Jumamosi, 30 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Waislamu: Kufunga Vyumba vya Ibada ni Shambulizi kwa Uislamu na Lazima Kukabiliwe kwa Upinzani Mkali, wa Pamoja wa Kisiasa

Baada ya mwelekeo hasi wa kisiasa kwenye vyumba vya ibada, idara ya Chuo Kikuu cha Copenhagen iliamua mwishoni mwa Novemba kufunga kile kinachoitwa “vyumba vya utulivu,” ambavyo Waislamu walikuwa wakivitumia kwa zaidi ya miaka ishirini, bila matatizo yoyote, na wanafunzi na wafanyikazi kuswali swala za kila siku. Uamuzi huu kwa mara nyingine tena umezua mjadala kuhusu vyumba hivi na kuhusu kama kunapaswa kuwepo na nafasi kwa Waislamu kutekeleza swala zao katika taasisi za elimu.

Soma zaidi...

Unyanyasaji wa Kimpangilio wa Kijinsia Dhidi ya Wanawake wa Sudan Hautoi Jibu lolote kwa Kukosekana kwa Dola Inayojali Heshima ya Mwanamke Mwislamu

Mnamo Alhamisi tarehe 11 Disemba, shirika, ‘The Strategic Initiative for Women in the Horn of  Africa’, liliripoti kuwa limerekodi karibu matukio 1300 ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake katika majimbo 14 nchini Sudan tangu vita vianze nchini humo mnamo Aprili 2023, huku Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vikilaumiwa kwa 87% ya visa hivi. Lilielezea unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake ukitumika kama silaha ya kimfumo katika mzozo huo, likisema “umeenea, unarudiwa rudiwa, unakusudiwa na mara nyingi unalenga”. Ubakaji ulichangia robo tatu ya matukio yaliyorekodiwa, huku visa 225 vikihusisha watoto, baadhi wakiwa na umri wa miaka 4. Matukio yalitokea majumbani, maeneo ya umma na pia yalijumuisha kizuizini cha muda mrefu cha wanawake ambao waliteswa, kubakwa na genge na ndoa za kulazimishwa. Mnamo Jumapili tarehe 7 Disemba, vikundi vya matibabu vya Sudan viliripoti kwamba watoto na wanawake kadhaa walinyanyaswa kingono na kubakwa walipokuwa wakikimbia kukamatwa kwa El Fasher huko Darfur na RSF Oktoba hii.

Soma zaidi...

Je, Vikosi vya Kiislamu vya Jeshi la Pakistan Sasa, Chini ya Uongozi wa Jenerali wa Marekani, Vitawalinda Mayahudi na Kuupokonya Silaha Upinzani wa Palestina?

Gazeti la Dawn liliripoti kwenye tovuti yake mnamo tarehe 13 Disemba, 2025 kwamba majeshi ya Waislamu huenda yakatumwa kuanzia mwezi ujao kwa ajili ya “Kikosi cha Kimataifa cha kuleta Utulivu” mjini Gaza. Hapo awali, mtawala kibaraka wa Marekani Shehbaz Sharif alikuwa tayari ametoa idhini “ya kikanuni” kwa kutumwa kwa vikosi vya Pakistan huko Gaza. Hata hivyo, wakiogopa upinzani mkali wa umma, watawala wa Waislamu mmoja baada ya mwengine wamekuwa wakionyesha kutokuwa na msaada kwao mbele ya Amerika. Hivyo sasa shetani Trump na wafuasi wake, watawala wa Waislamu, wanaunda njama mpya za kutumia vikosi vyetu vya Waislamu vya mujahid kuwalinda Mayahudi na kuwanyang'anya silaha Hamas na vikosi vyengine vya upinzani vya Palestina.

Soma zaidi...

Hukumu ya Kifo kwa Hasina: Udhalimu wa Kisekula Uliomuunda Hasina Ungalipo

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetoa hukumu ya kifo ya kihistoria dhidi ya mtawala wa Bangladesh aliyeondolewa madarakani Sheikh Hasina. Kwa watu waliokandamizwa wa Bangladesh, uamuzi huu unatoa uthibitisho wa kiishara uliochelewa kwa muda mrefu na unasimama kama shtaka lenye nguvu kwa utawala uliokanyaga ubinadamu wa kimsingi. Lakini uamuzi huu unahitaji tafakari ya kina, sio sherehe tu. Haki ya kweli inahitaji mabadiliko ya kimfumo, sio adhabu ya mtawala dhalimu tu. Chanzo kikuu ni mfumo wa kimataifa unaoongozwa na Marekani, ambao unahubiri demokrasia huku ukitekeleza ‘mantiki ya siasa za kijiografia’.

Soma zaidi...

