Alhamisi, 05 Rajab 1447 | 2025/12/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Utawala wa Uovu na Ghasia Utadumu kwa Muda Apendao Mwenyezi Mungu Uwepo!

Muhula wa bunge ulitarajiwa kuisha Novemba 2026, lakini rais alivunja bunge baada ya wabunge wanaounga mkono rais kuanzisha uchaguzi wa mapema wa bunge mnamo 25 Septemba. Uchaguzi ulifanyika dhidi ya mazingira ya kuzuiliwa kwa watu mashuhuri wa upinzani. Mnamo 24 Novemba wanachama wa chama cha upinzani cha Social Democratic Party Temirlan Sultanbekov na Ermek Ermatov, mwana wa rais wa zamani Kadyrbek Atambayev, na wengine walikamatwa. Zhaparov alifanya ujanja kama huo ili kuwaondoa wabunge wasiohitajika bungeni mnamo 2021.

Soma zaidi...

Kongamano la 2025 la Hizb ut Tahrir / Australia ‘Uislamu: Mabadiliko Ambayo Ulimwengu Inahitaji Sana’ Lahitimishwa kwa Mafanikio Makubwa

Hizb ut Tahrir / Australia ilikamilisha kwa mafanikio Kongamano lake la 2025 katika mazingira mazuri ya tafakari ya dhati na wasiwasi wa kweli kuhusu hali ya wanadamu na mwelekeo wake wa baadaye. Kongamano hilo lilijaa hotuba zenye hisia kali na hadhira iliyotiwa moyo na lilijumuisha ujumbe wa video unaotetemesha moyo kutoka katikati mwa Gaza iliyoharibiwa.

Soma zaidi...

Tishio la Kupiga Marufuku Hizb ut Tahrir nchini Australia

Kabla ya waathiriwa wa janga la Bondi hata kuzikwa, watetezi wanaounga mkono Uzayuni katika nchi hii walikuwa tayari wamekubaliana kuhusu simulizi yao na kuchochea orodha yao ya madai ya umma. Uchunguzi ndio umeanza tu, lakini watetezi wanaounga mkono Uzayuni katika nchi hii, wakichukua maelekezo kutoka kwa mhalifu wa kivita Netanyahu, wanasisitiza kwamba kipindi hiki chote kinaweza kuelezewa pekee kupitia jicho la chuki dhidi ya Mayahudi.

Soma zaidi...

Dola ya Kitaifa ndiyo Kikwazo Kikubwa Zaidi katika Kulinda Heshima na Maisha ya Waislamu Iwe nchini India au Gaza

Waziri wa Mambo ya Nje na Naibu Waziri Mkuu Ishaq Dar alilaani vikali tukio ambapo Waziri Mkuu wa Bihar Nitish Kumar alivua hijabu ya mwanamke wa Kiislamu Nusrat Parveen katika hafla ya serikali, akilitaja kuwa ‘la kuchukiza sana’. Dar alielezea tukio hilo kama la aibu, akisema lilionyesha haja ya haraka ya kulinda haki za wachache na kupunguza wimbi linaloongezeka la chuki dhidi ya Uislamu.

Soma zaidi...

Ukandamizaji Unaoongezeka wa Marekani dhidi ya Mashirika ya Kiislamu - Toleo la Texas

Katika hatua ya kushangaza wiki hii, Gavana wa Texas Greg Abbott alitangaza Baraza la Mahusiano ya Kiislamu na Kiamerika (CAIR) na Ikhwan al-Muslimin kama “mashirika ya kigaidi ya kigeni.” Tangazo lake linaharamisha makundi haya kumiliki mali huko Texas na kuidhinisha hatua za kisheria za serikali dhidi ya vyama vinavyohusiana nayo. Ingawa Abbott aliweka uamuzi huo kama msimamo dhidi ya “misimamo mikali,” hatua hiyo inawakilisha ongezeko kubwa la ulengaji unaoendelea wa mashirika ya Kiislamu na inaangazia mgogoro mkubwa wa uhuru wa kuzungumza, ukandamizaji wa serikali, na unafiki katika jinsi Amerika inavyowatendea raia wake Waislamu.

Soma zaidi...

Kifo cha Imam Fouad Saeed Abdulkadir: Pindi Hifadhi Inapogeuka Kuwa Mkasa

Idara ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) imethibitisha kifo cha Fouad Saeed Abdulkadir, raia wa Eritrea mwenye umri wa miaka 46, ambaye alifariki tarehe 14 Disemba akiwa kizuizini mwa ICE katika Kituo cha Ushughulikiaji cha Moshannon Valley huko Pennsylvania. Kulingana na ICE, Imam Abdulkadir anaripotiwa kupata maumivu ya kifua na kupokea uangalizi kutoka kwa wafanyikazi wa matibabu na huduma za matibabu za dharura. Kifo chake, mojawapo ya vifo kadhaa vilivyoripotiwa katika vituo vya ICE, bado kinachunguzwa na kimeongeza uchunguzi wa hali za uzuizi na upatikanaji wa huduma za afya za kutosha kwa wafungwa.

Soma zaidi...

Kipindi cha Tarique Rahman: Purukushani ya Kisiasa Kutoka kwa Mfumo wa Kisekula Uliovunjika

Huku Bangladesh ikiingia katika awamu muhimu ya kabla ya uchaguzi, kutangazwa kwa kurudi kwa Tarique Rahman, mwana wa Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh Khaleda Zia na kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Kizalendo cha Bangladesh (BNP), kumesababisha wimbi linalotabirika la umaarufu inaozingatia shakhsiya ya mtu. Simulizi hii, iliyokuzwa kwa ukali na chama chake, inamwakilisha kama suluhisho la pekee kwa changamoto za taifa. Lazima tuone hili kwa jinsi lilivyo: udanganyifu mkubwa wa kisiasa ambao unaficha kwa hatari uhalisia msingi wa mamlaka na mfumo wa leo.

Soma zaidi...

Taarifa ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari Wenye Kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan Unazidisha Majeraha na Kugawanya Nchi”

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Muawiya Othman, kufuatia ziara ya Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Utawala na Kamanda wa Jeshi, Luteni Jenerali Burhan, nchini Saudi Arabia, Muawiya alisema mnamo Jumatatu jioni, 15/12/2025: “Rais alielezea shukrani zake kamili kwa azimio la Rais wa Marekani Donald Trump la kushiriki katika juhudi za kufikia amani na kukomesha vita nchini humo, kwa ushiriki wa Ufalme wa Saudi Arabia. Mheshimiwa alithibitisha nia ya Sudan kufanya kazi na Rais Trump, Waziri wake wa Mambo ya Nje, na Mjumbe wake Maalum wa Amani nchini Sudan, ili kufikia lengo hili zuri bila shaka.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu