Jumapili, 23 Safar 1447 | 2025/08/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu

Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa: Chombo Mikononi mwa Makafari cha Kudhibiti Sera ya Ndani ya Nchi Inayokopa

Mnamo Jumatano, 9/7/2025, Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) ulionya kwamba uchumi wa Iraq unakabiliwa na changamoto kubwa. Bodi ya IMF, katika taarifa yake ya kuhitimisha mashauriano ya Kifungu cha IV na Iraq, ilisema kuna nafasi ya kuimarisha mapato yasiyo ya mafuta kupitia ongezeko la kodi na ushuru wa forodha.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Yaelekezeni macho yenu kwenye makasri ya watawala wenu, sio Ikulu ya White House!

Macho ya Waislamu kwa jumla, na waandishi wa habari, wachambuzi, waangalizi, na wale wanaohusika hasa, yanaelekea Ikulu ya White House, na kwenye matokeo ya mikutano ya Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, Benjamin Netanyahu. Je, Trump atamshinikiza Netanyahu kukubali kwa upole kusitisha vita vyake dhidi ya Gaza?

Soma zaidi...

Usaliti wa Watawala wa Pakistan na Kukumbatia Kwao Uhalalishaji wa Mahusiano: Utangulizi wa Kujiunga na Mkataba wa Khiyana wa Abraham na Kutumikia Maslahi ya Amerika ya Trump na Umbile la Kiyahudi

Marekani ya Trump sasa inajitahidi kuunda "Mashariki ya Kati Mpya," ambayo inatumikia maslahi ya Marekani katika kanda hiyo, shauku kuu ikiwa ni kuhakikisha amani, usalama, na upanuzi wa kambi ya kijeshi ya Amerika katika Ulimwengu wa Kiislamu, inayojumuishwa ndani umbile la Kiyahudi. Inatafuta kuliweka umbile la Kiyahudi kama mamlaka kuu katika eneo hilo kisiasa, kiuchumi, na kimfumo. Licha ya haya yote, vibaraka wa Amerika ya Trump wamekimbilia kutekeleza mradi huu, na kutumikia maslahi ya bwana wao.

Soma zaidi...

Ajali za Barabarani nchini Misri: Ushahidi Tosha wa Kukosekana kwa Ustawi wa Jamii na Ufisadi wa Mfumo wa Kirasilimali

Katika tukio ambalo limekuwa la kusikitisha, watu waliamka siku chache zilizopita na kushuhudia maafa mengine ambayo yalisababisha vifo vya watu tisa wasio na hatia katika ajali iliyotokea kwenye Barabara ya Kanda katika Jimbo la Monufia, chini ya wiki moja baada ya maafa ya kuhuzunisha ambapo wasichana wachanga kumi na nane waliangamia katika ajali sawia, ikitofautiana na ile ya awali tu na kwa idadi ya wahasiriwa. Barabara ya Kanda - ambayo serikali imekuwa ikiitangaza kwa muda mrefu kama "mafanikio ya kitaifa" - imekuwa shahidi wa kudumu wa upuuzi wa yale yanayodaiwa kuwa mafanikio yanayosifiwa na watawala huku wakijificha nyuma ya mabango ya vyombo vya habari vya uwongo na kupuuza haki msingi ya watu: kuishi kwa usalama kwenye barabara ambazo hazinyakui maisha yao.

Soma zaidi...

Utambuzi wa Urusi wa Serikali ya Afghanistan: Hatua Zaidi ya Kuzuia Kuibuka kwa Mfumo wa Kiislamu katika Kanda hii

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Afghanistan inauona utambuzi huu kama sehemu ya mchakato mpana ambao kwao utawala wa sasa utayeyushwa hatua kwa hatua ndani ya mfumo wa kimataifa wa kisekula wa dola ya kitaifa. Mfumo huu, baada ya muda, utaiweka mbali serikali hii na lengo kuu la Kiislamu la kusimamisha na kubeba Dini ya Mwenyezi Mungu (swt). Zaidi ya hayo, utambuzi huo unaweza kuigeuza Afghanistan kuwa uwanja wa vita vya kiushindani kati ya dola za kikanda na kimataifa.

Soma zaidi...

Mjadala juu ya Upandaji wa Malori ya Kuhitimu Unafichua Chuki iliyokithiri ya Vyombo vya Habari na Wanasiasa wa Denmark dhidi ya Uislamu

Wiki hii iliyopita kumeshuhudiwa vurumai kubwa la vyombo vya habari na kisiasa kutokana na machapisho ya mitandao ya kijamii ambapo Waislamu waliwapongeza wahitimu wa mwaka huu huku pia wakiwasilisha mtazamo wa Kiislamu kuhusu kupanda malori ya kuhitimu yenye sifa ya ulevi na tabia mbaya.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh Iliandaa Maandamano na Matembezi ya kupinga Uhamishaji wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, iliandaa maandamano na matembezi leo (Ijumaa, 4 Julai 2025) baada ya swala ya Ijumaa katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga uhamishaji unaoendelea wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa mtutu wa bunduki. Wanachama mbalimbali wa Hizb ut Tahrir walitoa hotuba katika maandamano hayo ambayo yalimalizika sambamba na matembezi.

Soma zaidi...

Watoto Wanakufa kwa Njaa... Huku Watawala Wakiendelea na Uzembe wao!

Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya ya Palestina mjini Gaza, Dkt. Munir Al-Barsh, alifichua kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaokufa kwa njaa, na kuthibitisha kwamba uvamizi "unafurahi kuwaua," huku kukiwa na mzingiro unaoendelea, kufungwa kwa vivuko, na kupuuza mfumo wa kimataifa. Katika mahojiano katika Chaneli ya Al Jazeera, Al-Barsh alisema kuwa idadi ya watoto waliouawa shahidi kutokana na utapiamlo uliokithiri imefikia 66 hadi sasa, kati yao wa hivi punde ni mtoto mchanga wa miezi mitatu Jouri Al-Masri, akibainisha kuwa makundi yaliyo hatarini zaidi, hasa miongoni mwao ni watoto, wamekuwa wahanga wakuu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu