Jumatatu, 12 Muharram 1447 | 2025/07/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uamuzi wa Mahakama ya Upeo Unaipa Zinaa Nafasi sawa na Ndoa

Mahakama ya Upeo imeamua kuwa watoto waliozaliwa nje ya ndoa na baba Waislamu wana haki ya kurithi mali ya baba yao, jambo linaloashiria maendeleo makubwa katika tafsiri ya sheria za kibinafsi za Kiislamu nchini Kenya. Hii ni baada ya Mahakama ya Juu mnamo Jumatatu tarehe 30 Juni kutupilia mbali rufaa ya Fatuma Athman Abud Faraj, ambaye alitaka kuwatenga watoto wa marehemu mumewe, Salim Juma Hakeem Kitendo, katika mali yake kwa madai kwamba walizaliwa nje ya ndoa inayotambulika ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Maumbile ya Mahusiano kati ya Uingereza na Urusi

Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."

Soma zaidi...

Ongezeko la Wanamgambo nchini Sudan Linasonga Kaskazini!

Tangu Ijumaa, tarehe 27/6/2025, vyombo vya habari vimeripoti kuwa Rais wa Eritrea Isaias Afwerki amekubali kutoa mafunzo kwa wapiganaji elfu 50 kutoka majimbo ya Kaskazini na Mto Nile katika mafunzo ya juu ya kijeshi, kulingana na ombi lililowasilishwa na mkuu wa Jimbo la Kaskazini, Mohamed Sayed Ahmed Al-Jakoumi, mkuu wa Upande wa Kaskazini wa Makubaliano ya Juba ya Amani ya Sudan.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran na Athari zake

Al Arabiya ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 27/6/2025: "Vyanzo vinne vyenye taaarifa vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kufikia hadi dolari bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya kiraia. Vyanzo hivyo viliongeza kuwa majadiliano haya yaliendelea wiki hii baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kwamba mapendekezo kadhaa yamewsilishwa, ya awali pamoja na yaliyoboreshwa, yakiwa na kifungu kimoja kisichobadilika, kisichoweza kujadiliwa : “kukomeshwa kabisa kwa urutubishaji wa urania ya Iran.”

Soma zaidi...

Kuibuka kwa Miungano Miwili Mipya ya Kijeshi katika Mashariki ya Kati, Caucasus, na Asia ya Kusini

Muungano kati ya Pakistan, Uturuki na Azerbaijan umekuwa ukichukua umbo kwa utaratibu uliopangwa, tangu viongozi wa nchi hizo tatu walipokutana kwenye mkutano wa kilele katika msimu wa kiangazi wa 2024. Mkutano huo uliwaleta pamoja Rais wa Uturuki Erdogan, Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, na Rais wa Azerbaijan, Ilham Aliyev. Uliangazia mahusiano ya kisiasa kati ya dola hizo tatu, na kushughulikia masuala ya kikanda na kimataifa kama vile Gaza, Cyprus, Kashmir, na suala la chuki dhidi ya Uislamu.

Soma zaidi...

Bajeti Mpya ya Misri ni Kati ya Tarakimu Zinazopotosha na Ukweli Usiokuwepo

Mnamo tarehe 16 Juni 2025, Mbunge wa Misri Diaa El-Din Dawood alipinga rasimu ya bajeti kuu ya mwaka wa fedha wa 2025/2026, akionyesha kuwa serikali inadai kupunguza deni la umma, wakati takwimu zinaonyesha kinyume chake. Alibainisha kuwa deni la ndani na nje limeongezeka kwa kiasi kikubwa tangu mwaka 2018, na kufikia jumla ya pauni trilioni 11.5 za Misri mwezi Juni 2024. Alieleza kuwa mikataba iliyotangazwa na serikali haitafsiri matokeo yanayoonekana kwa wananchi, akikosoa kuendelea kwa matumizi ya sera hizo hizo za kiuchumi. Pia alieleza kuwa mapato ya deni na malipo ya awamu pekee katika bajeti mpya yanafikia karibu pauni bilioni 4,382.6 za Misri.

Soma zaidi...

Kuna Tofauti Kubwa kati ya Utu chini ya Uislamu na Udhalilifu chini ya Ukandamizaji wa Tawala za Kitumwa

Kamati ya Kuu ya Mitihani ya Cheti cha Sudan ilitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na mashirika husika kuendelea kuunga mkono juhudi za Wizara ya Elimu na kusaidia kuwawezesha wanafunzi wote wa Sudan kufanya mitihani, hasa katika maeneo yaliyoathiriwa na vita na hali ngumu ya kibinadamu. (SUNA, Juni 26, 2025)

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya')

Kwa imani kamili juu ya qadhaa ya Mwenyezi Mungu na kutaka malipo kutoka Kwake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Jordan inaomboleza kwa kuondokewa na mmoja wa wabebaji wake wa Da’wah: Ustadh Yusuf Dhiab Al-Shalabi (Abu Diya'), ambaye alifariki dunia kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu mnamo Alhamisi, tarehe 1 Muharram 1447 H sawia na 26 Juni 2025 M, akiwa na umri wa miaka 89, baada ya kuugua kwa muda mrefu ambapo alikuwa na subira na kwa kutarajia malipo ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu