Jumanne, 01 Rabi' al-thani 1447 | 2025/09/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ummah Unahitaji Khilafah Kulinda Matukufu Yake Sio Mikataba ya Ulinzi ya Kuwalinda Watawala Vibaraka

Pakistan na Saudi Arabia zimeingia katika makubaliano ya kihistoria ya ulinzi wa pande zote, ambapo uvamizi wowote dhidi ya dola moja utachukuliwa kuwa shambulizi kwa pande zote mbili. ‘Mkataba wa Kimkakati wa Ulinzi wa Pamoja’ ulitiwa saini na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif na Mfalme Mtarajiwa wa Saudia Mohammad Bin Salman katika Kasri la Al-Yamamah jijini Riyadh mnamo Jumatano, 17 Septemba 2025.

Soma zaidi...

Mradi wa Reli wa China–Indonesia: Mkakati wa China Kuidhibiti Indonesia

Indonesia inafikiria kujadili upya deni la mradi wa reli ya mwendo kasi wa Jakarta–Bandung, unaojulikana kama Whoosh, kutokana na mzigo mzito wa kifedha unaouweka kwa mwendeshaji wa reli ya serikali Kereta Api Indonesia (KAI). Waziri wa Biashara Zinazomilikiwa na Serikali Erick Thohir alisema mpango huo utaruhusu KAI kusimamia treni huku serikali ikisimamia miundombinu. Mradi huo wenye thamani ya dolari bilioni 7.3 ulifadhiliwa hasa kupitia mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya China, awali kwa riba ya asilimia 2. Hata hivyo, kukatizwa na maambukizi na masuala ya ardhi yalisukuma gharama zaidi, na kuhitaji ufadhili wa ziada kwa riba ya asilimia 3.4.

Soma zaidi...

Uchaguzi wa Kidemokrasia si Lolote ila Minong'ono ya Ibilisi

Mnamo 13 Septemba 2025 kinyang’anyiro cha kuwania urais wa Zanzibar kilianza rasmi huku chama tawala – Chama Cha Mapinduzi (CCM) na chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo kikizindua kampeni zao. CCM ilisisitiza ‘utulivu’, ‘amani’ na ‘umoja’, huku chama cha ACT Wazalendo kikiweka kipaumbele katika uwajibikaji, usawa, na fursa za kiuchumi.

Soma zaidi...

Kukamatwa kwa Mamia ya Waandamanaji Wanaounga Mkono Palestina kwa Amani nchini Uingereza Yaonyesha Uhalisia wa Kinaya cha Demokrasia

Mnamo Jumamosi, tarehe 6 Septemba, karibu watu 900 walikamatwa katika maandamano ya kuunga mkono Palestina jijini London. Walikuwa wakipinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki na njaa kwa raia wasio na hatia mjini Gaza, pamoja na kupigwa marufuku kwa kundi la Palestine Action ambalo serikali ya Uingereza iliharamisha kuwa shirika la kigaidi mwezi Julai. Waliokamatwa ni pamoja na maaskofu, makasisi, walimu, madaktari, wahudumu wengine wa afya, na vizazi vya wahanga wa mauaji ya Holocaust pamoja na waandamanaji walemavu. Wengi walikuwa wazee – katika miaka yao ya 60, 70 na hata 80 – na walijumuisha mzee mmoja kipofu mwenye umri wa miaka 62 aliye katika kiti cha magurudumu.

Soma zaidi...

Matarajio Yasio na Msingi: Nchini Uzbekistan, Mhubiri Aliyetoka Nchini Uturuki Ashtakiwa

Mahakama ya Jinai ya Wilaya ya Uchtepa ya Tashkent ilianza kusikiliza mnamo Agosti 19 kesi ya jinai dhidi ya mtu wa dini Alisher Tursunov, anayejulikana kwa umma kwa jina bandia la Mubashshir Ahmad. Habari hiyo iliripotiwa na Aziz Abidov, mkuu wa huduma ya vyombo vya habari wa Mahakama ya Upeo ya Uzbekistan. Kulingana na tuhuma ya mashtaka, Tursunov anashtakiwa chini ya vifungu vitatu vya Kanuni ya Jinai ya Uzbekistan.

Soma zaidi...

Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark Ajifanya Kuijali Palestina, Huku Mikono Yake Ikiloa Damu ya Watu Wasio na Hatia wa Gaza

Tarehe 07-09-2025, Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark, Lars Løkke Rasmussen, alisafiri hadi Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kukutana na marafiki zake na wenzake Wazayuni “kuonyesha kujali” na “kutia shinikizo” kwa serikali vamizi ya Kizayuni. Ziara hii ya kirafiki utawala vamizi wa Kizayuni inakuja siku chache tu baada ya Waziri wa Mambo ya Nje huyo kuchapisha video kwenye mtandao wa kijamii, ambapo alitoa maoni kwamba “Serikali ya Denmark sasa inachukua hatua za kuondoa kura ya turufu ya Israel juu ya msimamo wetu [kuhusiana na utambuzi wa baadaye wa Palestina]”.

Soma zaidi...

Ndiyo, Uko Gaza na Gaza Inaangamizwa!

Huku uvamizi na mauaji ya halaiki mjini Gaza, yakiendelea kwa muda wa miezi 23, yamefikia kilele kwa matumizi ya silaha ya njaa inayoangamiza watu pamoja na majaribio ya mbinu mpya za mauaji zinazoitwa “mabomu ya roboti”; siasa za kinyonyaji na za kinafiki za watawala wa nchi za Kiislamu—wanaokabiliwa na ghadhabu za watu wao wenyewe kwa kuitelekeza Gaza—pia zimefikia kilele cha vilele.

Soma zaidi...

Uchaguzi wa DUCSU: Siasa za Kidemokrasia Zimeshindwa Kutumia Nguvu ya Vijana kwa Mabadiliko ya Kweli

Wanafunzi jumla wa Chuo Kikuu cha Dhaka, Chuo Kikuu cha Jahangirnagar, na Chuo Kikuu cha Rajshahi wametarajia kwa nguvu mabadiliko chanya ya kisiasa na uhakikisho thabiti wa ustawi wa wanafunzi baada ya uchaguzi uliodumu kwa muda mrefu wa vyama vyao vya wanafunzi mnamo Septemba. Wanafunzi wengi wa vyuo vikuu hivi walisema kwa uthabiti kwamba walitaka kukomeshwa kwa mila za unyonyaji za siasa za vyuo vikuu, na kuwataka wawakilishi wa wanafunzi wanaokuja kufanya kazi kwa ajili ya kulinda haki za wanafunzi. Walisisitiza kwamba wawakilishi wa wanafunzi waliochaguliwa lazima wawe sauti ya wanafunzi jumla ili kuhakikisha mazingira rafiki kwa wanafunzi katika vyuo vikuu kufuatia mabadiliko ya kisiasa ya Julai 2024 yaliyopatikana kupitia uasi mkubwa ulioongozwa na wanafunzi uliopindua utawala wa Awami League mnamo Agosti 5 mwaka huo.

Soma zaidi...

Kuweka Matumaini juu ya Kuvunjika kwa Safu za “Israel” ni Usaliti Mpya wa Gaza

Kura moja ya maoni ilifichua kuwa 56% ya “Waisraeli” wanaogopa kusafiri nje ya nchi, 67% wanaamini kuwa serikali haiwawakilishi na 62% wanaunga mkono makubaliano ya kina ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas, ikiwemo kuachiliwa huru kwa mateka. Tovuti ya “Zman Yisrael,” ambayo ilichapisha maelezo ya kura hiyo ya maoni mnamo tarehe 5 Septemba 2025, ilifafanua kuwa wengi wa “Waisraeli” walionyesha kutokuwa na uwezo wao wa kusafiri nje ya nchi kutokana na kuongezeka kwa ukosoaji wa kimataifa wa umbile lao pamoja na kutengwa kunakoendelea kwa kimataifa kwa dola yao na kuendelea kwa vita mjini Gaza.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu