Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 566
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa mara nyengine tena, Amerika inafichua kiburi chake mbele ya ulimwengu. Onyo la Donald Trump kwamba “mambo mabaya yatatokea” isipokuwa Afghanistan ikabidhi Kambi ya Anga ya Bagram inaakisi sauti ile ile ya kibeberu ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikifafanua sera ya Marekani kwa ardhi za Waislamu. Maneno kama haya sio lugha ya dola huru zinazoamiliana kwa usawa, bali ni maagizo ya mkoloni ambaye anaziona ardhi za Waislamu kama kituo cha kijeshi kwa ajili ya matamanio yake. Hii ndiyo hali halisi ya siasa za Magharibi: ushurutishaji, vitisho, na kudharau ubwana wa nchi zetu.
Mnamo Septemba 2025, “Israel” ilishambulia Doha, na kuua viongozi wa Hamas na mlinzi wa Qatar. Gazeti la ‘The Independent’ liliripoti kuwa Trump alikasirika kwa sababu Netanyahu alimfahamisha katika dakika za mwisho tu – “He's f***ing me” – huku vyanzo vya “Israel” badala yake vilizungumza kuhusu “idhini” ya Trump.
Tangu 1945 kumekuwa na angalau nchi mpya 34 ambazo zimetambuliwa na Umoja wa Mataifa. Hili lilitokana na wimbi la utaifa ambalo lilienea kote ulimwenguni kwa miongo kadhaa tangu katikati ya miaka ya 1900. Mipaka ya kindoto ilichorwa ili kutoa uhuru kwa makundi mbalimbali na haki ya kutawala, kwani nchi kama vile Sudan iliyoungana hapo awali zilitumbukia ndani ya mizozo na machafuko.
Miaka miwili baada ya mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kizayuni katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, likiungwa mkono kikamilifu na Marekani, NATO, na washirika wao makruseda, Umoja wa Mataifa na dola zenye nguvu duniani wamejibu kwa kulituza umbile hilo. Utambuzi wa “Dola ya Palestina” unakuja huku Gaza ikivuja damu, na baada ya dola 150+ tayari kutoa utambuzi sawia.
Huko Turkestan Mashariki, kina mama wanakamatwa, watoto wanatenganishwa na familia zao, na wasichana wenye umri mdogo wanafungwa kizazi... Katika Turkestan Mashariki, kundi la watu linachinjwa na kuangamizwa kimya kimya (Shirika la Habari la Turkestan Mashariki, 12/9/2025)
Uislamu ni dini ya haki ya Mwenyezi Mungu, ujumbe wa mwisho wa wahyi wa Mwenyezi Mungu na haki pekee ya kweli. Sheria na itikadi zengine zote duniani leo ni ya batili na potofu. Dini hii imekamilika katika sheria zake, inadhamini uadilifu kamilifu, rehma kamilifu, uongofu kamili, heshima kamilifu, na utumwa kamili kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu inatoka kwa Mwenyezi Mungu peke yake.
Kuondolewa kwa Mkataba wa Kijamii wa Nieuw (BMT) kutoka kwa serikali kuliwasilishwa haraka kwenye vyombo vya habari kama hatua ya kikanuni. Kana kwamba upande huo hatimaye ulivunja sera kwa sababu ya mateso ya kutisha ya Wapalestina mjini Gaza. Lakini hiyo ni dhana potofu. Kuondoka kwao sio dhihirisho la chukizo la kimaadili, bali ni hesabu za kisiasa. Haitoi BMT nje ya mradi wa kikoloni unaoitwa “Israel”, lakini inaonyesha jinsi wao pia wamenaswa kwa kina ndani yake.
Dola nyingi zaidi za Magharibi zinawasilisha wito wa suluhisho la dola mbili kama hatua ya kimaadili na ya haki. Lakini wale wanaotazama nyuma ya pazia wanaona kuwa halina uhusiano wowote na huruma kwa Wapalestina au utambuzi wa “haki yao ya uhuru”. Kinyume chake: ni hatua ya dharura ya kisiasa, inayoendeshwa na shinikizo kutoka kwa watu wao wenyewe na hasara inayokuja ya uhalali wa umbile la Kizayuni.
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir nchini Australia inaomboleza kifo cha mmoja wa watu ambaye mapenzi yake kwa Quran, Waumini na Dawah yaliwagusa watu wengi katika jamii (Mwenyezi (swt) amrehemu): Ndugu Khaled Ahmed Ibrahim Trad (Abu Muhammad)