Hasira ya Watu wa Gaza kutoka Ng'ambo za Bahari Inataka Mzingiro Uvunjwe... Watu wa Misri na Jeshi lake Watakasirika Lini? Lini Hasira yao Itakuwa Moto wenye Kuteketeza Umbile la Kiyahudi na Tawala za Mamluki Zinazolilinda?
- Imepeperushwa katika Misri
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Wakati Gaza ikiwa inakufa kwa njaa, ikizingirwa kwa kimya cha aibu cha Waarabu na njama ya wazi ya kimataifa, kijana mmoja wa Kimisri kutoka ng'ambo, Anas Habib, alifunga milango ya ubalozi wa Misri nchini Uholanzi na kumwaga unga kwenye kizingiti chake. Alipiga kelele kwa jina la watu waliozingirwa wa Gaza na kuliita jeshi lake nchini Misri kuvunja mzingiro, kufungua kivuko, na kumaliza njaa ya kupangwa... Kilio kutoka nchi ya mbali kilisikika ndani ya nyoyo huru. Je, kuna yeyote kati ya watu wa Misri atakayejibu? Je, kuna ulinzi wowote katika nyoyo za watu wa jeshi la Kinana? Au kufuli zilizowekwa kwenye ubalozi wa Misri jijini The Hague ni za kikatili kidogo kuliko kufuli zilizowekwa kwenye utashi na silaha zao?!