Badala yake, Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume Itazika Umoja wa Kiarabu na Tawala Zote za Madhara
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Rais wa Misri el-Sisi alisisitiza umuhimu wa kuimarisha mfumo wa hatua za pamoja za Waarabu na kuamsha dori ya Umoja wa Kiarabu kama "mwavuli mkuu na mfumo kamili wa kutetea maslahi ya dola za Kiarabu na Waarabu." Hii ilikuja wakati wa mapokezi yake mnamo Jumapili ya Nabil Fahmy, mgombea wa wadhifa wa Katibu Mkuu wa Umoja huo, na Ahmed Aboul Gheit, Katibu Mkuu wa sasa, ambaye muhula wake unaisha mwishoni mwa mwezi huu. El-Sisi pia alithibitisha "maono ya Misri ambayo yana nia ya kuchukua dori za kujenga ambazo zinakuza masuluhisho ya amani kwa migogoro ya eneo hilo."



