Kukamatwa kwa Mamia ya Waandamanaji Wanaounga Mkono Palestina kwa Amani nchini Uingereza Yaonyesha Uhalisia wa Kinaya cha Demokrasia
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumamosi, tarehe 6 Septemba, karibu watu 900 walikamatwa katika maandamano ya kuunga mkono Palestina jijini London. Walikuwa wakipinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki na njaa kwa raia wasio na hatia mjini Gaza, pamoja na kupigwa marufuku kwa kundi la Palestine Action ambalo serikali ya Uingereza iliharamisha kuwa shirika la kigaidi mwezi Julai. Waliokamatwa ni pamoja na maaskofu, makasisi, walimu, madaktari, wahudumu wengine wa afya, na vizazi vya wahanga wa mauaji ya Holocaust pamoja na waandamanaji walemavu. Wengi walikuwa wazee – katika miaka yao ya 60, 70 na hata 80 – na walijumuisha mzee mmoja kipofu mwenye umri wa miaka 62 aliye katika kiti cha magurudumu.