Alhamisi, 15 Muharram 1447 | 2025/07/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Trump Aitishia Gaza kwa Uvamizi wa Moja kwa Moja na Kuwafukuza Watu Wake

Jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Kiyahudi kwamba "Wapalestina hawana chaguo zaidi ya kuondoka Ukanda wa Gaza. Nataka kuona Jordan na Misri zikipokea Wapalestina kutoka Gaza. Hakuna badali kwa wakaazi wa Gaza isipokuwa kuondoka." Aliongeza, "Jordan na Misri tayari zimekataa kuwapokea wakaazi kutoka Gaza, lakini baadhi ya watu wanakataa mambo isipokuwa hatimaye kukubaliana nayo."

Soma zaidi...

Enyi Majeshi ya Waislamu: Nani Atawakomesha Wapumbavu Hawa Wawili?!

Jana usiku, chaneli za satelaiti zilitangaza sherehe za mapokezi ya Rais wa Marekani Donald Trump kwa Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, pamoja na mkutano wa waandishi wa habari uliotangulia mazungumzo yao. Trump alionekana kama mcheshi akilenga kufurahisha watazamaji wanaomtazama, kwa kauli zake za kizembe kuhusu Ukanda wa Gaza, na nia yake ya kuwaondoa watu wake na kuweka udhibiti wa Amerika juu yake.

Soma zaidi...

Al-Burhan Anatafuta Kuiga Mfumo Ule Ule wa Kisekula Uliopita

Katika hotuba iliyotolewa leo na Jenerali Al-Burhan, Mwenyekiti wa Baraza la Utawala na Amiri Jeshi Mkuu, alisema: "Kipindi kijacho kitashuhudia kuundwa kwa serikali ili kukamilisha kazi za mpito. Inaweza kuitwa serikali ya muda. Baada ya kuidhinishwa kwa waraka wa katiba, serikali itaundwa, na waziri mkuu atachaguliwa kutekeleza majukumu yake katika kusimamia baraza la mawaziri la serikali bila kuingiliwa."

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Komesheni Mambo Matatu ya Marekani ambayo Yanahusisha Uhalifu Mkali: Vita, Kuitenga Darfur, na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi

Kila mtu anashangaa juu ya siri iliyoko nyuma ya kuongezeka kwa kasi hii katika operesheni za kijeshi za jeshi hivi karibuni, kama vile vita vilivyokuwa hapo awali, na kwa zaidi ya mwaka mmoja, vimekuwa vikifanyika ndani ya duara lililofungwa, huku kukiwa na kusonga mbele na kurudi nyuma, bila ya kuwepo na uamuzi wa kijeshi kutoka upande wowote.

Soma zaidi...

Je, Ugaidi ni Quran na Vitabu, Enyi Mliofilisika

Tovuti ya Russia Today ilichapisha ripoti ya habari mnamo tarehe 5/2/2025 ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya magaidi yenye mafungamano na Hizb ut Tahrir katika Rasi ya Crimea na kuwakamata watu watano waliokuwa wakisajili wafuasi wa Hizb, ambayo imepigwa marufuku nchini Urusi." Ripoti hiyo ilijumuisha video inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba, ambapo ilionekana wazi kwamba kile ambacho idara ya usalama ya Urusi ilichukua kutoka kwa nyumba za Mashababu ni nakala za Al-Quran Al-Kareem, vitabu, na vijitabu vya kisiasa na kifikra vya Kiislamu - machapisho maarufu ya Hizb ut Tahrir kwa jina pamoja na maalumati yaliyomo.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Kuongezeka kwa Uhasama nchini Sudan

Al Arabiya Net ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 4/2/2025: "Jeshi na vikosi vyake vya usaidizi viliingia katika maeneo ya kusini-mashariki ya Jimbo la Khartoum wakati wa saa zilizopita, wakitokea Jimbo la Al-Jazeera.." na tovuti ya Youm7 ilichapishwa mnamo tarehe 2/2/2025: "Mwandishi wa Kituo cha Habari cha Cairo aliripoti katika habari mpya zinazochipuka kwamba jeshi la Sudan linachukua idadi kadhaa ya vijiji mashariki mwa mto Nile katika Jimbo la Khartoum." Kabla ya hapo, mnamo tarehe 11/ 1/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka vilishindwa na jeshi la Sudan katika mhimili wa Jimbo la Al-Jazeera na mji mkuu wake, Wad Madani, “na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Hemeti, alikiri katika kanda ya sauti iliyohusishwa naye kwamba vikosi vyake vilishindwa katika Jimbo la Al-Jazeera...” (Al-Jazeera 1/13/2025).

Soma zaidi...

Uhamisho au Ukombozi, enyi Umma wa Kiislamu?

Dhalimu wa Marekani, Trump, alisema katika mkutano na waandishi wa habari pamoja na mhalifu Netanyahu jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025: "Marekani itachukua Ukanda wa Gaza, na tutafanya kazi nayo pia" Aliongeza, "Tutageuza Ukanda wa Gaza ulioharibiwa kuwa Riviera ya Mashariki ya Kati." Alizungumzia juu ya umiliki wake wa muda mrefu wa Gaza na alisisitiza taarifa yake ya awali kuhusu kuwahamisha watu wa Gaza, ambapo alisisitiza kutiishwa kwa watawala wa Misri na Jordan na wasaidizi wao, akisema: "Misri na Jordan zilisema hazitapokea wakaazi kutoka Gaza, na mimi nasema lazima watapokea." Hapo ndio watawala watiifu, wasaliti.

Soma zaidi...

Kutangaza Jamhuri nchini Syria ni Usaliti wa Mapinduzi ya Kiislamu!

Ahmed al-Shara, ambaye alifanya ziara yake ya kwanza ya kigeni nchini Saudi Arabia baada ya kuchukua kiti cha Urais nchini Syria, alitoa taarifa muhimu kuhusu mustakabali wa Syria sambamba na ramani ya utendakazi ya kisiasa ambayo amedumisha katika mahojiano na televisheni ya Syria. Akiahidi kukuuza uchumi wa soko huru na vifaa vya uwekezaji, Shara alisema, "Syria ni nchi ambayo itahifadhi hali yake ya asili, muundo wa serikali utakuwa wa jamhuri, kutakuwa na bunge, tawi la utendaji na mamlaka zinazofanya kazi kwa ushirikiano kati yao." alitumia maneno yake. (Mawakala)

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Uhamishaji wa Watu wa Gaza

Al Jazeera ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 26/1/2025: “Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba anaishinikiza Jordan, Misri na nchi nyingine za Kiarabu kupokea wakimbizi zaidi wa Kipalestina kutoka Gaza, baada ya vita vya Israel dhidi ya Ukanda huo kusababisha mgogoro wa kibinadamu. Alipoulizwa ikiwa hili lilikuwa pendekezo la muda au la muda mrefu, Trump alisema, “Inaweza kuwa hili au lile.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu