Ijumaa, 18 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Simama pamoja na Watu Wasioteteleka wa Gaza, Sio na Trump Mwenye Kiburi!

Miaka miwili imepita tangu mauaji ya halaiki yanayofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi huko Gaza, ambalo liliyafanya ili kuficha kushindwa kukubwa lilikokupata mnamo Oktoba 7, 2023. Miaka miwili ambayo kila siku ilishuhudia mauaji mapya na ukatili usioelezeka, na dunia nzima imeshuhudia ukatili wa Mayahudi wanyakuzi ambao unakinzana na akili. Watoto, watoto wachanga, nyumba, shule, misikiti na hospitali zililengwa. Watawala wa nchi za Kiislamu walikutana mara kwa mara, wakazungumza, wakalaani, na kisha kutawanyika. Kila shutma iliwashajiisha Mayahudi kufanya uvamizi na mauaji makubwa zaidi. Umbile la Kiyahudi lilifikia hatua ya kuzuia kuingia kwa kipande cha mkate au tama la maji ndani ya Gaza kwa miezi mingi mirefu.

Soma zaidi...

Katika Ziara ya Amerika: Yote yako Pamoja – Kufedheheshwa, Kusihi, Uhalali, Makubaliano, na Majukumu Mapya!

Ziara ya Rais Erdoğan wa Uturuki nchini Marekani kushiriki katika mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ilikuwa mandhari ya kufedhehesha, sio kwake tu bali kwa viongozi wote wa dola pia. Rais mwenye kiburi wa Marekani Donald Trump alitoa hotuba mbele ya Baraza Kuu ambapo alitangaza kwamba “Marekani imebarikiwa kuwa na uchumi imara zaidi, mipaka yenye nguvu zaidi, jeshi lenye nguvu zaidi...” na kwamba ndani ya miezi minane ya utawala wake aliitoza dunia kodi ya ziada ya kiasi cha dolari trilioni 17, na kwamba Marekani iko katika nafasi nzuri huku nchi zengine “zinaenda kuzimu.” Alisema kuwa maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayana maana, na kudai kwamba alimaliza vita saba ndani ya miezi saba. Aliitaja tarehe saba ya Oktoba 2023 kama “unyama wa magaidi wa Hamas,” akizingatia kuwa suluhisho liko katika kuachiliwa huru mara moja kwa wafungwa, na kuongeza kuwa dini inayonyanyaswa zaidi duniani ni Ukristo.

Soma zaidi...

Enyi Wanajeshi wa Misri (Kinana): Vivuko vya Gaza havihitaji Malori, Bali vinahitaji Majeshi na Magari ya Kivita

Hali ya kibinadamu mjini Gaza imefikia viwango vya maafa ambavyo havijawahi kushuhudiwa. Idadi ya vifo vya mashahidi imezidi 65,000. Ripoti za kimataifa zinaweka idadi hiyo kuwa 40% zaidi. Hao ni zaidi ya mashahidi 100,000 na takriban wakimbizi wa ndani milioni 1.9, ambao ni karibu asilimia 90 ya wakaazi wa Ukanda wa Gaza, ambao wanaishi katika mazingira yasiyo ya kibinadamu, na kunyimwa mahitaji ya kimsingi ya maisha. Gaza inakabiliwa na njaa ya kweli, haswa katika sehemu ya kaskazini ya Ukanda huo. Hospitali zinafanya kazi chini ya 30% ya uwezo wao, na uhaba wa dawa na mafuta unaweka makumi ya maelfu ya wagonjwa katika hatari ya kifo cha polepole. Takwimu hizi zinafichua ukubwa wa maafa hayo na kuthibitisha kuwa kinachoendelea ni vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Gaza.

Soma zaidi...

Msimamo kwa Sherehe za Maadhimisho ya Mapinduzi Mawili ya Septemba Moja yaliingiza Usekula nchini Yemen na Mengine Yalitoa Wito wa Kuuimarisha!

Katika mwezi wa Septemba wa kila mwaka Yemen ina matukio mawili; la kwanza mnamo tarehe 26 Septemba 1962 ambayo ni kumbukumbu ya kupinduliwa kwa mfumo wa kifalme nchini Yemen Kaskazini, na la pili mnamo tarehe 21 Septemba 2014 ambayo ni kumbukumbu ya kuingia kwa Mahouthi jijini Sana’a ambayo ilisababisha udhibiti wao wa mikoa ya kaskazini.

Soma zaidi...

“Khiyana ya ‘Ruwaibidha’ (watawala wasiostahiki) na kuidhinishwa kwa mpango wa Trump kwa gharama ya damu ya mashahidi wa Palestina”

Baada ya hotuba ya rais wa Marekani kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa – ambayo asili ilikusudiwa kuhakiki kadhia ya Palestina – na katika wakati ambapo, kwa msimamo mmoja kutoka zaidi ya dola 150 kati ya dola 193 za Umoja wa Mataifa, “dola ya Palestina” tayari imetambuliwa, Rais Trump aliikejeli jumuiya ya kimataifa kwa kuyaita maneno ya “viongozi” kama “domo tupu.” Pia alikejeli makubaliano ya kimazingira, akaiichukulia mikataba ya uhamiaji kuwa ya kudharauliwa, na akakashifu mchakato wa Ulaya wa kuitambua Palestina kwa kuiita udhaifu. Hotuba yake ilionekana kama dua ya mwisho ya mazishi (fatiha) iliyosomwa juu ya makubaliano ya kimataifa, madai ya mtazamo wa upande mmoja wa Amerika katika masuala ya kimataifa, na tangazo la kulazimisha rai yake juu ya Mashariki ya Kati – haswa suala la Palestina.

Soma zaidi...

Maradhi ya Mkurupuko Yawaangamiza Watu kwa Kukosekana kwa Dola ya Ustawi

Maradhi matatu ya kimazingira—kipindupindu, homa ya dengue, na malaria—yanawaangamiza watu katika majimbo ya Khartoum, Al-Jazirah, na Darfur, katikati ya uzembe wa kutisha na aibu ya kukosekana kwa serikali inayojiita “Serikali ya Matumaini”! Kuna matumaini aina gani wakati watu wanaishi katika mazingira yasiyostahili hata kwa wanyama—mazingira yanayotawaliwa na waenezaji magonjwa, ikiwemo mbu wa malaria, mbu wa dengue, na nzi?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Ya‘qub Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan, atakuwa mgeni, chini ya kichwa: Ulaya na Ushawishi Wake kwa Matukio nchini Sudan.

Soma zaidi...

Kujibu Matamshi ya Mjumbe wa Marekani Tom Barrack

Kwa mara nyingine tena utawala wa Marekani unaonyesha sura yake halisi kupitia taarifa za mjumbe wake Tom Barrack, katika mahojiano yake yaliyotangazwa na Sky News na mtangazaji mkuu wa IMI International Hadley Gamble, ambaye alijiruhusu kuingilia waziwazi katika masuala ya Lebanon na kubainisha sifa za dori za taasisi ya Jeshi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu