Jumamosi, 01 Safar 1447 | 2025/07/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Soma zaidi...

Taarifa ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari Uliofanyika Jumamosi, 19/07/2025, jijini Port Sudan “Hakuna Serikali Inayoleta Matumaini Isipokuwa chini ya Uislamu na Dola yake ya Khilafah”

Mnamo Jumatatu, 19/05/2025, Mwenyekiti wa Baraza la Utawala, Abdel Fattah Al-Burhan, alitoa uamuzi wa kumteua afisa wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kamal Idris kuwa Waziri Mkuu kuunda serikali ya kitaalamu. Siku hiyo hiyo, Al-Burhan pia alitoa uamuzi wa kufutilia mbali agizo la hapo awali lililowapa wanachama wa Baraza Kuu usimamizi wa wizara na vitengo vya serikali ya kifederali.

Soma zaidi...

Majanga na Maafa ni Matokeo ya Kimaumbile ya Kukosekana Dola yenye Kujali

Katika msururu wa ajali za mara kwa mara na moto wa kutisha-hasa ule moto wa ukumbi wa harusi wa mwaka 2023 huko Ninawi, ambao uligharimu maisha ya zaidi ya watu 120 na kujeruhi 200; moto wa mwaka 2021 katika Hospitali ya Al-Hussein huko Dhi Qar, ambao uliua zaidi ya watu 92; na moto wa mwaka 2021 wa kituo cha utengaji wagonjwa wa COVID-19 katika Hospitali ya Ibn Al-Khatib jijini Baghdad, ambao ulisababisha vifo vya watu 82-unakuja msiba mwengine tena wa kutisha. Moto mkubwa ulizuka katika soko kuu la Kut jioni ya Jumatano, 16 Julai 2025. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq ilithibitisha kuwa moto huo, ambao ulizuka ndani ya jengo la biashara la ghorofa tano katikati mwa mji wa Kut, uliwaua watu 61, ikiwa ni pamoja na miili 14 iliyoungua ambayo bado haijatambuliwa. Waathiriwa wengi walikufa kutokana na kuvuta moshi. Wizara hiyo iliongeza kuwa jengo hilo ambalo lilikuwa na mkahawa na kituo cha biashara, lilikuwa limefunguliwa kwa siku saba pekee.

Soma zaidi...

Matukio ya Umwagaji damu huko Sweida Yafichua Hatari za Makundi Yenye Uhusiano wa Kigeni Uhalalishaji Mahusiano ni Jinai Inayohujumu Miaka 14 ya Muhanga wa Mapinduzi

Kufuatia siku kadhaa za mapigano makali yaliyogharimu maisha ya mamia ya ndugu zetu waliokufa shahidi, Wizara ya Ulinzi ghafla na kwa mshtuko ilitangaza Jumatano kuwa ni siku ya kuanza kujiondoa kwa jeshi la Syria katika mji wa Sweida. Haya yanajiri baada ya wito wa Marekani wa kuondoa vikosi vya serikali katika jimbo hilo na msururu wa mashambulizi makali ya anga yaliyofanywa na umbile la Kiyahudi mjini Damascus siku ya Jumatano, Julai 16, 2025, yakilenga jengo la Jeshi, Wizara ya Ulinzi na maeneo jirani ya Kasri la Rais. Mashambulizi ya awali yalikuwa yamepiga maeneo mengi viungani mwa Damascus, Daraa na Sweida, yakilenga maeneo ya kijeshi na misafara ya jeshi la Syria na vikosi jumla vya usalama vilivyokuwa vikielekea Sweida, na kusababisha idadi kubwa ya mashahidi na majeruhi.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi Habari

Kwa ndugu na dada zetu waheshimiwa katika vyombo vya habari, ikiwa ni pamoja na magazeti, redio, na runinga, sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tuna furaha kukualikeni kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari wenye kichwa: Hakuna Serikali inayoweza Kutoa Matumaini Isipokuwa chini ya Uislamu na Dola yake ya Khilafah.

Soma zaidi...

Bwawa la An-Nahdha: Silaha Mpya ya Marekani ya Kuvunja Utashi wa Misri na Kuzuia Ukombozi Wake kutokana na Utiifu

Tangu Ethiopia ilipotangaza ujenzi wa Bwawa la Kuu la Ethiopia la An-Nahda Dam kwenye  Nile ya Samawati mwaka 2011, uhalifu mkubwa wa kisiasa na wa kimkakati umekuwa ukijitokeza. Wale wenye ufahamu wanaona sio tu kama jengo la maji au mradi wa maendeleo, lakini kama chombo kipya cha kikoloni kinachotumiwa na Amerika kutawala eneo hili - hasa Misri, kitovu cha ardhi za Kiislamu, ambayo inakusudiwa kubaki kudhalilishwa chini ya shinikizo la kiuchumi, kisiasa, na hata la maji, kama sehemu ya mtindo mpya wa vita visivyo vya moja kwa moja.

Soma zaidi...

Mashambulizi ya "Warefu Tisa" yatamalizwa tu kwa Utekelezaji wa Adhabu za Sharia chini ya Dola ya Khilafah

Habiba Al-Amin, mwandishi wa habari wa tovuti ya Kush News, alishambuliwa vikali na wanachama wa genge la "Warefu Tisa" katika eneo la kivuko kwenda Port Sudan alipokuwa akiregea kutoka kwenye uangaziaji wa habari akiwa na wenzake kadhaa. Hili ni moja tu ya matukio mengi ya uporaji, ujambazi na mauaji katika miji inayodaiwa kuwa salama, kama vile Omdurman, Khartoum, na sasa mji mkuu wa utawala, Port Sudan. Hii ni miji iliyo chini ya udhibiti wa serikali na vyombo vyake vya usalama.

Soma zaidi...

Ziara ya Azerbaijan: Hatua kuelekea Kusukuma Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi Ambayo Itakuwa ni Mchomo wa Kisu ndani ya Moyo wa Ummah

Chanzo cha kidiplomasia jijini Damascus kilisema mnamo Jumamosi kwamba mkutano wa moja kwa moja utafanyika kati ya afisa mmoja wa Syria na afisa mwengine wa 'Israel' huko Baku kando ya ziara ya Rais wa Syria Ahmad Al-Shara nchini Azerbaijan, kulingana na shirika la habari la Agence France-Presse (AFP).

Soma zaidi...

Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu

Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa: Chombo Mikononi mwa Makafari cha Kudhibiti Sera ya Ndani ya Nchi Inayokopa

Mnamo Jumatano, 9/7/2025, Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ulionya kwamba uchumi wa Iraq unakabiliwa na changamoto kubwa. Bodi ya IMF, katika taarifa yake ya kuhitimisha mashauriano ya Kifungu cha IV na Iraq, ilisema kuna nafasi ya kuimarisha mapato yasiyo ya mafuta kupitia ongezeko la kodi na ushuru wa forodha.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu