Jumamosi, 22 Safar 1447 | 2025/08/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kashmir Haiwezi Kukombolewa Bila Kubadilisha Uongozi Unaopoteza Fursa ya Dhahabu ya Kuikomboa Kashmir, kwa ajili ya Kumfurahisha Trump

Leo, tarehe 5 Agosti 2025, miaka sita imepita tangu kuunganishwa kwa lazima kwa Kashmir Inayokaliwa kimabavu na Raja Dahir wa zama hizi, Modi. Kulingana na makubaliano yaliyofikiwa nchini Marekani, kuisalimisha Kashmir ilikuwa ni usaliti wa wazi wa uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan wa wakati huo, serikali ya Bajwa-Imran. Miezi michache tu baadaye, Jenerali Bajwa aliendeleza usaliti huu kwa kutia saini makubaliano ya kusitisha mapigano, na Dola ya Kibaniani kuhusiana na Kashmir. Hata hivyo, usaliti huu dhidi ya Waislamu wanaodhulumiwa na wanyonge wa Kashmir uliendelea hata zaidi ya hapo.

Soma zaidi...

Mahusiano ya Kigeni ni Jukumu la Dola Pekee, kwa kuwa Dola Pekee ndiyo iliyo na Haki ya Kuchunga Mambo ya Ummah Kivitendo

Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa wajumbe kutoka Muungano wa Vyama na Mavuguvugu ya Sudan Mashariki, wakiongozwa na Sheiba Dirar na kuandamana na kundi la watu mashuhuri, walikutana na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki mnamo Jumamosi, 2 Agosti 2025, afisini kwake huko Adi Halo, ambapo wajumbe hao walijadiliana naye hali ya sasa ya Sudan kwa jumla, kwa kuzingatia changamoto zinazoikabili Sudan Mashariki. Ujumbe huo pia ulisisitiza umuhimu wa uratibu na nchi jirani ili kusaidia utulivu wa nchi na kukabiliana na migogoro ya kisiasa na usalama.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Soma zaidi...

Sio Taarifa ya Bogotá wala Tangazo la New York litaweza kuliokoa umbile la Kiyahudi!

Wakati sera ya mauaji ya halaiki na njaa huko Gaza ikiendelea huku ukatili wake wote ukionekana na kusikilizwa na dunia nzima, Uturuki vile vile, inaendelea na hatua zake rasmi za kukabiliana na ongezeko la misimamo ya rai jumla nchini Uturuki. Hata hivyo, haikutia saini taarifa iliyotayarishwa na The Hague Group huko Bogotá, mji mkuu wa Colombia, Julai 15–16. Lakini katika kujibu majibu hayo, Wizara ya Mambo ya Nje ilidai kuwa taarifa hiyo huenda ikatiwa saini hadi Septemba 20, na Waziri wa Mambo ya Nje Hakan Fidan alitangaza kuwa wana dukuduku katika muktadha wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Sheria ya Bahari.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Kisimamo Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan cha Kuinusuru Gaza

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan imeandaa kisimamo mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan leo, Ijumaa, 7 Safar 1447 H sawia na tarehe 1 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa. Wanachama wa Hizb waliinua mabango yenye alama ishara: “Angusheni viti vya utawala vinavyozuia kusonga kwa majeshi kuinusuru Gaza.”

Soma zaidi...

Hotuba Iliyotolewa na Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan mnamo Ijumaa tarehe 1/8/2025 M

Je, hili linaweza kuwaziwa kutoka kwenu?! Vipi mnaweza kula, kunywa na kulala na hali ndugu zenu mjini Gaza wanauawa, wanahamishwa na kuwekwa njaa na Mayahudi wanaokalia kimabavu eneo la Isra ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)?! Dhambi liko juu ya shingo zetu sote ikiwa hatutawanusuru ndugu na dada zetu wa Gaza. Hatutaweza kuwanusuru isipokuwa majeshi ya Umma yasonge, kwani wao ni watoto wenu na ndugu zenu, na hakuna kitakachowaondoa Mayahudi isipokuwa dola ya Waislamu; Khilafah.

Soma zaidi...

Magereza ya Misri: Kati ya Mateso na Mauaji Pindi Heshima Inapokanyagwa Haki Huuawa!

Katika tukio jengine la mara kwa mara la uhalifu uliofichwa, kijana mmoja aitwaye Ayman Sabry alikufa ndani ya kituo cha polisi katika Jimbo la Dakahlia kutokana na mateso ya kikatili, ambayo yaliacha alama wazi kwenye mwili wake. Chini ya masaa 48 baadaye, kijana mwengine alikufa ndani ya Kituo cha Polisi cha Al-Saff katika Jimbo la Giza, huku kukiwa na ripoti thabiti za kutelekezwa kimakusudi, dhulma, na ukatili, na kuvigeuza vituo vya polisi kuwa sehemu za vifo cha polepole.

Soma zaidi...

Yeyote Anayezuia Mkate Usifike Gaza Hapaswi Kuzungumzia kuhusu Utu, Ewe Waziri wa Mambo ya Nje Rafah: Imo ndani ya Tundu la Uvamizi... au imo Ndani Mshiko wa Serikali ya Misri?!

Katika mandhari ambayo hakuna jicho linaloweza kukosa kuiona, watoto wa Gaza wanasimama kwenye vifusi vya nyumba zao, wakikimbilia tama la maji, kipande cha mkate, au dozi ya dawa, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri anajitokeza mbele yetu akizungumzia "nia ovu" na "heshima ya sera ya kigeni," katika jaribio la kuiondolea serikali ya Misri dori yake halisi katika mzingiro wenye kunyonga pumzi uliolazimishwa juu ya Ukanda wa Gaza.

Soma zaidi...

Ni Lazima ikumbukwe kwamba Marekani ni Nchi ya Kikoloni; Kujisalimisha kwa Sera zake za Ushuru Kutahatarisha Ubwana wa Taifa!

Marekani, mchuuzi wa kimataifa wa ubepari, imeibua 'dhoruba ya ushuru' duniani kote, ikipuuza kanuni za uchumi wa soko huria – moja ya falsafa kuu za ubepari – na sheria na kanuni za kile kinachojulikana kama Shirika la Biashara Duniani (WTO) ililounda. Hii, kwa mara nyingine, inathibitisha kwamba mfumo wa kibepari hauna utu na wa kinyonyaji. Serikali ya mpito ya Bangladesh imetabanni sera ya utiifu katika kukabiliana na hatua za ushuru za Marekani. Tayari wamefanya uamuzi wa kujitoa mhanga kununua ndege 25 za gharama kubwa aina ya Boeing, pamoja na kuagiza pamba na LNG kutoka Marekani, ingawa nchi nyingi zinaghairi oda zao kutokana na utendakazi duni wa Boeing. Na wanafanya mikutano ya moja kwa moja na Marekani, wakiweka umma katika giza kupitia 'makubaliano fiche ya kihistoria' (NDA).

Soma zaidi...

Serikali ya Muungano Msingi ni Hatua ya Juu katika Kuharakisha Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), kupitia muungano wao unaoitwa Muungano Msingi wa Sudan "Ta'sis," ulitangaza mnamo Jumamosi, 26/7/2025, uteuzi wa Rais na Makamu wa Rais wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu, ambayo ina maanisha kuundwa kwa serikali sambamba katika mamlaka inayoendeshwa na jeshi kutoka mji wa Port Sudan, mashariki mwa nchi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu