Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 605
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hakika, sisi katika familia ya Gazeti la Ar-Rayah tunatoa pongezi zetu za dhati kwa Ummah wetu wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Tunamwomba ﷻ aifanye Idd hii kuwa mwanzo wa kheri na baraka kwetu, ili Idd ijayo ije huku tukiishi chini ya heshima, ushindi, na tamkini, tukiwa tumehifadhiwa chini ya bendera ya Khilafah Rashida bendera ya (لا إله إلا الله محمد رسول الله) “La ilaha illa Allah, Muhammadur Rasul Allah” “Hakuna mungu wa haki ila Mwenyezi Mungu, Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Na hilo si gumu kwa Mwenyezi Mungu ﷻ. Mtume wa Mwenyezi Mungu (ﷺ) amesema, «... ثُمَّ تَكُونُ مُلْكاً جَبْرِيَّةً فَتَكُونُ مَا شَاءَ اللَّهُ أَنْ تَكُونَ ثُمَّ يَرْفَعُهَا إِذَا شَاءَ أَنْ يَرْفَعَهَا ثُمَّ تَكُونُ خِلَافَةً عَلَى مِنْهَاجِ النُّبُوَّةِ» “…Kisha kutakuwa na utawala wa dhulma, na utabakia kwa muda anaotaka Mwenyezi Mungu uwe kisha atauondoa anapotaka kuuondoa. Kisha itakuwepo Khilafah kwa Njia ya Utume.”