Alhamisi, 22 Muharram 1447 | 2025/07/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Dhalimu Hasina ameanguka, lakini Washirika wake Waaminifu wa Kihindi bado wapo na wanaendelea kueneza Uzushi dhidi ya Hizb ut Tahrir

Tungependa pia kusisitiza kwa Inspekta Jenerali wa Polisi wa Bangladesh Bw. M Mainul Islam kwamba unashikilia wadhifa wa uwajibikaji unaotaka kuzingatia ukweli halisi. Baada ya kumpindua dikteta Hasina, watu wa nchi yetu hakika hawatarajii uongo wa wazi kutoka kwa wadhifa wako kama vile maafisa wa kutekeleza sheria walivyofanya wakati wa utawala wa dhalimu Hasina.

Soma zaidi...

Mswada wa Marekebisho ya 26 ya Katiba: Chini ya Khilafah, Madaraka na Mamlaka Vinaamuliwa na Qur'an Tukufu na Sunnah, Wakati Kuna Mivutano ya Kuendelea ya Madaraka Chini ya Demokrasia

Chini ya mfumo tawala wa Demokrasia, mzizi halisi wa ufisadi ni uwezo wa walio wengi waliochaguliwa kubadili kila sheria, kila kifungu cha katiba, kila kanuni na kila agizo. Nguvu ya kutunga sheria inavipa vikundi tawala uwezo wa kubadilisha sheria kulingana na maslahi yao, sio tu kupitia mlango wa nyuma, lakini kupitia mlango wa mbele. Nguvu ya sheria ndiyo inayoliruhusu Bunge kuhalalisha wizi unaofanywa na waporaji na wafujaji kupitia Sheria ya Maridhiano ya Kitaifa, kukubali kunyang'anywa madaraka na madikteta kwa nguvu, kupitisha mipango kadhaa ya msamaha kwa mirengo inayotawala na kutoa kinga ya kikatiba ya kutoshtakiwa kwa wale wanaohusika na mambo muhimu zaidi ya nchi.

Soma zaidi...

Minawi Aidekeza Marekani na Kufumbia Macho Matendo ya Wale Wanaojitahidi Kusimamisha Khilafah, Kutangaza Uislamu Mtukufu!

Minawi na mabwana zake wa kikoloni wanajua kwamba Hizb ut Tahrir inafanya kazi pamoja na ndani ya Ummah kusimamisha utawala wa Mwenyezi Mungu kwa kusimamisha tena Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume, ahadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na bishara njema ya Mtume wake (saw). Hata hivyo, Minawi na walio nyuma yake wanataka kuficha ukweli huu.

Soma zaidi...

Serikali ya Mpito Imeweka Mfano wa Aibu kwa Kumkamata Imtiaz Salim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh

Katika majira ya mapema Oktoba 4, 2024, serikali ya mpito, kwa desturi ya serikali ya kidikteta ya Hasina aliyeondolewa madarakani, ilimkamata Imtiaz Salim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Bangladesh. Kwa mujibu wao, kosa lake ni kwamba alishiriki katika shughuli za kisiasa za Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

Mkataba wa Ummah Unatokana na Itikadi yake Safi, hautoki kwa Demokrasia Batili!

Demokrasia kwa ufupi ni mfumo wa ukafiri na hauna uhusiano wowote na Uislamu, na yeyote anayeilingania au kutaka utabikishwaji wake ni wa kutiliwa shaka na mpotoshaji, kwa sababu Ummah unatamani kurudisha heshima na fahari yake kupitia Uislamu na ushindi wa Mwenyezi Mungu tunapomnusuru Yeye na Dini Yake kwa kuregea kwenye umoja wetu katika mfumo wa Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Haishangazi hata kidogo kwamba Serikali ya Modi, kwa kuhofia kutokea kulikokaribia kwa Khilafah ingepiga marufuku Hizb ut Tahrir - Chama cha Kweli cha Kisiasa na Kisicho na Vurugu

Kwa kuhofia kuibuka Khilafah inayoongozwa na Hizb ut Tahrir, Wizara ya Mambo ya Ndani ya India (MHA) mnamo Alhamisi iliyopita (Oktoba 10, 2024) ilipiga marufuku Hizb ut Tahrir, ikieleza kwamba “inataka kusimamisha dola ya Kiislamu ya kimataifa na Khilafah, ikiwemo India, kupitia jihad na shughuli za kigaidi”.

Soma zaidi...

“Mngurumo wa Jeshi la Waislamu chini ya Khilafah unatosha kupambana na Umbile Haramu la Kiyahudi” Chini ya Bango hili, Hizb ut Tahrir/Wilayah Bangladesh iliandaa Maandamano katika Misikiti ya Dhaka na Chittagong

Tawala za kisekula katika nchi za Waislamu - vibaraka wa Magharibi, zinashirikiana katika vita vinavyoongozwa na Marekani dhidi ya Uislamu na Waislamu. Watawala wa Kiarabu katika Mashariki ya Kati na watawala wa Waislamu katika eneo letu, wanasaidia mtawalia kuimarisha mikono ya umbile haramu la ‘Israel’ na India. Ili kuchelewesha kudhihiri Khilafah - mlinzi wa Umma wa Kiislamu - wanaeneza uongo, propaganda na ukandamizaji dhidi ya wito wa Khilafah na Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

Wafu Wetu wako Peponi Wafu Wenu wako Motoni

Ulimwengu ulipokea habari za kuuawa kishahidi kwa shujaa Yahya Sinwar; ambaye alikuwa mwiba ubavuni na donge kwenye koo ya umbile la Kiyahudi na wale waliokuwa nyuma yake, waliopanga Operesheni Kimbunga cha Al-Aqsa mnamo Oktoba 7, 2023, operesheni ambayo ilitikisa umbile la Kiyahudi, kutishia uwepo wake, na kutuma ujumbe wa vitisho kwa viongozi wa nchi za makafiri; maana yake ni kwamba Waislamu wanakuja!

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu