Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo (478)
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan ina furaha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio nah amu na masuala ya umma kuhudhuria kikao kipya cha kisiasa, kinachomkaribisha Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, chenye kichwa: “Dori Iliyopewa Nchi Jirani katika Vita vya Sudan”
Afisi ya Habari ya Abu Dhabi iliripoti kwamba timu maalum za kukabiliana na dharura mnamo Jumapili zilidhibiti moto uliozuka katika jenereta ya umeme iliyoko nje ya eneo la ndani la Kiwanda cha Nguvu za Nyuklia cha Barakah katika eneo la Al Dhafra, kufuatia shambulizi la droni kwenye eneo hilo, bila majeraha yoyote au uvujaji wowote wa mionzi uliorekodiwa. Wizara ya Ulinzi ya Imarati ilieleza kwamba uchunguzi bado unaendelea ili kubaini chanzo cha mashambulizi hayo, ikibainisha kuwa maendeleo yoyote yatatangazwa mara tu uchunguzi utakapokamilika.
Serikali ya Uingereza imetangaza kupelekwa kwa silaha ya gharama nafuu ya kupambana na droni katika operesheni zake za kijeshi Mashariki ya Kati. Katika taarifa yake, ilisema, “Mfumo mpya sasa umepelekwa katika kumbi za operesheni katika eneo la Mashariki ya Kati.” Pia ilisema kwamba Uingereza “itachangia kwa droni, ndege za kivita, na manuari katika misheni ya kimataifa ili kulinda Mlango-Bahari wa Hormuz.”
Waziri wa Vita na anayeitwa Waziri wa Usalama wa Kitaifa katika umbile la Kiyahudi walitangaza kuanza kwa utekelezaji wa sheria ya adhabu ya kifo kwa wafungwa wanaotuhumiwa kutekeleza mauaji. Hili lilikuja “baada ya kamanda wa Kamandi Kuu katika jeshi la uvamizi, Avi Bluth, kusaini marekebisho ya amri ya kijeshi inayohusiana na Ukingo wa Magharibi” (Raya Network). Idhini ya Knesset ya uamuzi huo haikutosha kutumia sheria hiyo kwa Ukingo wa Magharibi, ambayo haiko chini ya sheria za kiraia moja kwa moja. Marekebisho haya, yaliyotolewa chini ya amri ya kijeshi, yanaruhusu sheria hiyo kutumika ndani ya mahakama za kijeshi zinazofanya kazi katika Ukingo wa Magharibi.
Kila mwaka, zaidi ya Waislamu milioni mbili kutoka kote ulimwenguni hukusanyika katika eneo takatifu la ardhi kufanya moja ya matendo matukufu zaidi ya ibada ya pamoja: Hijja. Mahujaji hufika wakiwa wamevaa mavazi meupe ya aina moja, wakitamka maneno ya pamoja, na kufanya ibada za pamoja - ushuhuda hai wa Dini inayovuka mipaka ya utaifa, lugha, utamaduni, na hadhi ya kijamii - yote yakiwa na kusudi moja: ibada ya Mwenyezi Mungu (swt).
Nyoyo zetu zimejaa huzuni kufuatia mauaji ya kusikitisha ya Waislamu watatu katika msikiti mmoja jijini San Diego wakati wa siku takatifu za kwanza za Dhul Hijjah, miongoni mwa siku takatifu zaidi katika kalenda ya Kiislamu. Familia na jamii zinapojiandaa kwa Idd al-Adha, wakati wa ibada, kujitolea muhanga, na umoja, waumini wasio na hatia badala yake walikutana na vurugu na chuki ndani ya nyumba ya Mwenyezi Mungu (swt).
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Dua kwa Naveed Butt – Mwenyezi Mungu Amfungue Kifungo Mwake
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan ilizindua kampeni ya mitandao ya kijamii, haswa kwenye mtandao wa X (zamani ikijulikana kama Twitter), yenye kichwa “Katika Kumbukumbu ya Miaka 14 ya Kutekwa Nyara Kwake... Mwachilieni Huru Naveed Butt!” Kampeni hii inalenga kuishinikiza serikali dhalimu ya Pakistan, ambayo huduma zao za siri zilimteka nyara Mhandisi Naveed Butt, msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir nchini Pakistan, miaka 14 iliyopita mbele ya familia yake na majirani zake.
Enyi Majeshi ya Pakistan! Fursa ya dhahabu iko mikononi mwenu. Simamisheni Khilafah, unganisheni Mashariki ya Kati chini ya uongozi wenu, na ifukuzeni Amerika kutoka katika Ardhi za Waislamu. Ahadi ya Mwenyezi Mungu ya tamkini na nasr (ushindi) wake iko pamoja nanyi. Dunia iko karibu na mabadiliko makubwa. Kwa nguvu ya Iman yenu, fuateni njia ya Ansar (ra) wa Al-Madina na muregeshe nuru ya Uislamu kwa ulimwengu kupitia mfumo wake wa utawala.