Jumanne, 01 Rabi' al-thani 1447 | 2025/09/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kukabiliana na Mayahudi ni jambo la Aqidah. Kujitayarisha kwa ajili yake Ni Faradhi ya Shariah, na Kuliepuka ni Maangamivu

Baadhi ya wanasiasa wa Syria hivi majuzi wamekuwa wakiendeleza wazo kwamba “hatutauza udanganyifu kwa watu wetu, na kwamba lazima tuchukue hatua ya kweli ili kujenga upya serikali.” Hili linafanywa kwa kisingizio kwamba “tunafahamu uwezo wetu wa kweli, na lugha ya vitisho haitakuwa na manufaa yoyote katika kukabiliana na uvamizi wa Kizayuni,” na kwamba “mazungumzo nao yanaendelea ili kuregea kwenye makubaliano ya 1974!”

Soma zaidi...

Maandamano ya Umwagaji damu nchini Indonesia na Chanzo Chake

Tangu tarehe 25 Agosti, 2025, Indonesia imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano makubwa yaliyorekodiwa katika maeneo 107 katika mikoa 32. Huku baadhi ya maandamano yakiendelea kuwa ya amani, mengi yalizidi kuwa ghasia zilizohusisha uharibifu na uchomaji moto. Maeneo kadhaa yalishuhudia machafuko makubwa zaidi, ikiwemo mji mkuu Jakarta, Java ya Kati, Java Mashariki, Java Magharibi, Yogyakarta, Sumatra Kaskazini, Nusa Tenggara Magharibi, Sulawesi Kusini, na Kalimantan Magharibi. Vituo vya umma, afisi za serikali, na hata mali za usalama wa taifa zilipata uharibifu mkubwa. Jijini Jakarta, kwa mfano, vituo 22 vya mabasi ya TransJakarta na vituo vya treni ya chini ya ardhi vya MRT viliharibiwa, huku hasara ikikadiriwa kuwa karibu rupiah bilioni 50.4 za Indonesia.

Soma zaidi...

Matukio ya Kisiasa ya Hivi Majuzi nchini Yemen Yanaonyesha Nini?

Mnamo Alhamisi, 28 Agosti, Waziri Mkuu wa Wizara ya Mabadiliko na Ujenzi, Ahmed Ghaleb Al-Rahwi, aliuawa, pamoja na mawaziri wengine tisa: Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu Mujahid Ahmed Abdullah Ali; Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji Moeen Hashim Ahmed Al-Mahaqri; Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji Radwan Ali Ali Al-Rubai; Waziri wa Mambo ya Nje na Wageni Jamal Ahmed Ali Amer; Waziri wa Umeme, Nishati na Maji Ali Seif Mohammed Hassan; Waziri wa Utamaduni na Utalii Ali Qasim Hussein Al-Yafei; Waziri wa Masuala ya Jamii na Leba Samir Mohammed Ahmed Bajaala; Waziri wa Habari Hashim Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din; na Waziri wa Vijana na Michezo Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid. Mawaziri wengine kadhaa bado wako katika hali mbaya na ya wastani, akiwemo Jalal Al-Ruwaishan, Naibu Waziri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi na Usalama. Umbile la Kiyahudi limeeleza kuwa lilifanya shambulizi hilo, likiwalenga Waziri wa Ulinzi Mohammed Al-Atifi na Mkuu wa Majeshi Mohammed Abdul Karim Al-Ghamari.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan kutibua mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Ummah ni suala nyeti, ambalo ni lazima hatua za uhai au kifo zichukuliwe, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi’ al-Awwal 1447 H, sawia 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa Kuhifadhi Qur'an. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, maulamaa, maafisa na wanajeshi, na wengineo, wakiwataka watimize wajibu wao wa Shariah wa kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Upenyaji wa Mayahudi wa Jeshi la Misri

Tangu serikali ya Misri itie saini Makubaliano ya Camp David mwaka 1979, jeshi la Misri limeingia katika njia ya utegemezi na upenywaji, likijitenga na kanuni yake ya awali ya kuulinda Ummah na kulinda mipaka yake dhidi ya maadui wake wa kweli, wa kwanza miongoni mwao ni Mayahudi walioinyakua Palestina. Hatua kwa hatua, taasisi hii imebadilika na kuwa chombo kilichozuiliwa, chini ya masharti ya adui, hata kushiriki katika kuilinda na kuiwezesha kupitia mikataba ya kijeshi, usalama, kiuchumi, na ushauri ambayo iliunda utaratibu kamili wa ushawishi wa Kiyahudi, ndani ya jeshi na dola.

Soma zaidi...

Tofauti Kubwa Kati ya Azimio la Istanbul na Fatwa Zilizotangulia!

Mwishoni mwa kongamano lao waliloliita “Gaza ni Jukumu la Kiislamu na la Kibinadamu” lililofanyika jijini Istanbul kwa siku sita la maulamaa, lililoandaliwa na Erdogan, walitoa tamko la mwisho. Walianza na aya za Qur’an kuhusu maandalizi na Jihad katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt), ili kwamba yeyote anayeisoma afikirie kwamba kitakachofuata kingekuwa ni programu ya kivitendo ya jinsi ya kujishughulisha mara moja na Jihad ambayo sio tu inaiondolea Gaza bali pia inaikomboa Palestina na al-Masjid al-Aqsa. Hata hivyo, uhalisia ulikuwa kinyume.

Soma zaidi...

Utegemezi wa Dola za Kikoloni za Kikafiri Humpora Mtu Utashi wa Kisiasa, Hupotosha Dira ya Mtu na Kupoteza Nguvu za Mtu

Kwa kuzingatia ukandamizaji unaoendelea Syria kwa matakwa ya Amerika na mfumo wa kimataifa, watu wanahisi wameporwa utashi wao, kukosa uwezo wa kufanya maamuzi yao wenyewe, na kuhofia mustakabali wao. Ili kuelewa ni nani anayeamua mambo nchini Syria na kwa nini tumepoteza uwezo wetu wa kufanya maamuzi, lazima tuhakiki mkondo wa mapinduzi ya Syria tangu mwanzo wake.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu