Kwa Uislamu, Watu wa Sudan Wanayeyushwa ndani ya Chungu Kimoja, na Wanaishi Maisha yenye Staha na Haki Chini ya Dola Yake
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Idadi ya watu wa Sudan inakadiriwa kufikia milioni 49.4, kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) mwaka 2024. Asilimia tisini na sita ya wakaazi wote ni Waislamu, huku jamii ndogo ya Wakristo na watu binafsi wakifuata dini za kipagani. Jamii ya Wasudan inaundwa na makabila ya asili ya Waarabu, Waafrika, na Wanubi, yakiwakilisha zaidi ya makabila 500. Waarabu wanaunda kabila kuu, linalojumuisha 70% ya idadi ya watu, pamoja na makabila mengine, yakiwemo Beja, Nuba, Fulani, Geberti, Fur, Masalit, na mengineyo.