Kuitelekeza Gaza ni Doa katika vipaji vya Nyuso Zenu Enyi Wanajeshi wa Kinana na muhimu zaidi, ni Swali kutoka kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama
- Imepeperushwa katika Misri
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kila siku, mtoto mjini Gaza hufa kwa njaa, au mzee hupumua pumzi yake ya mwisho bila dawa, au mwanamke hufunga macho yake kwa mara ya mwisho kwa maumivu yasiyoweza kuvumilika kutokana na kiu au njaa. Kila saa mbingu hutokwa na machozi, mawe yanapiga kelele, na ardhi inawalaani wale waliowaacha peke yao. Hii ndiyo Gaza... Gaza, ambayo imezingirwa si tu kwa mipaka na vifaru, bali na uzio wa usaliti uliosukwa na viongozi wa majeshi, watawala wa khiyana, na kimya cha Umma wao.