Ijumaa, 18 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ummah Unahitaji Khilafah Kulinda Matukufu Yake Sio Mikataba ya Ulinzi ya Kuwalinda Watawala Vibaraka

Pakistan na Saudi Arabia zimeingia katika makubaliano ya kihistoria ya ulinzi wa pande zote, ambapo uvamizi wowote dhidi ya dola moja utachukuliwa kuwa shambulizi kwa pande zote mbili. ‘Mkataba wa Kimkakati wa Ulinzi wa Pamoja’ ulitiwa saini na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif na Mfalme Mtarajiwa wa Saudia Mohammad Bin Salman katika Kasri la Al-Yamamah jijini Riyadh mnamo Jumatano, 17 Septemba 2025.

Soma zaidi...

Kwa Uislamu, Watu wa Sudan Wanayeyushwa ndani ya Chungu Kimoja, na Wanaishi Maisha yenye Staha na Haki Chini ya Dola Yake

Idadi ya watu wa Sudan inakadiriwa kufikia milioni 49.4, kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) mwaka 2024. Asilimia tisini na sita ya wakaazi wote ni Waislamu, huku jamii ndogo ya Wakristo na watu binafsi wakifuata dini za kipagani. Jamii ya Wasudan inaundwa na makabila ya asili ya Waarabu, Waafrika, na Wanubi, yakiwakilisha zaidi ya makabila 500. Waarabu wanaunda kabila kuu, linalojumuisha 70% ya idadi ya watu, pamoja na makabila mengine, yakiwemo Beja, Nuba, Fulani, Geberti, Fur, Masalit, na mengineyo.

Soma zaidi...

Khilafah pekee ndio inayojali Maslahi ya Watu na ndio Mlinzi wa Haki na Mahitaji yao

Hali mbaya ambayo Sudan imefikia kufuatia vita vya kikatili vilivyoanza miaka miwili iliyopita kati ya vikosi vya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka sio siri. La kusikitisha, watu wasio na hatia wa Sudan wamelipia, na wanaendelea kulipia, gharama ya mzozo huu mbaya wa kimataifa unaoendeshwa na silaha za ndani kwa lengo la kuichana nchi na kulinda maslahi ya Amerika, Ulaya, na wengineo!!

Soma zaidi...

Operesheni ya Shujaa Aliyeuawa Shahidi Abdul Muttalib Al-Qaisi Inathibitisha Azma ya Ummah Kupambana na Mayahudi hadi Watakapotokomezwa, Licha ya Watawala wa Kiarabu Kushindwa

Jana, 10 Septemba 2025, kamanda wa Kamandi Kuu ya jeshi la umbile la Kiyahudi alitangaza kuundwa kwa kitengo kipya cha kijeshi, kinachoitwa “Kitengo cha Gilead,” katika Bonde la Jordan, kitakacho kaa kwenye Bonde la Jordan. Kitengo hichi cha kikanda kina jukumu la kulinda mipaka ya mashariki ya Mayahudi katika Bonde la Jordan na Bahari ya Dead. Aliashiria kuwa kuanzishwa kwa kitengo hicho kunajiri ndani ya muundo wa kile alichoelezea kama “masomo ya kujifunza kutokana na kushindwa kugumu kwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.” Uundaji huu mpya unakuja baada ya vitisho vya viongozi wa umbile la Kiyahudi kupanuka hadi nchini Jordan na kwengineko chini ya mwavuli wa mradi wa “Israel Kubwa”, uliotangazwa na Netanyahu, uliobarikiwa na Trump, na kutangazwa wazi na Smotrich, Waziri wa Fedha wa umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Matukio ya Kisiasa ya Hivi Majuzi nchini Yemen Yanaonyesha Nini?

Mnamo Alhamisi, 28 Agosti, Waziri Mkuu wa Wizara ya Mabadiliko na Ujenzi, Ahmed Ghaleb Al-Rahwi, aliuawa, pamoja na mawaziri wengine tisa: Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu Mujahid Ahmed Abdullah Ali; Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji Moeen Hashim Ahmed Al-Mahaqri; Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji Radwan Ali Ali Al-Rubai; Waziri wa Mambo ya Nje na Wageni Jamal Ahmed Ali Amer; Waziri wa Umeme, Nishati na Maji Ali Seif Mohammed Hassan; Waziri wa Utamaduni na Utalii Ali Qasim Hussein Al-Yafei; Waziri wa Masuala ya Jamii na Leba Samir Mohammed Ahmed Bajaala; Waziri wa Habari Hashim Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din; na Waziri wa Vijana na Michezo Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid. Mawaziri wengine kadhaa bado wako katika hali mbaya na ya wastani, akiwemo Jalal Al-Ruwaishan, Naibu Waziri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi na Usalama. Umbile la Kiyahudi limeeleza kuwa lilifanya shambulizi hilo, likiwalenga Waziri wa Ulinzi Mohammed Al-Atifi na Mkuu wa Majeshi Mohammed Abdul Karim Al-Ghamari.

Soma zaidi...

Kukabiliana na Mayahudi ni jambo la Aqidah. Kujitayarisha kwa ajili yake Ni Faradhi ya Shariah, na Kuliepuka ni Maangamivu

Baadhi ya wanasiasa wa Syria hivi majuzi wamekuwa wakiendeleza wazo kwamba “hatutauza udanganyifu kwa watu wetu, na kwamba lazima tuchukue hatua ya kweli ili kujenga upya serikali.” Hili linafanywa kwa kisingizio kwamba “tunafahamu uwezo wetu wa kweli, na lugha ya vitisho haitakuwa na manufaa yoyote katika kukabiliana na uvamizi wa Kizayuni,” na kwamba “mazungumzo nao yanaendelea ili kuregea kwenye makubaliano ya 1974!”

Soma zaidi...

Maandamano ya Umwagaji damu nchini Indonesia na Chanzo Chake

Tangu tarehe 25 Agosti, 2025, Indonesia imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano makubwa yaliyorekodiwa katika maeneo 107 katika mikoa 32. Huku baadhi ya maandamano yakiendelea kuwa ya amani, mengi yalizidi kuwa ghasia zilizohusisha uharibifu na uchomaji moto. Maeneo kadhaa yalishuhudia machafuko makubwa zaidi, ikiwemo mji mkuu Jakarta, Java ya Kati, Java Mashariki, Java Magharibi, Yogyakarta, Sumatra Kaskazini, Nusa Tenggara Magharibi, Sulawesi Kusini, na Kalimantan Magharibi. Vituo vya umma, afisi za serikali, na hata mali za usalama wa taifa zilipata uharibifu mkubwa. Jijini Jakarta, kwa mfano, vituo 22 vya mabasi ya TransJakarta na vituo vya treni ya chini ya ardhi vya MRT viliharibiwa, huku hasara ikikadiriwa kuwa karibu rupiah bilioni 50.4 za Indonesia.

Soma zaidi...

Mradi wa Reli wa China–Indonesia: Mkakati wa China Kuidhibiti Indonesia

Indonesia inafikiria kujadili upya deni la mradi wa reli ya mwendo kasi wa Jakarta–Bandung, unaojulikana kama Whoosh, kutokana na mzigo mzito wa kifedha unaouweka kwa mwendeshaji wa reli ya serikali Kereta Api Indonesia (KAI). Waziri wa Biashara Zinazomilikiwa na Serikali Erick Thohir alisema mpango huo utaruhusu KAI kusimamia treni huku serikali ikisimamia miundombinu. Mradi huo wenye thamani ya dolari bilioni 7.3 ulifadhiliwa hasa kupitia mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya China, awali kwa riba ya asilimia 2. Hata hivyo, kukatizwa na maambukizi na masuala ya ardhi yalisukuma gharama zaidi, na kuhitaji ufadhili wa ziada kwa riba ya asilimia 3.4.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu