Jumamosi, 28 Rajab 1447 | 2026/01/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria Kongamano kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Kuvunjwa Khilafah katika Hoteli ya Al-Busayri Plaza

Kwa mnasaba wa tukio la kupita miaka 105 ya hijriya tangu kuvunjwa kwa Dola ya Waislamu, Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H, na kama mwendelezo wa kuwakumbusha Waislamu faradhi ya kufanya kazi ya kuiregesha kama Dola ya Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan yatoa heshima kukualikeni kuhudhuria kongamano lenye kichwa: “Sudan Kati ya Sera ya Mipaka ya Damu na Sera ya Kuwaunda Watu Kuwa Ummah Mmoja”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Visimamo Kadhaa katika Miji Tofauti Tofauti kote nchini Sudan

Ndani ya muundo wa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mnamo Rajab 1342 H, na kama ukumbusho kwa Ummah wa tukio hili chungu, si kwa lengo la kulia juu ya historia tukufu iliyopotea, bali ili kuchochea azma ili Ummah uweze kutimiza wajibu wake wa kusimamisha Khilafah ili kuishi chini ya sheria za Mola wa Mlezi Walimwengu na kuondoa dhambi ya kifo cha Jahiliyyah kutoka shingoni mwake, Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan walifanya matembezi kadhaa katika miji tofauti kote Sudan, kufuatia swala ya Ijumaa mnamo 20 Rajab 1447 H, sawia na 9 Januari 2026 M

Soma zaidi...

Mkutano na Hotuba katika Mji wa El Obeid

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, wanachama wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano na hotuba ya hadhara katika mji la El Obeid, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini, mnamo Jumatano, 18 Rajab 1447 H, sambamba na 7 Januari 2026 M, katika uwanja wa Msikiti wa Soko la Al-Salihin.

Soma zaidi...

Kuhutubia Umma katika Mji wa Al-Ubayyid kama Sehemu ya Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Wanachama wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika mji wa Al-Ubayyid walitoa hotuba ya hadhara mnamo siku ya Ijumaa, 13 Rajab 1447 H, sawia na 2 Januari 2026 M, kufuatia swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Soko la Karima Kaskazini. Ustadh Ahmed Wada’a Abdul Karim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumza, akielezea kwamba hakuna heshima au usalama isipokuwa chini ya Khilafah. Kisha akahutubia ujumbe kwa wale walio katika nyadhifa za mamlaka na ushawishi, wasomi, wanasiasa, na wanahabari, akiwahimiza kusimama na kufanya kazi ili kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah... Dunia Inajitayarisha Kurudi Kwake

Mtu anaweza kufikiri, huku akiangalia yanayojiri hivi karibuni katika ngazi ya kimataifa na katika ardhi za Kiislamu, kwamba uhalisia unazidi kuwa wa giza tororo kwa Umma wa Kiislamu, na kwamba matumaini ya kuamka kwake na kuregeshwa kwa heshima yake yanafifia au kupungua. Hata hivyo, kutafakari haya yanayojiri kunaonyesha kwamba yanafichua matumaini ambayo yanajajidishwa na kuzidi kuwa makubwa, na mbinu ya kuelekea mwamko siku baada ya siku.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Yafanya Mikutano Kadhaa katika Miji mbalimbali nchini Sudan

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, mnamo Rajab 1342 H, na kuukumbusha Ummah kuhusu tukio la kusikitisha lililosababisha Ummah kumpoteza Imam wake, ngao, umoja wake kuvunjika, na kafiri mkoloni kuutawala, kudhibiti maamuzi yake ya kisiasa, kiuchumi, na kijeshi, na kuhamasisha Ummah kufanya kazi ya kuregesha maisha kamili ya Kiislamu kupitia kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume

Soma zaidi...

Kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105, Tunaufufua Wito kwa Majeshi Yote ya Ummah Kuhamasisha Nguvu Zao Ili Kusimamisha Khilafah Rashida

Mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na tarehe 3 Machi, 1924 M, amri ovu ilitolewa na lile lililoitwa Bunge Kuu la Kitaifa, ikielezea kufutwa rasmi kwa Khilafah. Kwa kuvunjwa kwa Khilafah, hukmu za Sharia ziliondolewa, kiapo cha utiifu (Bay’ah) kilisitishwa, na ardhi za Waislamu zilichanwa vipande vipande kwa misingi ya kitaifa na kikabila kuwa vijidola tete, tegemezi, na dhaifu. Vibaraka wa kulipwa waliteuliwa kuzitawala. Fikra ya umoja ilipigwa pigo kubwa. Kwa kuangamia kwake, Bayt al-Maqdis na Ardhi Iliyobarikiwa zilianguka, na umbile lenye saratani la Kiyahudi lilipandwa katikati ya ardhi za Waislamu.

Soma zaidi...

Pindi Uwakilishi Unapokuwa Badali ya Wahyi

Kuapishwa kwa Zohran Mamdani mnamo tarehe 1 Januari 2026, kama wengi kabla yake, kunasherehekewa kama hatua muhimu kwa “uwakilishi wa Waislamu” ndani ya demokrasia ya Magharibi. Hata hivyo, zaidi ya siasa za nembo na utambulisho kuna swali zito zaidi, ambalo linagusa msingi wa itikadi ya kisiasa ya Uislamu: Je, inaruhusiwa kwa Muislamu kushikilia wadhifa wa utunzi wa sheria?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah (Rajab 1342 - Rajab 1447 Hijri)

Sisi katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan tunafuraha ya kuwakaribisha wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wenye hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Umma cha kila mwezi, ambacho mwezi huu kitakuwa na kichwa: Khilafah Ilivunjwa, na Afya ya Watoto Wetu Ikakiukwa

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafurahi kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo mgeni atakuwa ni Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil) – Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan – chenye kichwa: Kwa Mnasaba Kumbukumbu ya Kuvunjwa kwa Khilafah (Ukhalifa): Kusimamishwa kwake tena ni Faradhi ya Sharia

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu