Jibu kwa Mwandishi wa Makala (Usekula na Ugumu wa Historia ya Uislamu Iliyoghushiwa)
- Imepeperushwa katika Sudan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Uislamu ni itikadi ya kiroho na kisiasa ambayo ilikuja kushughulikia matatizo ya wanadamu, kwa kutambua kwamba wanadamu wana silika (ghariza) na mahitaji ya kimwili ambayo yanahitaji kushibishwa. Uislamu umebainisha jinsi mahitaji haya yanavyopaswa kukidhiwa bila ya ziada au upungufu, kupitia hukmu kutoka kwa Mwenye hekima, Mjuzi wa yote. Yeye aliyewaumba wanadamu anajua kipi kuna manufaa na kipi kina madhara kwao! Ukosefu wa elimu wa mwandishi juu ya hukmu hizi haumwondolei jukumu; badala yake, unasisitiza kutoujua kwake Uislamu.



