Watawala wa Pakistan wanaogopa mwamko wa Kiislamu unaoongezeka miongoni mwa Waislamu wa Pakistan na, kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Utendakazi, wanajaribu—bila mafanikio—kuusimamisha kwa kuigeuza Pakistan kuwa “dola ngumu zaidi.”
- Imepeperushwa katika Pakistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mwenendo mkali na wa kikatili wa watawala dhidi ya mkutano wa TLP umesababisha mawimbi ya wasiwasi katika duara za kidini za Pakistan na kumshangaza kila Muislamu mwenye ufahamu. Hata hivyo, mbinu hii ya kiimla ya watawala wa Pakistan si kitendo cha pekee au kisicho cha kawaida; bali ni sehemu ya msururu wa hatua mfululizo ambazo watawala wamechukua katika siku za hivi karibuni, hatua zilizozidi wakati watawala wa Pakistan walipokubali kutekeleza mpango wa Trump pamoja na watawala wa nchi za Kiarabu na zengine za Kiislamu, mpango ambao lengo lake ni kulinda uwepo wa Mayahudi kutokana na upinzani wa Waislamu wa Palestina.