Mauaji ya Pilkhana Yalikuwa Njama ya India ya Kudhoofisha Jeshi la Nchi hii - Ripoti Hii ya Tume Huru ya Uchunguzi ya Kitaifa Imethibitisha Ukweli ambao Hizb ut Tahrir Iliuwasilisha kwa Taifa kwa Ujasiri Miaka Kumi na Sita Iliyopita. Tunatoa Wito Ten

Tume Huru ya Kitaifa ya Uchunguzi iliyoundwa na serikali ya mpito kuhusu mauaji ya Pilkhana, na kusababisha vifo vya maafisa 57 wenye sifa nzuri, yaliyotokea katika Makao Makuu ya BDR mnamo Februari 25 na 26, 2009, imetoa ripoti yake ya uchunguzi. Uchunguzi umethibitisha kuhusika kwa Hasina na washirika wake Tapas na wengineo katika kutekeleza njama ya India ya kudhoofisha jeshi la nchi hii. Tunataka sana adhabu ya haraka kwa wahalifu hawa waliohusika katika tukio hilo na kutangazwa kwa India kama dola adui. Lazima mukumbuke kwamba chama cha kisiasa chenye busara na ikhlasi, Hizb ut Tahrir, kilikuwa cha kwanza kuleta ukweli huu kwa ujasiri kwa taifa

Soma zaidi...

‘Mkataba wa Mageuzi ya Julai: Udanganyifu Mkubwa’: Hizb ut Tahrir Yalaani Mkataba huo, na Kuhimiza Badali Msingi ya Kisiasa kwa Demokrasia Iliyofeli

Katika kujibu hotuba ya hivi karibuni ya Mshauri Mkuu Profesa Yunus kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Kitaifa wa Julai na kura ya maoni kuhusu mapendekezo ya mageuzi ya katiba katika Mkataba huo, Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh inatoa onyo kali kwamba mapendekezo ya mageuzi na mchakato wake wa utekelezaji si kitu zaidi ya hatua ya juu juu ambayo inashindwa kushughulikia sababu za msingi za mgogoro wa kisiasa wa Bangladesh. Inatoa udanganyifu wa mabadiliko ili kuhifadhi dhati ya mfumo wa kidemokrasia uliofeli.

Soma zaidi...

Jeshi la Bangladesh Lazima Likatae Kuwa Rafiki wa Wakoloni kwa Jina la kile kinachoitwa Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa na Kurudisha Hatima Yake kama Walinzi wa Ummah

Jeshi la Bangladesh linathibitisha shambulizi baya la droni kwenye kambi ya Umoja wa Mataifa katika eneo la Abyei nchini Sudan mnamo 13 Disemba 2025. Shambulizi hili liliwaua walinda amani sita wa Bangladesh na kuwajeruhi wengine wanane. Wakati huu wa kuhuzunisha moyo hauhitaji maombolezo tu, bali pia tathmini mpya muhimu ya misheni ambayo kwayo walitoa maisha yao.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Kihalifu ya Palestina, ikiwemo Wizara ya Masuala ya Wanawake, Yakimbilia Kutekeleza Miradi ya Maadui wa Uislamu ya Kuharibu Familia, Kuvunja Jamii, na Kumponda Mwanamke wa Kiislamu Anayezaa Mashujaa

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Masuala ya Wanawake ilifichua kwamba Wizara hiyo ilifanya warsha pamoja na Kamati ya Mpito ya Kuandika Katiba ili kujadili sifa za kuzifanyia kazi kwenye rasimu ya katiba na kuingiza masuala ya wanawake katika vifungu vyake. Kulingana na taarifa hiyo: “Kwa ushiriki mpana kutoka kwa taasisi rasmi na za kiserikali, taasisi za wanawake na haki za binadamu, na mashirika ya kiraia, na kwa uhudhuriaji mkubwa kutoka kwa viongozi wanawake wa Kipalestina walioko ughaibuni nchini Syria, Jordan, Lebanon, Misri, na Ulaya, Wizara ya Masuala ya Wanawake ilifanya warsha pana ya kitaifa kwa ushirikiano na Kamati ya Mpito ya Kuandika Katiba ya Palestina, kama sehemu ya kuimarisha mazungumzo ya kitaifa kuhusu kuandika katiba inayoakisi matarajio ya watu wa Palestina na kuhakikisha uwepo changamfu wa masuala ya wanawake katika maudhui yake.”

Soma zaidi...

Moyo wa Hebron na Msikiti wa Ibrahimi Wafanywa Kuwa wa Kiyahudi kwa Kufuata Hatua Zile Zile kama Ulivyofanywa kuwa wa Kiyahudi Msikiti wa Al-Aqsa

Baada ya umbile la Kiyahudi kuamua kuhamisha mamlaka ya kiidara ya Msikiti wa Ibrahimi kutoka Manispaa ya Hebron hadi “Baraza la Kidini la Kiyahudi huko Kiryat Arba,” na baada ya umbile hilo kukataa pingamizi iliyowasilishwa na Manispaa ya Hebron kuhusu uamuzi huu, pamoja na uamuzi uliofuata wa kugeuza ua wa ndani wa Msikiti wa Ibrahimi kuwa uwanja wa umma, na pamoja na vyama vya Kiyahudi vinavyofanya kazi ya kununua nyumba katika mji wa Hebron (al-Khalil) - moyo wa Mji wa Hebron, huku Msikiti wa Ibrahimi ukiwa kiini chake, unafanywa kuwa wa Kiyahudi waziwazi mbele ya ulimwengu na mbele ya Umma wa Kiislamu, kama vile eneo la Safari ya Usiku ya Mtume wake (saw) na viunga vyake linavyofanywa kuwa la Kiyahudi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu