Ijumaa, 08 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa wafikia Kukaba Uchumi wa Yemen ili Kukamata Rasilimali Zetu za Kiuchumi

Mnamo tarehe 15/10/2025, Gavana wa Benki Kuu ya Aden, Ahmed Al-Maabqi, alikutana jijini Washington D.C., na mkuu wa ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) nchini Yemen, Esther Pérez Ruiz, na mwakilishi wa IMF, Mohamed Maait, akiandamana na Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Waziri Msaidizi wa Fedha Abdul Qader Amin. Hii ilifuatiwa na mkutano kati ya Waziri wa Mipango na Ushirikiano wa Kimataifa na Gavana wa Yemen kwa Benki ya Dunia, Waed Badhib, na Riccardo Puliti, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa wa Kanda ya Mashariki ya Kati, pamoja na ushiriki wa Naibu Waziri wa Mipango Nizar Basuhaib, Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Abdul Qader Amin, kwa uwepo wa Stefan G. G. Reimbert, Mkurugenzi wa Kanda wa Benki ya Dunia katika Mashariki ya Kati, na Dina Abu Ghaida, Meneja wa Benki ya Dunia nchini Yemen.

Soma zaidi...

Mafunzo Kutokana Na Jinsi Nchi Kubwa Zaidi ya Kidemokrasia Duniani Inavyowafelisha Wanawake wa Kiislamu

Gazeti la ‘The Indian Express’ limechapisha makala yenye kichwa “Pindi kutokuwepo kukizungumza kwa sauti ya juu zaidi kuliko uwepo: Wanawake wa Kiislamu na Bunge la India”. Yanazungumzia ukosefu mkubwa wa uwakilishi wa wanawake wa Kiislamu katika afisi yake. Tangu Lok Sabha ya kwanza (Bunge la Kidemokrasia la India) mnamo 1952, ni wanawake kumi na nane pekee Waislamu ambao wamekuwa wachangamfu ndani bunge. Uwakilishi mdogo umerekodiwa katika kitabu kipya kilichoandikwa na waandishi wa habari Rasheed Kidwai na mwanasayansi wa siasa Ambar Kumar Ghosh chenye kichwa “Kukosekana Bungeni: Wanawake wa Kiislamu katika Lok Sabha”, kilichochapishwa na Juggernaut (2025). Waandishi hawajali katika utambuzi wao wa jinsi uwakilishi kama huo ulivyokuwa mara nyingi. Kwa vyama vingi vya kisiasa, ugombezi wa mwanamke wa Kiislamu ulifanya kazi kama ishara tu badala ya athari na ushawishi halisi.

Soma zaidi...

Kuwakataa Wanariadha wa ‘Israel’: Kipimo Halisi cha Msimamo Madhubuti wa Indonesia?

Indonesia: Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) ilikataa rufaa ya Shirikisho la Michezo ya Viungo (Gymnastics) la ‘Israel’ (IGF) kuruhusu wanariadha wake kushiriki Mashindano ya Dunia ya Sanaa za Gymnastiki jijini Jakarta, Indonesia, kuanzia Oktoba 19–25, 2025. Serikali ya Indonesia iliwanyima viza wachezaji sita wa mazoezi ya viungo wa ‘Israel’, ikionyesha uungaji mkono kwa Wapalestina na shinikizo la ndani. IGF ilkata rufaa kwa CAS na Shirikisho la Kimataifa la Gymnastiki (FIG), ikiomba hatua za kuhakikisha ushiriki au kubatilisha michezo hiyo. CAS ilitupilia mbali rufaa zote mbili, na FIG ilisema haina mamlaka juu ya maamuzi ya visa. Indonesia ilithibitisha tena msimamo wake, ikiegemea katika sera yake ya kigeni na hisia za umma.

Soma zaidi...

Ukamatwaji wa Wanachama wa Hizb ut Tahrir jijini Beirut!

Katika marudio ya mbinu na hatua za ukamataji holela wa vyombo vya usalama bila msingi wowote wa kisheria, wa watu—baadaye waliotambuliwa kuwa wanachama wa chombo cha usalama chenye mfungamano na serikali—wakiwa kwenye pikipiki waliwakamata wanachama wawili wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Lebanon walipokuwa wakigawanya taarifa moja ya kulaani kuendelea kwa uvamizi wa Kiyahudi dhidi ya Lebanon na watu wake. Kukamatwa huku kulitokea jana, 17/10/2025, baada ya Swala ya Ijumaa mbele ya Msikiti wa Imam Ali katika eneo la Tariq al-Jadida jijini Beirut.

Soma zaidi...

Kupigwa Marufuku kwa Hizb ut Tahrir? – Kufilisika kwa Demokrasia

Kufuatia kampeni ya uzushi ya kibinafsi dhidi ya mmoja wa wanachama wetu iliyofanywa na vyombo vya habari na wanasiasa—kutokana tu na matamshi na maadili yake ya Kiislamu—pande zote tatu za serikali ya Denmark sasa zimejadidisha wito wao wa kisiasa wa kupiga marufuku Hizb ut Tahrir nchini Denmark. Hii ni mbali na wanasiasa wa mara ya kwanza wa Denmark kucheza “karata ya upigaji marufuku” kutokana na kutapatapa kifikra. Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, kwa nyakati tatu tofauti, amegundua kwamba hakuna msingi wa kikatiba wa upigaji marufuku wa aina hiyo.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu