamata mwanafunzi Saif Abu al-Hawa alipokuwa akiondoka Chuo Kikuu cha Bethlehem mnamo Jumanne, 9 Disemba 2025. Kwa kutumia majambazi wasaliti na kisha kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama vya PA, katika tukio linaloakisi mbinu za ujambazi na vitisho vya PA dhidi ya watu wa Palestina, hawazuiwi na Dini wala sheria, wala hata utakatifu wa chuo kikuu ambacho Saif alitoka. Kisha alifikishwa mbele ya mahakama mnamo Alhamisi, ambapo jaji aliongeza kifungo chake kwa siku kumi na tano, licha ya kwamba hakufanya uhalifu wowote. Kosa lake pekee lilikuwa kutaja Hukm Shari’ kwamba Waislamu hawaruhusiwi kushiriki katika sherehe za sikukuu za Kikristo!

Soma zaidi...

Mamlaka ya Kihalifu ya Palestina, ikiwemo Wizara ya Masuala ya Wanawake, Yakimbilia Kutekeleza Miradi ya Maadui wa Uislamu ya Kuharibu Familia, Kuvunja Jamii, na Kumponda Mwanamke wa Kiislamu Anayezaa Mashujaa

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Masuala ya Wanawake ilifichua kwamba Wizara hiyo ilifanya warsha pamoja na Kamati ya Mpito ya Kuandika Katiba ili kujadili sifa za kuzifanyia kazi kwenye rasimu ya katiba na kuingiza masuala ya wanawake katika vifungu vyake. Kulingana na taarifa hiyo: “Kwa ushiriki mpana kutoka kwa taasisi rasmi na za kiserikali, taasisi za wanawake na haki za binadamu, na mashirika ya kiraia, na kwa uhudhuriaji mkubwa kutoka kwa viongozi wanawake wa Kipalestina walioko ughaibuni nchini Syria, Jordan, Lebanon, Misri, na Ulaya, Wizara ya Masuala ya Wanawake ilifanya warsha pana ya kitaifa kwa ushirikiano na Kamati ya Mpito ya Kuandika Katiba ya Palestina, kama sehemu ya kuimarisha mazungumzo ya kitaifa kuhusu kuandika katiba inayoakisi matarajio ya watu wa Palestina na kuhakikisha uwepo changamfu wa masuala ya wanawake katika maudhui yake.”

Soma zaidi...

Moyo wa Hebron na Msikiti wa Ibrahimi Wafanywa Kuwa wa Kiyahudi kwa Kufuata Hatua Zile Zile kama Ulivyofanywa kuwa wa Kiyahudi Msikiti wa Al-Aqsa

Baada ya umbile la Kiyahudi kuamua kuhamisha mamlaka ya kiidara ya Msikiti wa Ibrahimi kutoka Manispaa ya Hebron hadi “Baraza la Kidini la Kiyahudi huko Kiryat Arba,” na baada ya umbile hilo kukataa pingamizi iliyowasilishwa na Manispaa ya Hebron kuhusu uamuzi huu, pamoja na uamuzi uliofuata wa kugeuza ua wa ndani wa Msikiti wa Ibrahimi kuwa uwanja wa umma, na pamoja na vyama vya Kiyahudi vinavyofanya kazi ya kununua nyumba katika mji wa Hebron (al-Khalil) - moyo wa Mji wa Hebron, huku Msikiti wa Ibrahimi ukiwa kiini chake, unafanywa kuwa wa Kiyahudi waziwazi mbele ya ulimwengu na mbele ya Umma wa Kiislamu, kama vile eneo la Safari ya Usiku ya Mtume wake (saw) na viunga vyake linavyofanywa kuwa la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Kampeni ya Umbile la Kizayuni katika Ukingo wa Kaskazini Magharibi ni Sehemu ya Mpango wake wa Kuimarisha Makaazi na Kuimarisha Udhibiti wake katika Eneo Hilo. Je, Hakuna Kiongozi Anayeongozwa na Mungu wa Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa?!

Hawa hapa Mayahudi wakizidi kuwa wakali zaidi katika Ukingo wa Magharibi, wakitangaza “operesheni ya kijeshi” kaskazini mwake, wakibomoa nyumba na kuzigeuza zengine kuwa kambi za kijeshi, wakinyang'anya ardhi, wakikamata kundi la Wapalestina na kuua kundi jengine, wakiharibu mifereji ya maji na kung'oa miti, na operesheni yao ya kijeshi inaenea hadi sehemu iliyobaki ya Ukingo wa Magharibi, katikati yake na kusini yake, na hii inaendana na kile walowezi hao wanachofanya, kwa kuzingatia kutolewa kwa sheria inayowaruhusu kupata mali katika Ukingo wa Magharibi, ambayo ilitanguliwa na kufutiliwa mbali kwa sheria ya kutengwa kaskazini yake.

Soma zaidi...

Gaza Inavuna Mavuno Uchungu ya Baraza la Usalama na Uamuzi wa Baraza la Amani

Siku chache baada ya uamuzi wa Baraza la Usalama, watu wa Gaza walianza kuvuna hasara yake; katika muda usiozidi masaa 24, mashahidi 34—wengi wao wakiwa watoto na wanawake—walikuwa wamepanda daraja hiyo hadi kufikia Alhamisi asubuhi, 20/11/2025, pamoja na makumi ya waliojeruhiwa kutokana na uzito wa njaa na kwenye makucha ya baridi kali. Damu hizi safi zilikuwa maana halisi ya uamuzi ulioipa Amerika usimamizi na mamlaka juu ya Ukanda wa Gaza, ikiruhusu kukata vichwa kama ilivyotaka. Ni uamuzi uliopuuza damu, utajiri, na ardhi za watu wa Palestina katika Ukingo wa Magharibi na kuachilia mkono wa Mayahudi kutumbukia ndani ya damu yetu, ambayo ilienea zaidi ya Gaza hadi Kambi ya Ain al-Hilweh nchini Lebanon.

Soma zaidi...

Abbas, Akizungumza kutoka Pango la Maadui wa Uislamu jijini Paris, Anathibitisha Dori ya Kihalifu ya Mamlaka ya Palestina katika Kutekeleza Sera za Marekani na Mayahudi Zinazolenga Kufuta Kadhia ya Palestina na Kuwakata Watu wa Palestina na Watoto Wa

Katika mkutano kati ya Abbas na Macron jijini Paris mnamo Jumanne, 11 Novemba 2025, ambapo kuundwa kwa kamati ya pamoja ya Ufaransa na Palestina ya kuandika katiba ya dola ya Palestina kulitangazwa (Al Jazeera Mubasher), Abbas anaonekana kupata msukumo kutoka kwa historia ya dola zilizo katika eneo hili zilizopitisha katiba za Magharibi kama msingi wa sheria zao. Wamewachukua Wamagharibi kama mabwana zao, badala ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Abbas hakuweza kufanya chochote ila kugeukia Paris na kuwaomba mabwana zake kuandika katiba ya dola iliyo kwenye karatasi—dola ambayo hawezi kuingia au kutoka bila idhini ya Mayahudi.

Soma zaidi...

Uvamizi wa Waliolaaniwa Haukomi Je, kuna kiongozi anayeongozwa na Mungu ambaye atakomesha

Uvamizi dhidi ya Gaza unajirudia kama kile ambacho afisi ya mhalifu Netanyahu ilikiita “mashambulizi makali katika Ukanda wa Gaza” (Al Jazeera), ikidai kwamba Hamas ilifanya shambulizi dhidi ya wanajeshi wake katika Ukanda wa Gaza na kujibu uvunjaji wa makubaliano ya kuregesha miili - ingawa Hamas ilikana uhusiano wake na tukio la ufyatuaji risasi (Al Jazeera). Umbile hilo liliwaua zaidi ya mashahidi hamsini ndani ya masaa, huku likidai kwamba mashambulizi hayo hayamaanishi kuvunjika kwa makubaliano ya kusitisha mapigano! Na Trump anathibitisha kwamba mashambulizi ya Mayahudi hayatahujumu usitishaji mapigano!

Soma zaidi...

Mpango wa Trump ni Sumu Hatari, Ukaliaji Kimabavu wa Marekani na Umoja wa Mataifa wa Gaza, na Uhalifu Mkubwa Uliofanywa na Watawala wa Waislamu

Kujisalimisha na kutoa silaha, kuregeshwa kwa mateka na mabaki ya wafu, na uvamizi unaoongozwa na Marekani, inayoongozwa na Trump kwa jina la Baraza la Amani, likisaidiwa na mwenye chuki dhidi ya Uislamu, Tony Blair, na kutekelezwa na tawala za eneo hili – hizi ndizo sifa za mpango mpya wa Trump, ambao aliutangaza. Amewashukuru viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu na washirika wake barani Ulaya kwa mwitikio wao wa dhati kwake, na kutangaza kuwa viongozi wa eneo hilo wanashiriki kikamilifu katika mpango huo wa amani.

Soma zaidi...

Miradi ya Wamarekani – Mayahudi ni Miradi ya Jinai na Uhaini, Iwe Inatekelezwa na PLO au Wengine

Chaneli 5 ya Kiebrania, kama ilivyoripotiwa na Al Jazeera, ilitangaza ripoti iliyosema kwamba Netanyahu anafanya mkutano kujadili kuchukua nafasi ya Mamlaka ya Palestina pamoja na viongozi wa kikabila huko Al-Khalil (Hebron). Taarifa ilitolewa baadaye na Gavana wa Al-Khalil (katika kujibu mashauri yanayoendelea ya serikali ya uvamizi kuhusu kuitenganisha Al-Khalil kutoka kwa jiografia ya kitaifa na kuikabidhi kwa utawala wa kikabila).

Soma zaidi...

Na anaye fedheheshwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumhishimu. [Al-Hajj: 18]

Baada ya maafikiano yote yaliyofanywa na PLO, ambayo yalifikia uhaini mkubwa kwa kuitoa sehemu kubwa ya Palestina. Na baada ya kukubalika kwake kuwa chombo cha usalama (katika muundo wa mamlaka) kinachowapiga vita watu wa Palestina, kupokonya silaha kambi za ndani ya Palestina kwa kuua, kuzingira na kukamata, na nje ya Palestina kwa uratibu na serikali za Syria na Lebanon, ili kuzuia tishio lolote, kubwa au dogo, kwa usalama wa Mayahudi ndani au karibu na Palestina.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu