Jumamosi, 26 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kimbunga cha Al-Aqsa kiko Hai na Kinaendelea

Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa haikuwa tukio la muda mfupi ambalo lilimalizika kwa makubaliano ya mhalifu Trump na dola ya kikafiri nyuma yake, Marekani, muungaji mkono rasmi wa umbile la Kiyahudi. Badala yake, Kimbunga cha Al-Aqsa kilikuwa ni cheche iliyowasha moto ndani ya nyoyo za Waislamu, na kuzifungua akili na nyoyo zao. Waliona unyonge na uovu wa watawala wao wasaliti, na wakatambua unafiki wa wale wanaodai kuwa ni na ubinadamu, na wanaotetea haki za wanawake na watoto. Wakawa na hakika kwamba sheria za kimataifa, na mikataba si chochote ila ni silaha inayotumiwa na makafiri, dhidi ya Uislamu na Waislamu.

Soma zaidi...

Utumiaji kama Silaha wa “Chuki dhidi ya Mayahudi” kunyamazisha Nusra ya Ukombozi wa Palestina

Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na mijadala mingi nchini Uingereza ikiashiria kuwepo mafungano kati ya maandamano ya Palestina na kuongezeka kwa chuki dhidi ya Mayahudi na mashambulizi dhidi ya Mayahudi nchini humo. Kabla ya kumbukumbu ya mwaka wa 2 wa shambulizi la Octoba 7 la Hamas dhidi ya umbile la Kizayuni, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer, aliwataka wanafunzi wasijiunge na maandamano yanayoiunga mkono Palestina siku hiyo, akionya juu ya “kuongezeka chuki dhidi ya Mayahudi katika barabara zetu”, na kwamba “sio tamaduni ya Uingereza kuwa na heshima ndogo kwa wengine” kwa kufanya maandamano juu ya kumbukumbu hiyo, na kuongeza kuwa maandamano yametumiwa  na baadhi kama “udhuru wa kuchukiza kuwashambulia Mayahudi wa Kiingereza”.

Soma zaidi...

Ulaya Inaendelea Kuunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza

Licha ya kauli mbiu tupu kuhusu kuitambua dola ya Palestina, Ulaya inaendelea kusafirisha silaha kwa umbile hilo la Kizayuni. Habari zilizovuja zilizopatikana na gazeti la Denmark zinafichua kuwa hivi majuzi mwezi wa Agosti, serikali ya Denmark ilituma vifaa vya silaha kwa ndege zilizotumiwa kuua watoto mjini Gaza.

Soma zaidi...

Mpango wa Trump wa Gaza ni Mpango Muovu wa Usaliti Unaolenga Kuangamiza Kadhia ya Palestina

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kuwa Waziri Mkuu wa “Israel” Benjamin Netanyahu amekubali mpango wenye vipengee 20 ambao ungemaliza vita katika Ukanda wa Gaza. Trump na Netanyahu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya mkutano wao jijini Washington. Trump alisema kuwa amani ya Gaza ilikuwa karibu sana kupatikana na kumshukuru Netanyahu kwa kuidhinisha mpango huo (DW Turkish 29.09.2025).

Soma zaidi...

Hotuba ya Rais Erdoğan ya Umoja wa Mataifa: Maneno Yaso Vitendo

Rais Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba yake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, alielezea kile kinachotokea Gaza kama “mauaji ya halaiki,” alisisitiza kuwa Israel inaua watoto kila siku, na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua. Akisambaza picha kutoka Gaza, Rais Erdoğan alisema: “Hakuna vita mjini Gaza ... Huu ni uvamizi, uhamishaji, ufukuzaji, mauaji ya halaiki na uharibifu wa maisha.”

Soma zaidi...

Musibabaishwe na Mikutano, Fungueni Mipaka

Katika Mkutano wa Kilele wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) na Ligi ya Nchi za Kiarabu uliofanyika jijini Doha, mji mkuu wa Qatar, Rais Erdoğan alisema: “Tunafahamu kuwa Israel haitasimama katika muda mfupi isipokuwa itakabiliwa na hisia kali na vikwazo. Tunafahamu kwamba tunazo mbinu za kuzuia hili.” (Agencies 15.09.2025)

Soma zaidi...

Tamasha la OIC Lahitimisha kwamba Qatar na Dola za Kiarabu Zisalie Waaminifu kwa Kuwa Kiatu Kilicho Chakaa cha Amerika Huku Zikibweka Vikali Mawinguni

Kufuatia shambulizi la kombora la umbile la Kizayuni dhidi ya wanachama wa Hamas nchini Qatar, taarifa ya mwisho ya mkutano wa dharura wa kilele wa Waarabu-Waislamu (OIC na Ligi ya Waarabu) uliofanyika jijini Doha mnamo 15 Septemba 2025, “unashutumu vikali uvamizi wa Israel dhidi ya Qatar, na kuutaja kuwa ni kama pigo kwa matarajio yoyote ya amani katika eneo hilo. Tangazo hilo zilizisihi nchi wanachama kuzingatia upya mafungamano yao ya kidiplomasia na kiuchumi na Israel na kufuata hatua za kisheria dhidi yake.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu