Jumatatu, 07 Sha'aban 1447 | 2026/01/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Tanzania Yafanya Semina kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah iliyotokea mnamo Rajab 1342 H / Machi 1924 M, jana, Jumapili, 29 Rajab 1447 H / 18 Januari 2026 m, Hizb ut Tahrir / Tanzania ilifanya semina fupi katika Masjid Taqwa, Ilala Bungoni katika jiji la Dar es Salaam.

Soma zaidi...

Mwenye Hekima si Yule Anayesitasita Kati ya Mema na Maovu, Bali Yule Anayechagua Mema

Ni sababu gani za udhaifu wa Waislamu leo? Kwa nini heshima yao inavunjwa, ardhi yao inanyakuliwa, na wanamefukarishwa na kutiwa njaa, lakini hawajitetei dhidi ya dhulma, udhalilifu, na kudunishwa? Kwa nini wanatazamana wakifa kwa njaa, mauaji, na mateso mikononi mwa makafiri wahalifu bila kuinua kidole? Kwa nini wanahisi hawana msaada, dhaifu, na watiifu kwa Magharibi mbele ya majanga na vitisho vyote vinavyowapata?

Soma zaidi...

Kongamano la kila Mwaka la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon Kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon ilifanya kongamano lake la kila mwaka la kisiasa kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”, ambapo wazungumzaji kutoka Lebanon, Syria, Uturuki, na Gaza walishiriki.

Soma zaidi...

Mapendekezo ya Kongamano Lililofanywa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Kukumbuka 105 Hijri Tangu Kuvunjwa kwa Khilafah

Mnamo Jumamosi, tarehe 28 Rajab 1447 H, sambamba na tarehe 17 Januari 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan ilifanya kongamano la kumbukumbu ya miaka 105 tangu kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu ya Khilafah. Kongamano hilo lilihudhuriwa na watu mashuhuri, wakiwemo wanasiasa, watu mashuhuri wa vyombo vya habari, wasomi, na viongozi wa jamii. Kwa kuzingatia kwamba kumbukumbu hii chungu inakuja huku sisi nchini Sudan tukiteseka kutokana na vita vilivyowashwa na ubeberu wa Marekani, ikiwatumia vibaraka wake wa ndani kusambaratisha kile kilichobaki cha umoja wa nchi yetu chini ya sera yake inayoitwa “Mipaka ya Damu”. Hivyo, kichwa cha kongamano letu kilikuwa: “Sudan Kati ya Sera za Mipaka ya Damu na Kuunganisha Watu Kuwa Umma Mmoja.”

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama jijini Umdurman Vyalikamata Kundi la Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Kufuatia utekelezaji wa mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan wa visimamo vitatu katika maeneo tofauti tofauti katika jiji la Omdurman, asubuhi ya Jumatano iliyopita, 25 Rajab 1447 H, sambamba na 14/1/2026 M, ndani ya muundo wa kukumbusha tukio la kupita kwa miaka 105 tangu kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mwezi Rajab 1342 H, vyombo vya usalama viliendelea kuwakamata wanachama watano wa Hizb: Al-Radi Muhammad Ibrahim, Fadlallah Ali Suleiman, Omar Al-Bashir, Hassan Fadl, na Mujahid Adam. Kisha waliachiliwa baada ya Magharibi siku ya Jumatano baada ya nambari zao za simu kuchukuliwa na baada ya kunyakua mabango ambayo Mashababu hao wa Hizb ut Tahrir walikuwa wamebeba katika visimamo hivyo vitatu. Kisha waliitwa mnamo alasiri ya Alhamisi, 15/1/2026, na wangali wako kizuizini hadi wakati wa kuandika taarifa hii!!

Soma zaidi...

Hitimisho la Kampeni “Khilafah sio Ndoto… Bali, ni Kilio cha Ulimwengu Unaowaka Moto!”

Leo, kwa Msaada Wake, tunahitimisha kampeni ya kimataifa iliyozinduliwa na Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa maelekezo ya Amiri wa Hizb ut Tahrir, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, ambayo iliamshwa na wanaume na wanawake wa Hizb ut Tahrir kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Mikutano na Matembezi ya Kulaani Yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh: Enyi Watu! Pingeni Mpango wa Kupeleka Jeshi Letu Gaza chini ya Kikosi Kilichopendekezwa na Trump, na Takeni Msimamo Wazi kutoka kwa Wagombea katika Uchaguzi Ujao

Hizb ut Tahrir katika Wilayah Bangladesh, iliandaa mikutano na matembezi mengi ya kulaani leo, Ijumaa (16 Januari 2026), baada ya swala ya Ijumaa, katika majengo mbalimbali ya misikiti jijini Dhaka na Chattogram, dhidi ya mpango wa kupeleka vikosi vya nchi hii kwa “Kikosi cha Kuleta Utulivu wa Kimataifa” kilichopendekezwa na Trump huko Gaza. Ili kupinga mpango huu mbaya wa Marekani, na kuwataka wagombea na vyama vya kisiasa katika uchaguzi ujao kuelezea msimamo wao kuhusu suala hili.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu