Jumatatu, 16 Rajab 1447 | 2026/01/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kifo cha Imam Fouad Saeed Abdulkadir: Pindi Hifadhi Inapogeuka Kuwa Mkasa

Idara ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) imethibitisha kifo cha Fouad Saeed Abdulkadir, raia wa Eritrea mwenye umri wa miaka 46, ambaye alifariki tarehe 14 Disemba akiwa kizuizini mwa ICE katika Kituo cha Ushughulikiaji cha Moshannon Valley huko Pennsylvania. Kulingana na ICE, Imam Abdulkadir anaripotiwa kupata maumivu ya kifua na kupokea uangalizi kutoka kwa wafanyikazi wa matibabu na huduma za matibabu za dharura. Kifo chake, mojawapo ya vifo kadhaa vilivyoripotiwa katika vituo vya ICE, bado kinachunguzwa na kimeongeza uchunguzi wa hali za uzuizi na upatikanaji wa huduma za afya za kutosha kwa wafungwa.

Soma zaidi...

Ukandamizaji Unaoongezeka wa Marekani dhidi ya Mashirika ya Kiislamu - Toleo la Texas

Katika hatua ya kushangaza wiki hii, Gavana wa Texas Greg Abbott alitangaza Baraza la Mahusiano ya Kiislamu na Kiamerika (CAIR) na Ikhwan al-Muslimin kama “mashirika ya kigaidi ya kigeni.” Tangazo lake linaharamisha makundi haya kumiliki mali huko Texas na kuidhinisha hatua za kisheria za serikali dhidi ya vyama vinavyohusiana nayo. Ingawa Abbott aliweka uamuzi huo kama msimamo dhidi ya “misimamo mikali,” hatua hiyo inawakilisha ongezeko kubwa la ulengaji unaoendelea wa mashirika ya Kiislamu na inaangazia mgogoro mkubwa wa uhuru wa kuzungumza, ukandamizaji wa serikali, na unafiki katika jinsi Amerika inavyowatendea raia wake Waislamu.

Soma zaidi...

Himaya Yashambulia Gaza - Sami Hamdi na Kifo cha Upinzani

Baada ya umbile la Kizayuni kuifahamisha Marekani kuhusu uamuzi wake wa kuanza tena operesheni zake za uhalifu mjini Gaza, zaidi ya wakaazi 109 wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina - wakiwemo watoto 46 - waliuawa shahidi, na wengine wengi walijeruhiwa tangu Jumanne jioni, 28 Oktoba 2025, katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa kote Ukanda wa Gaza. Mabomu hayo yalilenga nyumba za raia na shule inayowahifadhi watu waliokimbia makaazi yao huko Beit Lahia, kaskazini mwa Gaza.

Soma zaidi...

Msako Mkali wa Amerika dhidi ya Mashirika ya Kiislamu

Katika mahojiano ya hivi majuzi na mtangazaji wa redio Sid Rosenberg, Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alionyesha mchakato unaoendelea wa kuiorodhesha Ikhwan al-Muslimin na CAIR kama mashirika ya kigaidi. Waziri Rubio alisema kwamba uorodheshaji kama huo ulikuwa "katika kazi zao, na ni wazi kuna matawi tofauti tofauti ya Ikhwan al-Muslimin, kwa hivyo itabidi uliorodheshe kila moja yao."

Soma zaidi...

Tanzia ya Anas Al-Sharif na Wenzake

Jioni ya Jumapili, 10 Agosti 2025, hema dogo la vyombo vya habari mbele ya Hospitali ya Al-Shifa Medical Complex katika Mji wa Gaza liliharibiwa kabisa na shambulizi la moja kwa moja kutoka kwa umbile la Kizayuni, na kuua waandishi wa habari watano waliokuwa wakinakili mauaji ya halaiki yanayoendelea huko Gaza. Miongoni mwa waliouawa shahidi walikuwa wanahabari Anas Al-Sharif, Mohammad Qreiqeh, na wapiga picha Ibrahim Zaher, Moamen Aliwa, na Mohammad Noufal. Mwenyezi Mungu (swt) awakubalie miongoni mwa Mitume, wakweli, mashahidi na watu wema – ni maswahaba wema walioje.

Soma zaidi...

Amerika Yala Sanamu Lake Yenyewe!

Katika Arabuni ya kabla ya Uislamu, baadhi ya Waarabu walikuwa wakitengeneza masanamu yao kutokana na tende; walipohisi njaa, wangekula miungu yao! Leo, historia inajirudia yenyewe, lakini kwa umbo gumu zaidi. Mfumo wa Kimagharibi ambao hapo awali uliinyanyua fahamu ya uhuru hadi kwenye hadhi takatifu—uhuru wa fikra, dhamiri, na dini; uhuru wa kuzungumza na kujieleza; uhuru wa kukongamana kwa amani; ushiriki wa kisiasa; ulinzi wa haki za walio wachache; na kukataza utesaji na kutendewa kikatili – sasa unasaliti maadili haya haya yanapokinzana na maslahi ya mabepari na kipote cha watawala.

Soma zaidi...

Hakuna Tofauti Kati ya Uhalifu wa huko New Orleans na Ukatili Unaofanywa na Umbile la Kizayuni huko Gaza

FBI imefichua utambulisho wa mhusika wa shambulizi la kugonga na gari huko New Orleans, Marekani, ambalo lilisababisha vifo na majeruhi ya makumi ya watu wakati wa sherehe za mwaka mpya. Mshambuliaji huyo alitambuliwa kama askari wa zamani wa Wanamaji. Mamlaka mjini New Orleans ziliripoti vifo vya watu 10 na wengine 30 kujeruhiwa baada ya lori kuingia kwenye umati wa watu. Vyombo vya habari vya Marekani viliripoti kwamba watu kadhaa walipoteza maisha baada ya gari hilo kugonga mkusanyiko wa watu kwenye Barabara ya Bourbon katika Mtaa wa Wafaransa wa New Orleans mnamo siku ya Jumatano. Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Nje ya “Israel” ilisema kwamba “Waisraeli” wawili walijeruhiwa katika tukio hilo.

Soma zaidi...

Biden Asherehekea Kuuwawa kwa Yahya Al-Sinwar!

Katika taarifa yake ya kina, Rais Joe Biden alithibitisha kwamba ujasusi wa Marekani ulisaidia “Israel” kumpata na kumlenga Yahya Al-Sinwar, pamoja na viongozi wengine wa Hamas waliojificha chini ya ardhi. “Kwa marafiki zangu wa Israel, hii ni siku ya afueni na tafakari, sawa na mandhari nchini Marekani baada ya Rais Obama kuamuru uvamizi wa Osama Bin Laden mwaka wa 2011,” Biden alisema. “Yahya Al-Sinwar alikuwa kizuizi kikubwa cha amani. Kizuizi hicho sasa kimeondoka, lakini kazi nyingi inabaki mbele.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu