Alhamisi, 11 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/05/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Ulikutana na Kiongozi (Amir) wa Makabila ya Hausa Mjini Port Sudan

Mnamo Alhamisi, 21/5/ 2026, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, Ustadh Nasser Ridha, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mratibu wa Kamati ya Mawasiliano, walikutana na Amiri wa makabila ya Hausa katika Wilayah ya Port Sudan, Ustadh Salih Abdul Rahman, nyumbani kwake.

Soma zaidi...

Msamaha Jumla; Uadilifu Nusu ni Dhulma, na Hakuwezi Kuwa na Msamaha Jumla wa Kibaguzi!

Mnamo Mei 19, 2026, tovuti ya Lebanon Debate ilichapisha kile ilichokiita toleo la mwisho lililorekebishwa la sheria ya msamaha wa jumla. Ilionekana wazi kwamba sheria hii haikuwa ya jumla, ikiwajumuisha raia wote, bali iliundwa kwa vipimo vya kimadhehebu, ubaguzi, na hesabu finyu, zisizo na uwazi. Inaonyesha mwendelezo wa enzi ya dhulma iliyowekwa na utawala wa Assad mhalifu na wafuasi wake nchini Lebanon, na mtazamo unaokataa kuhama kutoka wazo la udhalimu hadi wazo la haki na usawa. Zaidi ya hayo, ukiukwaji wa kisheria uliibuka katika kuingiliwa kwa kimabavu wakati wa uandishi wa sheria ya msamaha wa jumla! Ni chini ya kanuni gani za kisheria au mifumo ya kimataifa ambapo kitu kama hicho kipo?! Ni katika chombo hiki dhaifu tu, ambacho kinathibitisha kila siku kwamba ni mkusanyiko tu wa madhehebu ambayo nchi imeundwa, si nchi ya kawaida ambapo madhehebu huishi pamoja kama mataifa mengine, mradi tu yachague mfumo wa utawala unaoegemea msingi wa utunzaji wa haki wa raia wake, usio na ukandamizaji na unyanyasaji wa kiholela!

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mazungumzo ya Usaliti Kati ya Lebanon na Umbile la Kiyahudi

Jijini Washington, mazungumzo yalifanyika kati ya mabalozi wa Lebanon na umbile la Kiyahudi. Hii ilionekana kama mazungumzo ya kiwango cha juu cha amani, pamoja na makubaliano ya kusitisha mapigano ya siku kumi ambayo baadaye yaliongezwa hadi miezi mitatu mnamo Aprili 24, 2026. Hata hivyo, umbile la Kiyahudi linaendelea kuzidisha uchokozi wake, “jeshi la uvamizi lilitangaza kwamba lilifanya mfululizo wa mashambulizi usiku kucha likilenga zaidi ya maeneo hamsini kusini mwa Lebanon...” (Al-Jumhur, Mei 2, 2026). Je, nia, kama Trump alivyosema, ni amani kupitia nguvu? Basi watawala wa Lebanon wanawezaje kukubali mazungumzo haya ya usaliti ambayo waziwazi, na si kwa siri, yanamaanisha kupanda treni ya uhalalishaji mahusiano?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ushirika Mkuu wa Ushirikiano wa Ulinzi (MDCP) kati ya Marekani na Indonesia

Mnamo 13 Aprili 2026, Waziri wa Ulinzi wa Marekani na Waziri wa Ulinzi wa Indonesia walitangaza kuanzishwa kwa Ushirika Mkuu wa Ushirikiano wa Ulinzi (MDCP) kati ya Marekani na Indonesia. Kabla ya hili, hati ya siri kutoka Idara ya Ulinzi ya Marekani ilivuja kuhusu idhini ya safari za anga za juu za ndege za Marekani kupitia anga ya Indonesia. Je, maudhui ya makubaliano haya ni yapi na athari zake ni zipi? Athari zake ni zipi kwa uhusiano wa Indonesia na Amerika? Na athari zake ni zipi kwa uhusiano wa Indonesia na China?

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Takbira “Allahu Akbar na Sheria ni ya Mwenyezi Mungu Pekee”

Baada ya swala ya Ijumaa mnamo tarehe 5 Dhul-Hijjah 1447 H, matembezi ya Takbira (Allahu Akbar) yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu, Tunis. Umati mkubwa wa Watunisia ulishiriki, wakipiga Takbir na Tahleel (Allahu Akbar na La Ilaha illa Allah), na kuandamana kupitia barabara kuu za mji mkuu zinazoelekea Barabara ya Al-Thawra (Mapinduzi). Mabango yaliinuliwa, ikiwa ni pamoja na moja lililoandikwa, “Allahu Akbar, na sheria ni ya Mwenyezi Mungu pekee,” jengine liliandikwa, “Allahu Akbar: Uislamu ndio kitambulisho chetu na Khilafah ndio Dola yetu,” na la tatu liliandikwa, “Allahu Akbar, Uislamu ni dini yetu na njia yetu ya maisha, Khilafah ni dola yetu, na Jihad ni njia yetu.”

