Jarida la UQAB Toleo 102 - Julai 2025
- Imepeperushwa katika Jarida la UQAB
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir Wilayah ya Kenya imechapisha toleo jipya la Jarida la UQAB kwa ajili ya mwezi wa Julai 2025 M.
Hizb ut Tahrir Wilayah ya Kenya imechapisha toleo jipya la Jarida la UQAB kwa ajili ya mwezi wa Julai 2025 M.
Mahakama ya Upeo imeamua kuwa watoto waliozaliwa nje ya ndoa na baba Waislamu wana haki ya kurithi mali ya baba yao, jambo linaloashiria maendeleo makubwa katika tafsiri ya sheria za kibinafsi za Kiislamu nchini Kenya. Hii ni baada ya Mahakama ya Juu mnamo Jumatatu tarehe 30 Juni kutupilia mbali rufaa ya Fatuma Athman Abud Faraj, ambaye alitaka kuwatenga watoto wa marehemu mumewe, Salim Juma Hakeem Kitendo, katika mali yake kwa madai kwamba walizaliwa nje ya ndoa inayotambulika ya Kiislamu.
Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."
Tangu Ijumaa, tarehe 27/6/2025, vyombo vya habari vimeripoti kuwa Rais wa Eritrea Isaias Afwerki amekubali kutoa mafunzo kwa wapiganaji elfu 50 kutoka majimbo ya Kaskazini na Mto Nile katika mafunzo ya juu ya kijeshi, kulingana na ombi lililowasilishwa na mkuu wa Jimbo la Kaskazini, Mohamed Sayed Ahmed Al-Jakoumi, mkuu wa Upande wa Kaskazini wa Makubaliano ya Juba ya Amani ya Sudan.
Al Arabiya ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 27/6/2025: "Vyanzo vinne vyenye taaarifa vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kufikia hadi dolari bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya kiraia. Vyanzo hivyo viliongeza kuwa majadiliano haya yaliendelea wiki hii baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kwamba mapendekezo kadhaa yamewsilishwa, ya awali pamoja na yaliyoboreshwa, yakiwa na kifungu kimoja kisichobadilika, kisichoweza kujadiliwa : “kukomeshwa kabisa kwa urutubishaji wa urania ya Iran.”
Muungano kati ya Pakistan, Uturuki na Azerbaijan umekuwa ukichukua umbo kwa utaratibu uliopangwa, tangu viongozi wa nchi hizo tatu walipokutana kwenye mkutano wa kilele katika msimu wa kiangazi wa 2024. Mkutano huo uliwaleta pamoja Rais wa Uturuki Erdogan, Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, na Rais wa Azerbaijan, Ilham Aliyev. Uliangazia mahusiano ya kisiasa kati ya dola hizo tatu, na kushughulikia masuala ya kikanda na kimataifa kama vile Gaza, Cyprus, Kashmir, na suala la chuki dhidi ya Uislamu.
Mnamo tarehe 16 Juni 2025, Mbunge wa Misri Diaa El-Din Dawood alipinga rasimu ya bajeti kuu ya mwaka wa fedha wa 2025/2026, akionyesha kuwa serikali inadai kupunguza deni la umma, wakati takwimu zinaonyesha kinyume chake. Alibainisha kuwa deni la ndani na nje limeongezeka kwa kiasi kikubwa tangu mwaka 2018, na kufikia jumla ya pauni trilioni 11.5 za Misri mwezi Juni 2024. Alieleza kuwa mikataba iliyotangazwa na serikali haitafsiri matokeo yanayoonekana kwa wananchi, akikosoa kuendelea kwa matumizi ya sera hizo hizo za kiuchumi. Pia alieleza kuwa mapato ya deni na malipo ya awamu pekee katika bajeti mpya yanafikia karibu pauni bilioni 4,382.6 za Misri.
Kamati ya Kuu ya Mitihani ya Cheti cha Sudan ilitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na mashirika husika kuendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Elimu na kusaidia kuwawezesha wanafunzi wote wa Sudan kufanya mitihani, hasa katika maeneo yaliyoathiriwa na vita na hali ngumu ya kibinadamu. (SUNA, Juni 26, 2025)
Kwa imani kamili juu ya qadhaa ya Mwenyezi Mungu na kutaka malipo kutoka Kwake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Jordan inaomboleza kwa kuondokewa na mmoja wa wabebaji wake wa Da’wah: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya'), ambaye alifariki dunia kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu mnamo Alhamisi, tarehe 1 Muharram 1447 H sawia na 26 Juni 2025 M, akiwa na umri wa miaka 89, baada ya kuugua kwa muda mrefu ambapo alikuwa na subira na kwa kutarajia malipo ya Mwenyezi Mungu.