Udhalimu wa Watawala Wakandamizaji Unaweza Kukomeshwa Tu Kupitia Mabadiliko Msingi
- Imepeperushwa katika Iraq
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tangu Jumamosi iliyopita, mkoa wa Erbil umekuwa ukishuhudia mvutano wa kiusalama kufuatia maandamano ya makabila ya Herki katika wilaya ya Khabat, yakikituhumu Chama cha Kidemokrasia kwa kukaidi ahadi zake za kuwapa viti vitatu bungeni kwa badali ya kabila hilo kuwapa kura zao katika uchaguzi. Maandamano hayo kisha yakageuka kuwa mapigano kati ya makabila ya Herki na vikosi vya usalama, na kusababisha vifo na majeraha. Katika tukio muhimu, kabila hilo lilitangaza uhamasishaji wa jumla huko Erbil, na waandamanaji wakachoma makao makuu ya Chama cha Kidemokrasia cha Kurdistan katika wilaya hiyo leo, Jumatatu.



