Jumanne, 18 Safar 1447 | 2025/08/12
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marufuku ya Vitabu ya Serikali ya Kibaniani: Jaribio la Kufuta Mapambano na Mihanga ya Kiislamu katika Kashmir Inayokaliwa Kimabavu

Katika onyesho la wazi la ukosefu wa usalama na unafiki, serikali inayoitwa ya “kidemokrasia” ya India, chini ya utawala wake wa kibaniani wa BJP, imetoa amri ya kupiga marufuku vitabu 25 vinavyoandika uhalisia wa kihistoria wa ukaliaji wake wa kimabavu wa Kashmir. Hatua hii, ya tarehe 5 Agosti 2025, inatoka kwa Idara ya Mambo ya Ndani ya idara wa Jammu na Kashmir, ikitangaza kwamba kazi hizi “feki” chini ya Kifungu cha 98 cha Bhartiya Nyaya Sanhita 2023, ikizituhumu kwa kueneza “simulizi za uwongo”, kupigia debe kujitenga, na kutukuza “ugaidi”.

Soma zaidi...

Wamisri Wawili Wapotezwa Kwa Nguvu Baada ya Kuwataka Maafisa wa Usalama Kupinga Mzingiro wa Gaza

Vijana wawili wametoweka baada ya video yao kusambaa mitandaoni inayoonyesha wakivamia kituo cha polisi katika makao makuu ya Usalama wa Dola katika kituo cha polisi cha Ma’asara huko Helwan kusini mwa Cairo, ambapo waliwaweka wanausalama kwenye seli ya gereza. Kusudio la hatua hii ilikuwa kupinga utepetevu wa maafisa kwa watu wa Gaza.

Soma zaidi...

Heshima yote ni kwa Mwenyezi Mungu

Bunge la Seneti mnamo Alhamisi lilipitisha azimio kwa kauli moja, kulaani tukio la mauaji ya wenza mchana kweupe kwa maagizo ya Jirga kwa jina la kile kinachoitwa “mauaji ya heshima” huko Balochistan. Lilisema mauaji haya ya kinyama hayawezi na hayapaswi kufunikwa na hoja yoyote ya kitamaduni, kikabila, au kimila kwa kisingizio cha kile kinachojulikana kama ghairat au “heshima.” Kwa kweli ni uhalifu ambao umelivunjia heshima taifa. Jaribio lolote la kuhalalisha uhalifu kama huo kwa msingi wa “desturi au heshima” halikubaliki kabisa, kama ilivyo kwa mchakato mzima wa kulaumiwa kwa mwathiriwa.

Soma zaidi...

Mkataba wa Biashara na Unyenyekeaji wa Indonesia kwa Maslahi ya Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza makubaliano ya kibiashara na Indonesia, kupunguza ushuru unaotishiwa wa 32% kwa bidhaa za Indonesia hadi 19%. Kwa upande wake, Indonesia ilijitolea kununua nishati ya Marekani kwa dolari bilioni 15, bidhaa za kilimo kwa dolari bilioni 4.5, na ndege 50 za Boeing, ikiwa ni pamoja na aina ya 777. Trump alidai Marekani itapata ufikiaji kamili wa soko la Indonesia bila kulipa ushuru. Makubaliano hayo yalifuatia vitisho vya ushuru wa juu na yalikamilishwa baada ya mazungumzo na Rais wa Indonesia Prabowo Subianto. Bado haijulikani ni lini upunguzaji wa ushuru na ununuzi utaanza kutekelezeka. Biashara ya Indonesia na Marekani ilifikia karibu dolari bilioni 40 mwaka 2024, na nakisi ya biashara ya bidhaa za Marekani ya takriban dolari bilioni 18.

Soma zaidi...

Idhini ya Marekani sio Kipimo cha Uamuzi wa Kisiasa kwa Umma wa Kiislamu

Mnamo tarehe 17 Julai 2025, Dawn News ilinukuu kutoka Reuters, "Ikulu ya White House mnamo Alhamisi ilisema kwamba hakuna ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump iliyopangwa Pakistan "kwa wakati huu" baada ya kuenea kwa taarifa za safari hiyo. Mapema siku hiyo, baadhi ya vituo vya habari vya televisheni vya ndani viliripoti, vikinukuu vyanzo, kwamba Trump alitarajiwa kuzuru Pakistan mwezi Septemba. Chaneli za habari zilisema kwamba Trump pia angetembelea India baada ya kuwasili jijini Islamabad mwezi Septemba. Chaneli hizo baadaye ziliondoa ripoti zao.” [Dawn]

Soma zaidi...

Uislamu uko Mbali na Mazungumzo ya Dini Mseto

Mnamo tarehe 5 Julai 2025, jumba jipya la ibada katika Kanisa la Arise and Shine Tanzania lililopo Kawe, viungani mwa jiji la Dar es Salaam lilizinduliwa. Kanisa hilo linaongozwa na Mwinjilisti na anayejiita ‘mtume’ Boniface Mwamposa ambaye mahubiri yake mwaka 2020 yalileta msiba wa vifo vya waumini zaidi ya 20 kutokana na mkanyagano waliokuwa wakikimbia kupakwa mafuta yenye baraka.

Soma zaidi...

Mpango wa Mosaic: Kubadilisha Chapa Mkakati Uliofeli na Jaribio Jipya la Kuidhibiti Taliban

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hivi karibuni lilifanya kikao maalum kujadili hali ya Afghanistan. Katika mkutano huu, Roza Otunbayeva, mkuu wa Misheni ya Misaada ya Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan (UNAMA), aliwasilisha mfumo mpya wa kina unaoitwa "Mpango wa Mosaic." Alisisitiza kuwa mpango huu haulengi "kusawazisha hali nchini Afghanistan," bali unalenga kuendeleza maslahi ya kweli ya watu wa Afghanistan.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu