Miradi ya Wamarekani – Mayahudi ni Miradi ya Jinai na Uhaini, Iwe Inatekelezwa na PLO au Wengine
- Imepeperushwa katika Palestina
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Chaneli 5 ya Kiebrania, kama ilivyoripotiwa na Al Jazeera, ilitangaza ripoti iliyosema kwamba Netanyahu anafanya mkutano kujadili kuchukua nafasi ya Mamlaka ya Palestina pamoja na viongozi wa kikabila huko Al-Khalil (Hebron). Taarifa ilitolewa baadaye na Gavana wa Al-Khalil (katika kujibu mashauri yanayoendelea ya serikali ya uvamizi kuhusu kuitenganisha Al-Khalil kutoka kwa jiografia ya kitaifa na kuikabidhi kwa utawala wa kikabila).