Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo (479)
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Malaysia (HTM) uliwasilisha hati ya pingamizi kwa Wizara ya Mawasiliano huko Putrajaya kuhusu kuandaliwa kwa tamasha la “KL Headline Msimu wa 2026”. Hatua hii ilichukuliwa ili kuihimiza serikali kufuta tamasha hilo mara moja, kutokana na madhara makubwa ambayo lingesababisha kwa jamii na ukiukaji wake wa wazi wa sheria ya Kiislamu. Hati hiyo ilipokelewa na Bi. Wan Saidatul Shafina binti Mohamed Amin, Katibu wa Idara ya Mawasiliano ya Kimkakati na Masuala ya Taasisi, kwa niaba ya Wizara. Pia alitenga muda wa kusikiliza maelezo kamili na ya kina ya sababu za pingamizi zilizowasilishwa na Hizb ut Tahrir Malaysia.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon: Maoni ya kila Wiki: “Udanganyifu wa Mazungumzo ya Fedheha!”
Kuala Lumpur iko tayari kuibuka kama mahali mwanana pa ziara za matamasha ya kimataifa barani Asia kupitia “KL Headline Msimu wa 2026,” ambao unakutanisha maonyesho 25 ya wasanii wa kimataifa katika mwaka mzima wa 2026. Mji mkuu wa Malaysia umepangwa kuwa mwenyeji wa maonyesho 25 ya wasanii wa kimataifa katika maeneo sita, yakiwalenga zaidi ya mashabiki 500,000 kutoka pwani za ndani na nje ya nchi - kulingana na mratibu, Live Nation Malaysia.
Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan iliandaa amali katika afisi yake ya Khartoum kusherehekea Idd al-Adha kwa mwaka 1447 H (2026 M). Wakati wa amali hiyo, Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil), msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alitoa hotuba na kujibu maswali kutoka kwa waliohudhuria.