Mikutano na Matembezi ya Kulaani Yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh: Enyi Watu! Pingeni Mpango wa Kupeleka Jeshi Letu Gaza chini ya Kikosi Kilichopendekezwa na Trump, na Takeni Msimamo Wazi kutoka kwa Wagombea katika Uchaguzi Ujao
- Imepeperushwa katika Bangladesh
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir katika Wilayah Bangladesh, iliandaa mikutano na matembezi mengi ya kulaani leo, Ijumaa (16 Januari 2026), baada ya swala ya Ijumaa, katika majengo mbalimbali ya misikiti jijini Dhaka na Chattogram, dhidi ya mpango wa kupeleka vikosi vya nchi hii kwa “Kikosi cha Kuleta Utulivu wa Kimataifa” kilichopendekezwa na Trump huko Gaza. Ili kupinga mpango huu mbaya wa Marekani, na kuwataka wagombea na vyama vya kisiasa katika uchaguzi ujao kuelezea msimamo wao kuhusu suala hili.



