Jumamosi, 21 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/13
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mtihani wa Gaza

Mwenyezi Mungu (swt) hakumuumba mwanadamu bila ya kuweka mbele yake mitihani kulingana na ukubwa wa Imani yake na kujitolea kwake katika Dini, ili Mwenyezi Mungu (swt) apate kujua ni nani atakayekuwa na subira mbele ya mitihani hiyo na kuweka tegemeo lake (tawakkul) kwa Mwenyezi Mungu (swt) . Haya ni ili Mwenyezi Mungu (swt) amuepushe na fitna. Ama wale ambao watafeli ndani ya mitihani hiyo, watafeli tu kwa sababu ya hukumu yao mbaya, kughafilika kwao na Amri za Mwenyezi Mungu (swt), na Imani yao dhaifu.

Soma zaidi...

Swahaba Mtukufu Mus’ab ibn Umair, Mwenyezi Mungu (swt) Amuwie Radhi

Katika kundi la majina yenye kung'aa ya maswahaba watukufu, jina la Mus’ab bin Umair (ra) linajitokeza kama ishara ya muhanga na uthabiti. Mus’ab alikuwa mshika mwenge wa Da’wah katika hatua zake zote, kwani alikuwa ni kijana miongoni mwa vijana bora wa Makka, aliyejulikana kwa uzuri wake, harufu ya kupendeza, na maisha ya anasa, kiasi kwamba Maswahaba, Mwenyezi Mungu (swt) awawie radhi wote, wakasema juu yake, ما رأينا بمكة أحدا انعم عيشا من مصعب بن عمير “Hatujamuona mtu yeyote mjini Makka ambaye aliishi kwa neema kuliko Mus’ab bin Umair.”

Soma zaidi...

Masharti ya Ufahamu wa Kisiasa na Uundaji wa Sera (Sehemu ya 3) Dori ya Ramani katika Ufahamu wa Kisiasa

Maelezo yanayohusiana na ramani hayaishii tu katika kujua eneo la nchi ambayo tukio mahususi linalochunguzwa linahusiana. Badala yake, inapanuka hadi kuelewa eneo la nchi kwenye ramani, asili ya jiografia inayohusiana na nchi, asili ya mipaka yake, mafungamano yake na bahari, mafungamano yake na vipengee muhimu vya kijiografia, na kufahamu hali ya ya watu kulingana na idadi ya watu, msongamano wa watu, asili na sifa za idadi ya watu, na umiliki wake wa nishati na teknolojia.

Soma zaidi...

Harakati ya Taliban na Fursa ya Kusimamisha Khilafah

Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu