Jumapili, 27 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Umuhimu wa Kimkakati wa Siasa za Kijiografia za Sudan

Sudan ni nchi yenye umuhimu mkubwa wa kisiasa za kijiografia, unaotokana na ardhi yake kubwa, maliasili nyingi, na eneo ambalo linaiweka kitovu cha baadhi ya njia muhimu zaidi za kibiashara na kisiasa duniani. Licha ya kukabiliwa na miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu wa kisiasa, Sudan inasalia kuwa kitovu cha maslahi kwa dola zenye nguvu za kieneo na kimataifa kutokana na nafasi yake ya kimkakati na uwezo wake ambao haujatumiwa. Umuhimu wake sio wa kisasa tu bali pia wa kihistoria, haswa katika zama ambazo ilikuwa sehemu ya Khilafah kubwa zaidi ya Kiislamu, ambapo ilichukua nafasi muhimu katika kuunganisha na kuimarisha ulimwengu mpana wa Kiislamu. Na umuhimu wake utabaki mbeleni, Khilafah itakaporegea.

Soma zaidi...

Umuhimu wa Kimkakati wa Eneo la Sudan

Aprili 15, 2025 ilitimiza miaka miwili tangu Sudan kukumbwa na vita vya maangamivu vya wenyewe kwa wenyewe, na kusababisha moja ya majanga makubwa zaidi ya kibinadamu duniani leo. Miaka miwili iliyopita mwezi Aprili, mapigano yalizuka kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), na kuwahamisha mamilioni ya watu, na kuiingiza nchi katika uhaba mkubwa wa chakula, na kuharibu huduma muhimu za afya na elimu. Licha ya maafa ya kibinadamu ambayo yametokea, vita vya Sudan kwa kiasi kikubwa vimeepukana na muanga wa kimataifa. Sudan ni vita iliyosahauliwa, haswa kwa ulimwengu wa Magharibi ambao unaweza kuzingatia Ukraine pekee. Je, ni mambo gani ya siasa za kijiografia ambayo yanaifanya Sudan kushawishika kuyapigania?

Soma zaidi...

Uislamu Uliingiaje Sudan?

Kabla ya kuwasili kwa Uislamu, eneo linalojulikana leo kama Sudan halikuwa umbo lililounganishwa kisiasa, kitamaduni au kidini. Ilikuwa makao ya makabila, desturi, na imani mbalimbali. Upande wa kaskazini, Wanubi walifuata Ukristo wa Kiorthodoksi, na lugha ya Kinubi, pamoja na lahaja zake mbalimbali, ilikuwa njia ya siasa, utamaduni, na mawasiliano. Katika mashariki, makabila ya Beja, vizazi vya Hamu (mwana wa Nuhu), walikuwa na lugha yao wenyewe tofauti, utamaduni, na matendo ya kidini. Upande wa kusini, makabila ya Zanj, yenye sifa na lugha zao za kipekee, yalishikamana na imani za kipagani, na tofauti kama hizo zilikuwepo katika upande wa magharibi.

Soma zaidi...

Musiiangushe Gaza, Enyi Waislamu

Ni masikitiko kwa usaliti! Maumivu yake yanaumiza moyo. Hakika, usaliti ni mchungu zaidi kwa nafsi kuliko maumivu ya njaa, kifungo, na mateso. Wananchi wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina wakiwemo watu wa Gaza wanautaka Umma wa Kiislamu kuwanusuru na kuwakomboa, kwa sababu udugu wa Kiislamu unawataka Waislamu kuwanusuru wanaodhulumiwa miongoni mwao.

Soma zaidi...

Mtihani wa Gaza

Mwenyezi Mungu (swt) hakumuumba mwanadamu bila ya kuweka mbele yake mitihani kulingana na ukubwa wa Imani yake na kujitolea kwake katika Dini, ili Mwenyezi Mungu (swt) apate kujua ni nani atakayekuwa na subira mbele ya mitihani hiyo na kuweka tegemeo lake (tawakkul) kwa Mwenyezi Mungu (swt) . Haya ni ili Mwenyezi Mungu (swt) amuepushe na fitna. Ama wale ambao watafeli ndani ya mitihani hiyo, watafeli tu kwa sababu ya hukumu yao mbaya, kughafilika kwao na Amri za Mwenyezi Mungu (swt), na Imani yao dhaifu.

Soma zaidi...

Vita vya Sudan Vilivyosahauliwa: Janga kwa Ummah

Sudan inavuja damu. Na ulimwengu hauelewi kabisa. Sasa ikiingia katika mwaka wake wa tatu mbaya, vita vya kikatili kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF), vinavyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), vimeiingiza nchi katika machafuko na kuibua moja ya maafa ya kutisha zaidi ya kibinadamu ya zama zetu. Hata hivyo, licha ya ukubwa wa uharibifu na mateso, vita vya Sudan vinapuuzwa, kusahauliwa—vimenyamazishwa na kutojali kwa ulimwenguni.

Soma zaidi...

Sudan: Janga la Karne Lililofichika Machoni mwa Ulimwengu

Dola ya Kiislamu, mlinzi wa watu wake, haipo. Waislamu wameishi katika taabu, mateso, na majanga duniani kote. Sudan hivi sasa inakabiliwa na moja ya majanga mabaya zaidi ya kibinadamu katika historia ya kisasa kutokana na mapigano ya umwagaji damu ambayo yamekuwa yakiendelea kwa miaka miwili kati ya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), na kusababisha maafa ya kutisha ambayo hakuna anayezungumza au kujaribu kuzuia. Huu ni mzozo uliosahaulika ambao vyombo vya habari haviupi mwanga, na ambao maelezo yake hayafichuliwi na dola yoyote au hata taasisi zake.

Soma zaidi...

Mustakabali wa Vita vya Kisasa na Dori Iliyokosekana ya Khilafah

Vita vinavyoendelea katika sehemu mbalimbali za dunia—hasa vita kati ya Urusi na Ukraine na mzozo kati ya Iran na umbile la Kiyahudi—vinaonyesha wazi kwamba ulimwengu umeingia katika awamu mpya na tofauti ya vita vya kijeshi na kijasusi. Mtazamo wa kale wa vita, uliopitwa na wakati, unaojengwa juu ya vikosi vikubwa vya askari wachanga, vifaru, na mizinga, unabadilika kwa kasi na kuporomoka. Leo, dola kama vile Marekani, China na Urusi zinatenga bajeti kubwa kwa viwanda vya juu vya kijeshi na zinafafanua upya mbinu mpya za kivita. Vita kwenye mstari wa mbele wa kisasa havikomei tena kwa risasi na bunduki – ni vita vya operesheni za kimahesabu (algorithms), akili ya bandia, droni, mtandao na mawimbi ya satelaiti.

Soma zaidi...

Njama Endelevu, Iliyoimarishwa ya Kimataifa ya Kuzuia Mapinduzi ya ash-Sham yasifikie Malengo na Misingi yake

Mwenyezi Mungu (swt) alipowapa watu wa ash-Sham baraka za kumwangusha dhalimu mhalifu wa Syria, asubuhi ya tarehe 8 Disemba 2024, licha ya mipango na njama kubwa zilizopangwa na ulimwengu wote wa Magharibi, ukiongozwa na Marekani, ili kuyabatilisha mapinduzi na kuyazuia yasifikie lengo lake, ulikuwa ni utashi, azma, na Iman ya watu ash-Sham, kwa zana zao hafifu na za kawaida, ambapo hatimaye walishinda dhidi ya jumuiya ya kimataifa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu