Enyi Waislamu: Kufunga Vyumba vya Ibada ni Shambulizi kwa Uislamu na Lazima Kukabiliwe kwa Upinzani Mkali, wa Pamoja wa Kisiasa
- Imepeperushwa katika Denmark
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Baada ya mwelekeo hasi wa kisiasa kwenye vyumba vya ibada, idara ya Chuo Kikuu cha Copenhagen iliamua mwishoni mwa Novemba kufunga kile kinachoitwa “vyumba vya utulivu,” ambavyo Waislamu walikuwa wakivitumia kwa zaidi ya miaka ishirini, bila matatizo yoyote, na wanafunzi na wafanyikazi kuswali swala za kila siku. Uamuzi huu kwa mara nyingine tena umezua mjadala kuhusu vyumba hivi na kuhusu kama kunapaswa kuwepo na nafasi kwa Waislamu kutekeleza swala zao katika taasisi za elimu.



