Jumamosi, 19 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuweka Matumaini juu ya Kuvunjika kwa Safu za “Israel” ni Usaliti Mpya wa Gaza

Kura moja ya maoni ilifichua kuwa 56% ya “Waisraeli” wanaogopa kusafiri nje ya nchi, 67% wanaamini kuwa serikali haiwawakilishi na 62% wanaunga mkono makubaliano ya kina ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas, ikiwemo kuachiliwa huru kwa mateka. Tovuti ya “Zman Yisrael,” ambayo ilichapisha maelezo ya kura hiyo ya maoni mnamo tarehe 5 Septemba 2025, ilifafanua kuwa wengi wa “Waisraeli” walionyesha kutokuwa na uwezo wao wa kusafiri nje ya nchi kutokana na kuongezeka kwa ukosoaji wa kimataifa wa umbile lao pamoja na kutengwa kunakoendelea kwa kimataifa kwa dola yao na kuendelea kwa vita mjini Gaza.

Soma zaidi...

Ndiyo, Uko Gaza na Gaza Inaangamizwa!

Huku uvamizi na mauaji ya halaiki mjini Gaza, yakiendelea kwa muda wa miezi 23, yamefikia kilele kwa matumizi ya silaha ya njaa inayoangamiza watu pamoja na majaribio ya mbinu mpya za mauaji zinazoitwa “mabomu ya roboti”; siasa za kinyonyaji na za kinafiki za watawala wa nchi za Kiislamu—wanaokabiliwa na ghadhabu za watu wao wenyewe kwa kuitelekeza Gaza—pia zimefikia kilele cha vilele.

Soma zaidi...

Marekani inatia Mikono yake Michafu katika Kila Mzozo; Sudan sio Tofauti

Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, Amerika imejidhihirisha kama mpangaji mkuu nyuma ya baadhi ya mizozo ya kunyama na ya ghasia zaidi kote duniani. Kutoka Urusi na Ukraine hadi India na Pakistan hadi China na Taiwan hadi Syria, Iraq, Afghanistan, Yemen, Kenya, Mali, Cameroon, na hii ni mifano michache tu! Hata hivyo, hakuna kilichoifichua Marekani zaidi ya uungaji mkono wake usio na haya na ushiriki wake katika mauaji ya halaiki yanayotokea Gaza dhidi ya watu wa Palestina. Kabla ya uvamizi, kuzingirwa kabisa, na kuangamizwa kwa Gaza, watu wengi hawakujua jinsi serikali ya Marekani ilivyokuwa chafu na jinsi wanavyoweza kuwatembeza wachezaji kama poni kwenye bao la chess.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mkakati wa Amerika na Suluhisho la Dola Mbili

Tunajua kwamba mkakati wa Marekani wa kuasisi umbile la Kiyahudi katika moyo wa nchi za Kiislamu, kwa sehemu kubwa, umeegemezwa kwenye suluhisho la dola mbili. Hata hivyo, chini ya Trump, mkakati huu umeanza kuatelekezwa, au angalau kunyamaziwa, jambo ambalo limezua maswali. Kwa mfano, Trump alisema, "Unapotazama ramani, ramani ya Mashariki ya Kati, 'Israel' ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ardhi hizi kubwa mno. Kwa hakika nilisema: 'Je, kuna njia yoyote ya kupata zaidi? Ni ndogo..." (Sky News, 19/8/2024). Je, hii inamaanisha kuwa mradi wa suluhisho la dola mbili wa Amerika umekufa na kukamilika, au bado ungali hai?

Soma zaidi...

Kuzaliwa kwa Uongofu: Nuru Inayoondoa Giza Lililopo

Sayari ya Dunia, na hasa Bara Arabu, lilikuwa likiishi katika giza kuu lililofanya maisha ya binadamu yafanane na kuzimu. Kulikuwa na giza katika nyanja za itikadi, siasa, uchumi, mahusiano ya kijamii, na nyanja zote za maisha. Vita viliwasaga watu bila sababu, wenye nguvu walikuwepo huku wanyonge wakipotea na kutokuwepo, dhulma ilitanda maeneo yote, na utumwa ulifikia viwango vyake vya chini kabisa na vya udhalilishaji kabisa.

Soma zaidi...

Usaliti wa Magharibi kwa Wale Wanaoitumikia Katika Vita Dhidi ya Uislamu

Mkakati na sera ya Wakoloni wa Magharibi kuelekea Umma wa Kiislamu imejikita katika kupiga vita Uislamu kama fahamu ya kihadhara na kimfumo. Ilifanya kazi kupitia njama kubwa na ovu za kuivunja Dola ya Kiislamu, kuikata vipande vipande, na kuzuia kuregea kwake madarakani na kuwaunganisha Waislamu. Ili kutekeleza sera na njama zake, Wakoloni wa Magharibi waliwaajiri baadhi ya wana wa Waislamu, wakiwalea kwa uangalifu katika fikra, siasa, utawala na vyombo vya habari. Kama vile orientalisti mmoja alivyosema, “Mti wa Uislamu lazima ukatwe kupitia mmoja wa watoto wake.”

Soma zaidi...

Uchaguzi wa DUCSU: Siasa za Kidemokrasia Zimeshindwa Kutumia Nguvu ya Vijana kwa Mabadiliko ya Kweli

Wanafunzi jumla wa Chuo Kikuu cha Dhaka, Chuo Kikuu cha Jahangirnagar, na Chuo Kikuu cha Rajshahi wametarajia kwa nguvu mabadiliko chanya ya kisiasa na uhakikisho thabiti wa ustawi wa wanafunzi baada ya uchaguzi uliodumu kwa muda mrefu wa vyama vyao vya wanafunzi mnamo Septemba. Wanafunzi wengi wa vyuo vikuu hivi walisema kwa uthabiti kwamba walitaka kukomeshwa kwa mila za unyonyaji za siasa za vyuo vikuu, na kuwataka wawakilishi wa wanafunzi wanaokuja kufanya kazi kwa ajili ya kulinda haki za wanafunzi. Walisisitiza kwamba wawakilishi wa wanafunzi waliochaguliwa lazima wawe sauti ya wanafunzi jumla ili kuhakikisha mazingira rafiki kwa wanafunzi katika vyuo vikuu kufuatia mabadiliko ya kisiasa ya Julai 2024 yaliyopatikana kupitia uasi mkubwa ulioongozwa na wanafunzi uliopindua utawala wa Awami League mnamo Agosti 5 mwaka huo.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu