Jumatano, 08 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan inafuraha kuwaalika ndugu zetu wanahabari, wanasiasa, na wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha kisiasa, ambacho kitamkaribisha Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, chenye kichwa: Msimamo wa Serikali kuhusu Kufutwa kwa Kadhia ya Palestina na Hukmu ya Sharia juu yake.

Soma zaidi...

Watu Wapendao Uislamu wa Nchi Wameukataa Mkataba wa Julai, ambao umejengwa juu ya Msingi wa Usekula na Demokrasia Batili ya Magharibi, Na Wanataka Mkataba wa Madina uliojengwa juu ya Msingi wa Imani yao Safi ya Kiislamu

Mnamo 17 Oktoba 2025, kipote cha wanasiasa wenye uchu wa madaraka nchini humu walitia saini ‘Mkataba wa Julai - suluhisho la kisiasa lililoandikwa kwa kuzingatia imani potofu za kidemokrasia ya kisekula na mfumo wa Wakoloni makafiri wa Magharibi hasa Marekani-Uingereza, na kuweka mfano mwengine wa kuchukiza wa usaliti kwa Uislamu na Waislamu, na utiifu kwa nchi za Magharibi. Mfumo huu wa kisekula wa kibepari uliotungwa na wanadamu umefeli katika nchi zote duniani. Jambo hili ni la kweli mithili ya mwangaza wa mchana kwamba, mfumo huu wa ukandamizaji unalinda maslahi ya tabaka tawala, mabepari wachache na wakoloni wa Magharibi, na kuwanyonya watu wengi zaidi. Mnashuhudia kwamba kizazi cha vijana (Gen-Z) katika nchi nyingi wanaasi tabaka tawala la kibepari moja baada ya jengine na kuwaangusha watawala.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa wafikia Kukaba Uchumi wa Yemen ili Kukamata Rasilimali Zetu za Kiuchumi

Mnamo tarehe 15/10/2025, Gavana wa Benki Kuu ya Aden, Ahmed Al-Maabqi, alikutana jijini Washington D.C., na mkuu wa ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) nchini Yemen, Esther Pérez Ruiz, na mwakilishi wa IMF, Mohamed Maait, akiandamana na Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Waziri Msaidizi wa Fedha Abdul Qader Amin. Hii ilifuatiwa na mkutano kati ya Waziri wa Mipango na Ushirikiano wa Kimataifa na Gavana wa Yemen kwa Benki ya Dunia, Waed Badhib, na Riccardo Puliti, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa wa Kanda ya Mashariki ya Kati, pamoja na ushiriki wa Naibu Waziri wa Mipango Nizar Basuhaib, Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Abdul Qader Amin, kwa uwepo wa Stefan G. G. Reimbert, Mkurugenzi wa Kanda wa Benki ya Dunia katika Mashariki ya Kati, na Dina Abu Ghaida, Meneja wa Benki ya Dunia nchini Yemen.

Soma zaidi...

Ukamatwaji wa Wanachama wa Hizb ut Tahrir jijini Beirut!

Katika marudio ya mbinu na hatua za ukamataji holela wa vyombo vya usalama bila msingi wowote wa kisheria, wa watu—baadaye waliotambuliwa kuwa wanachama wa chombo cha usalama chenye mfungamano na serikali—wakiwa kwenye pikipiki waliwakamata wanachama wawili wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Lebanon walipokuwa wakigawanya taarifa moja ya kulaani kuendelea kwa uvamizi wa Kiyahudi dhidi ya Lebanon na watu wake. Kukamatwa huku kulitokea jana, 17/10/2025, baada ya Swala ya Ijumaa mbele ya Msikiti wa Imam Ali katika eneo la Tariq al-Jadida jijini Beirut.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi 26 Rabi’ al-Akhir 1447 H sawia na 18/10/2025 M Anwani: “Mkanganyiko wa Serikali katika Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu na Athari Zake

Baada ya kujitenga kwa Sudan Kusini mwaka wa 2011, na Sudan kupoteza zaidi ya 75% ya mauzo yake ya nje ya mafuta, dhahabu iliibuka kama njia badali kuu ya kufidia hasara hii na kupata faida kwa fedha za kigeni. Uchimbaji madini ulikuwa umeenea sana nchini Sudan baada ya karibu mwaka wa 2008, na uzalishaji wa dhahabu wa Sudan ukawa mkubwa, na kufikia tani 73.8 mwaka wa 2024, na kushika nafasi ya tano barani Afrika. (AlJazeera.net). Hata hivyo, uzalishaji huu mkubwa haukuinufaisha serikali wala watu; uliporwa na watu binafsi, na makampuni ya kigeni na ya ndani, na hata kile kinachozalishwa kupitia uchimbaji wa jadi hununuliwa na kutolewa kimagendo na baadhi ya makampuni na mashirika. Ili kuthibitisha kile tulichosema kuhusu hili, tunahakiki migodi mikubwa zaidi ya dhahabu nchini Sudan, kwa njia ya mfano na sio kipekee, na jinsi serikali inavyoshughulikia migodi hii!

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chahitimisha Kampeni yake ya Kimataifa: “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kimeendesha kampeni ya kimataifa ya kuinua ufahamu wa kimataifa na kuleta muanga wa kimataifa kuhusu mgogoro wa kutisha wa kibinadamu uliosababishwa na mzozo nchini Sudan ambao umekuwa ukiendelea kwa miaka mitatu na nusu sasa. Mzozo huu usio na maana, kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) vinavyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (“Hemedti”), umesifiwa kama “Vita Vilivyosahaulika” kutokana na kutopokea uangaziaji wa vyombo vya habari na uangalizi wa kimataifa unaostahili.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tunafuraha kuwaalika ndugu wanahabari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza, wenye kichwa: Mkanganyiko wa Serikali Kuhusu Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu