Sudan: Janga la Karne Lililofichika Machoni mwa Ulimwengu
- Imepeperushwa katika Siasa
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Dola ya Kiislamu, mlinzi wa watu wake, haipo. Waislamu wameishi katika taabu, mateso, na majanga duniani kote. Sudan hivi sasa inakabiliwa na moja ya majanga mabaya zaidi ya kibinadamu katika historia ya kisasa kutokana na mapigano ya umwagaji damu ambayo yamekuwa yakiendelea kwa miaka miwili kati ya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), na kusababisha maafa ya kutisha ambayo hakuna anayezungumza au kujaribu kuzuia. Huu ni mzozo uliosahaulika ambao vyombo vya habari haviupi mwanga, na ambao maelezo yake hayafichuliwi na dola yoyote au hata taasisi zake.