Soma zaidi...

Umaskini Ulioenea na wa Kimuundo Nchini Afghanistan: Matokeo ya Kufeli Kutabikisha Mfumo wa Kiuchumi wa Uislamu—Na Uendelevu wa Fikra ya Kiuchumi ya Enzi ya Jamhuri

Ripoti za hivi karibuni—ikiwa ni pamoja na ripoti ya kushtua ya BBC kutoka mkoa wa Ghor, kujichoma moto kwa mhandisi jijini Kabul, na simulizi zinazorudiwa rudiwa za watu wanaouza figo—zimefichua janga la kibinadamu linaloumiza moyo wa kila Muislamu. Katika baadhi ya miji, foleni ndefu za watu wanaotafuta kazi, njaa, na umaskini zimekuwa uhalisia unaoonekana. Wengine, wakiwa wamekandamizwa na umaskini na madeni, wamelazimika kuwauza binti zao wadogo ili kuokoa maisha ya wanafamilia wengine. Ripoti za UNDP zinaonyesha kwamba watu watatu kati ya kila wanne nchini Afghanistan hawawezi kukidhi mahitaji yao ya msingi ya maisha, na zaidi ya asilimia kumi ya idadi ya watu wako ukingoni mwa njaa.

Soma zaidi...

ACSA na GSOMIA: Watu Wenye Ufahamu na Wanasiasa Wenye Ikhlasi Wanapaswa Kujitokeza Kuilinda Nchi Isije Kuwa Nchi ya Kitumwa

Inatisha sana kwa watu wa Bangladesh, wakati vyanzo mbalimbali vinathibitisha kwamba Marekani na Bangladesh zinaendelea na mfululizo wa mikataba ya ulinzi na biashara chini ya ‘Mkataba wa Biashara wa Pamoja (ART)’ wa kikoloni. Kampeni ya Marekani ya GSOMIA ilihama kutoka fahamu dhahania hadi ramani halisi mnamo Machi 2022, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani wa wakati huo Victoria Nuland alipowasilisha rasimu ya Mkataba Mkuu wa Usalama wa Taarifa za Kijeshi (GSOMIA) ndani ya mfumo wa Mkakati wa Marekani wa Indo-Pacifiki (IPS) ulitarajiwa mnamo 2017 na kuandikwa mnamo 2019. Ingawa ziara ya Nuland ilikuwa alama muhimu kwa GSOMIA, Mkataba wa Upataji na Huduma Mtambuka (ACSA) uliinuliwa rasmi mnamo Aprili 2019 na kuitekelezwa wakati wa Mazungumzo ya 7 ya Usalama jijini Dhaka.

Soma zaidi...

Hakuna Mwisho wa Mauwaji kwa Watoto wa Palestina na Lebanon Bila Kuondolewa kwa Umbile la Kiyahudi

Mnamo tarehe 13 Mei, UNICEF iliripoti kwamba angalau watoto 59 waliuawa au kujeruhiwa nchini Lebanon katika wiki iliyopita kutokana na shambulizi la umbile la Kiyahudi nchini humo. Tangu kuanza kwa usitishaji mapigano mnamo tarehe 17 Aprili 2026, angalau watoto 23 wameuawa na 93 kujeruhiwa, na kufikisha jumla ya watoto 200 waliouawa na 806 waliojeruhiwa nchini Lebanon tangu tarehe 2 Machi. Mapema mwezi huu, iliripotiwa kwamba msichana wa miaka 12 na baba yake waliuawa huko Nabatieh baada ya Jeshi la Ulinzi la ‘Israel’ kumlenga kupitia droni kwa mashambulizi matatu ili kuhakikisha kwamba haishi.

Soma zaidi...

Pakistan yenye Nyuklia Ni Sehemu Isiyofutika ya Ummah wa Kiislamu, Yenye Uwezo wa Matokeo Katika Kiwango cha Kimataifa, Baada ya Kusimamishwa Khilafah Rashida

Kitengo cha vyombo vya habari cha vikosi vya jeshi vya Pakistan, Inter-Services Public Relations (ISPR), kilitoa taarifa kwa vyombo vya habari mnamo tarehe 17 Mei 2026, kikijibu kuwepo tishio kutoka kwa kamanda wa jeshi la Mabaniani, ambalo lilisema, “COAS ya India ilitoa taarifa ya uchochezi wakati wa mahojiano ya hivi karibuni kwamba ‘Pakistan inapaswa kuamua kama inataka kuwa sehemu ya jiografia na historia’...

Soma zaidi...

Ikiwa Serikali ya Iran Itaanguka, Je, Putin Ataipoteza Asia ya Kati?

Tangu kuanza kwa uvamizi wa kijeshi wa Marekani na umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran, mamlaka za nchi hiyo zimeonyesha azma yao na kukataa kwao kukubali matakwa ya Marekani. Iran inaendelea kufuata sera huru ya kigeni kulingana na maslahi yake. Uhusiano wake na Urusi na China unatumika kama mfano wa hili.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu