Ijumaa, 18 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kutoka Uingereza hadi Australia: Utambuzi wa Uongo Unafungua Njia ya Uhalalishaji Mpana zaidi wa Mahusiano

Miaka miwili baada ya mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kizayuni katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, likiungwa mkono kikamilifu na Marekani, NATO, na washirika wao makruseda, Umoja wa Mataifa na dola zenye nguvu duniani wamejibu kwa kulituza umbile hilo. Utambuzi wa “Dola ya Palestina” unakuja huku Gaza ikivuja damu, na baada ya dola 150+ tayari kutoa utambuzi sawia.

Soma zaidi...

Majibu ya Vyombo vya Habari kwa Yaliyomo kwenye Makala ya Mwandishi Sabah Muhammad Al-Hassan

Hizb ut Tahrir ni chama cha kisiasa ambacho mfumo wake ni Uislamu, kinataka kurudisha mfumo kamili wa maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume kwa njia ya kisiasa, na hakitekelezi vitendo vyovyote vya kisilaha si kwa kumwogopa mtu yeyote, bali ni kujifunga na njia ya Mtume (saw) katika kusimamisha dola ya kwanza ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Suluhisho la Dola Mbili: Njia ya Uhai kwa “Israel”, Sio kwa Palestina

Dola nyingi zaidi za Magharibi zinawasilisha wito wa suluhisho la dola mbili kama hatua ya kimaadili na ya haki. Lakini wale wanaotazama nyuma ya pazia wanaona kuwa halina uhusiano wowote na huruma kwa Wapalestina au utambuzi wa “haki yao ya uhuru”. Kinyume chake: ni hatua ya dharura ya kisiasa, inayoendeshwa na shinikizo kutoka kwa watu wao wenyewe na hasara inayokuja ya uhalali wa umbile la Kizayuni.

Soma zaidi...

Kutambuliwa kwa Dola ya Palestina Kutambuliwa kwa Mayahudi Kunyakua 78% ya Palestina!

Uingereza, Canada, Australia na Ureno zililitambua ile inayoitwa “Dola ya Palestina,” na kufuatiwa na nchi kadhaa katika mkutano wa ngazi ya juu wa kimataifa wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliofanyika kuanzia Septemba 22-30, 2025, na ulioongozwa na Ufaransa na Saudi Arabia. Utambuzi huu ulikaribishwa na watawala Ruwaibidha (wajinga wasio na maana) wa Waislamu, pamoja na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu na Jumuiya ya Waarabu. Jambo la kushangaza ni kwamba, ilikaribishwa pia na mashirika ya Kipalestina, ambayo yanaona kuwa ni matunda ya uthabiti wao, kana kwamba Palestina imekombolewa na na umbile la Kiyahudi kung'olewa!

Soma zaidi...

Marekani Yaendesha Uharibifu... Na Watawala ni Watiifu kwa Miradi Yake ya Kikoloni!

Mamlaka zilizofuatana juu ya nchi yetu hazikujiepusha na kutii mashinikizo ya Marekani, kwa kukubali kushiriki katika kuimarisha mkakati wake wa kikoloni katika kuitawala dunia nzima, ikiwemo kanda yetu ya Waarabu na eneo letu la Afrika. Hii ni kama vile kusainiwa na utawala wa Sebsi juu ya uamuzi wa Barack Obama wa kuipa Tunisia hadhi ya Mshirika Mkuu Asiyekuwa mwanachama wa NATO, au kufungua nchi yetu kwa mpango wake barani Afrika kwa kuandaa, kwa mwaka wa nane mfululizo, mazoezi ya kijeshi ya African Lion 2025, ambapo Jenerali Dagvin Anderson, kamanda wa Kamandi ya Marekani ya Umoja wa Mataifa Afrika (AFRICOM) alisema mbele ya Kamati ya Huduma za Silaha katika Bunge la Congress la Marekani kwamba Morocco na Tunisia ni miongoni mwa washirika wenye uwezo mkubwa wa kusafirisha usalama barani humo.

Soma zaidi...

Makubaliano ya Aibu ya Kuhalalisha Usalama na Mayahudi na Miradi ya Ugawaji ni Hatari Kubwa Inayolenga Kuvunja Utashi wa Kiota na Ushindi Uliopata

Katika taarifa ambazo, kusema kwa uchache, ni hatari, zilizotolewa na mkuu wa awamu ya mpito, Ahmed al-Sharaa, vipengee vya hali ya sasa ya Syria vilifichuliwa. Alionyesha kwamba “Syria inajua jinsi ya kupigana, lakini haitaki tena vita,” na kwamba “haina chaguo ila kufikia makubaliano ya usalama na Israel,” wakati “kujitolea kwa Israel kwa makubaliano haya ni suala tofauti.” Pia alieleza kuwa matukio ya Sweida yalikuwa tu “mtego uliotayarishwa makhsusi kuzuia makubaliano ya awali juu ya utaratibu wa usalama,” na kwamba “baadhi ya mirengo ndani ya SDF na PKK ilivuruga makubaliano ya Machi na kupunguza kasi ya mchakato huo.” Amesisitiza kuwa “hali ya kaskazini mashariki mwa Syria inatishia usalama wa kitaifa wa Uturuki pamoja na Iraq,” na akadokeza kuwa “ikiwa uwiano hautafikiwa ifikapo Disemba, Uturuki inaweza kuchukua hatua za kijeshi.”

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari yenye kichwa: “Taarifa ya Quad na Ubwana Uliopotea”

Wanaofuatilia suala la Sudan na mapambano makali ya kimataifa juu ya ardhi yake wanajua vyema kwamba vita hivi vinaendeshwa na Marekani ili kung'oa ushawishi wa Kiingereza na kuichana Sudan kwa kutenganisha Darfur, na kwamba hatua zote za kisiasa zinazofanywa na Amerika au vyombo vyake nchini Sudan zinalenga kuondoa juhudi zozote ambazo zingewarudisha watu wa Uingereza kwenye mandhari.

Soma zaidi...

Operesheni ya Shujaa Aliyeuawa Shahidi Abdul Muttalib Al-Qaisi Inathibitisha Azma ya Ummah Kupambana na Mayahudi hadi Watakapotokomezwa, Licha ya Watawala wa Kiarabu Kushindwa

Jana, 10 Septemba 2025, kamanda wa Kamandi Kuu ya jeshi la umbile la Kiyahudi alitangaza kuundwa kwa kitengo kipya cha kijeshi, kinachoitwa “Kitengo cha Gilead,” katika Bonde la Jordan, kitakacho kaa kwenye Bonde la Jordan. Kitengo hichi cha kikanda kina jukumu la kulinda mipaka ya mashariki ya Mayahudi katika Bonde la Jordan na Bahari ya Dead. Aliashiria kuwa kuanzishwa kwa kitengo hicho kunajiri ndani ya muundo wa kile alichoelezea kama “masomo ya kujifunza kutokana na kushindwa kugumu kwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.” Uundaji huu mpya unakuja baada ya vitisho vya viongozi wa umbile la Kiyahudi kupanuka hadi nchini Jordan na kwengineko chini ya mwavuli wa mradi wa “Israel Kubwa”, uliotangazwa na Netanyahu, uliobarikiwa na Trump, na kutangazwa wazi na Smotrich, Waziri wa Fedha wa umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu