Jumapili, 27 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uchaguzi wa DUCSU: Siasa za Kidemokrasia Zimeshindwa Kutumia Nguvu ya Vijana kwa Mabadiliko ya Kweli

Wanafunzi jumla wa Chuo Kikuu cha Dhaka, Chuo Kikuu cha Jahangirnagar, na Chuo Kikuu cha Rajshahi wametarajia kwa nguvu mabadiliko chanya ya kisiasa na uhakikisho thabiti wa ustawi wa wanafunzi baada ya uchaguzi uliodumu kwa muda mrefu wa vyama vyao vya wanafunzi mnamo Septemba. Wanafunzi wengi wa vyuo vikuu hivi walisema kwa uthabiti kwamba walitaka kukomeshwa kwa mila za unyonyaji za siasa za vyuo vikuu, na kuwataka wawakilishi wa wanafunzi wanaokuja kufanya kazi kwa ajili ya kulinda haki za wanafunzi. Walisisitiza kwamba wawakilishi wa wanafunzi waliochaguliwa lazima wawe sauti ya wanafunzi jumla ili kuhakikisha mazingira rafiki kwa wanafunzi katika vyuo vikuu kufuatia mabadiliko ya kisiasa ya Julai 2024 yaliyopatikana kupitia uasi mkubwa ulioongozwa na wanafunzi uliopindua utawala wa Awami League mnamo Agosti 5 mwaka huo.

Soma zaidi...

Kuweka Matumaini juu ya Kuvunjika kwa Safu za “Israel” ni Usaliti Mpya wa Gaza

Kura moja ya maoni ilifichua kuwa 56% ya “Waisraeli” wanaogopa kusafiri nje ya nchi, 67% wanaamini kuwa serikali haiwawakilishi na 62% wanaunga mkono makubaliano ya kina ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas, ikiwemo kuachiliwa huru kwa mateka. Tovuti ya “Zman Yisrael,” ambayo ilichapisha maelezo ya kura hiyo ya maoni mnamo tarehe 5 Septemba 2025, ilifafanua kuwa wengi wa “Waisraeli” walionyesha kutokuwa na uwezo wao wa kusafiri nje ya nchi kutokana na kuongezeka kwa ukosoaji wa kimataifa wa umbile lao pamoja na kutengwa kunakoendelea kwa kimataifa kwa dola yao na kuendelea kwa vita mjini Gaza.

Soma zaidi...

Uagizaji Mchele kutoka Nje: Ukoloni na Uuaji wa Kilimo

Mahakama Kuu ya Kenya hivi majuzi imeondoa marufuku ya serikali ya kuagiza mchele kutoka nje ya nchi bila ushuru, na hivyo kufungua njia kwa wafanyibiashara kulijaza sokoni kwa mchele wa bei nafuu wa kigeni. Ingawa hatua hiyo inaweza kusherehekewa na wengine kama njia ya kupunguza gharama ya maisha, athari zake za kina haziwezi kupuuzwa.

Soma zaidi...

Kuhuisha Uislamu: Njia Pekee ya Kuepuka Majanga

Mafuriko ya hivi majuzi nchini Pakistan yameharibu Khyber Pakhtunkhwa na Sindh, huku maeneo mengine yakipambana na barabara zilizojaa maji ambayo yamegeuza maisha ya kila siku kuwa hatari. Masaibu ya kupoteza maisha na riziki katika KPK yamewaacha watu na hofu. Kinachosumbua zaidi ni kukosekana kwa vifaa sahihi vya uokoaji – na kufanya wengi kuhoji uwezo wa serikali kujibu. Wafanyikazi wa uokoaji wanaachwa wakifanya kila kitu kwa mikono, na kwa mara nyingine tena, ni watu wa eneo hilo ambao, waliopata ukakamavu kwa miaka ya kupuuzwa, wanajua lazima wajitegemee wenyewe kwa sababu ima utakuja msaada mdogo hautakuja kabisa.

Soma zaidi...

Uongozi wa Kiislamu Unapokosekana, Ukandamizaji Hutawala

Marekani kwa mara nyengine tena imefichua hali yake ya kiuadui ya sera yake ya kibeberu ya mambo ya nje kwa kutuma manuari tatu kuelekea pwani ya Venezuela. Washington inahalalisha hatua hiyo kupitia tuhuma za muda mrefu kwamba Venezuela inashiriki katika ulanguzi wa madawa ya kulevya-shtaka ambalo Caracas inakataa vikali kama lisilo na msingi na linalochochewa kisiasa.

Soma zaidi...

Uislamu ni Ujumbe kwa Wanadamu Wote!

Leo hii, watawala mafisadi na wasio na thamani ambao wamejinyakulia madaraka katika ardhi za Waislamu kwa kujidai kuwa wao ndio viongozi wa Uislamu, wanaonyesha na kujifakharisha juu ya mafanikio ya Waislamu huko nyuma, kuwa ni tunu za kihistoria na kiroho, bila ya kuhusisha amri za Shariah kwao wenyewe na mfumo wao wa utawala. Wanazitumia hisia za Waislamu kwa kuwalaza usingizi na kuzikandamiza hasira zao, ambazo hukimbilia uhuru na kujitahidi kutabikisha Shariah katika maisha yao.

Soma zaidi...

Uhuru wa Kweli kwa Indonesia

Sherehe ya miaka 80 ya Siku ya Uhuru wa Indonesia ilichangamshwa na mavazi ya kitamaduni ya kupendeza katika Kasri la Merdeka, Jakarta, Jumapili, Agosti 17, 2025. Waziri wa Afya Budi Gunadi Sadikin alihudhuria akiwa amevalia vazi la Batak, akisema alilichagua kwa sababu ya turathi ya mke wake. Waziri wa Nishati na Rasilimali za Madini Bahlil Lahadalia alivalia vazi la kitamaduni la Solo, akibainisha kuwa hapo awali alikuwa amevaa mavazi ya Papua, Sulawesi, na Maluku. Rais Prabowo Subianto alionekana akiwa amevalia Nusantara yenye rangi ya pembe za ndovu akiwa na peci nyeusi, songket sarong, yenye maua ya yasmini. Watu mashuhuri Raffi Ahmad na Nagita Slavina walivalia mavazi ya Kijava, huku Raffi akiwakumbusha wananchi kuchangia vyema kwa taifa. Mabalozi kutoka nchi marafiki walihudhuria wakiwa wamevalia suti rasmi, huku wananchi wengi pia wakiwa wamevalia mavazi ya kikanda, yakionyesha umoja katika utofauti katika sherehe hizo.

Soma zaidi...

Ndoto ya Kikoloni ya ‘Dola Mbili’ kwa Palestina

Wakati Gaza ikiendelea kuungua, huku makumi ya watu wakiuawa katika Ukanda huo kila siku, huku wakaazi wake wakiendelea kufa kwa njaa, na wakati ghasia zikiongezeka katika Ukingo wa Magharibi mikononi mwa uvamizi wa kinyama wa Kizayuni, kumekuwa na msukumo mpya, hasa wa baadhi ya nchi za Magharibi, kwa ajili ya ‘Suluhisho la Dola Mbili’ kwa Palestina ambayo wanatoa hoja kuwa litaweza kutatua mzozo wa muda mrefu katika eneo hilo. Ufaransa, Uingereza na Canada miongoni mwa mataifa mengine zimetangaza nia yao ya kuitambua dola ya Palestina, ikiwa masharti maalum yatatimizwa.

Soma zaidi...

Marufuku ya Vitabu ya Serikali ya Kibaniani: Jaribio la Kufuta Mapambano na Mihanga ya Kiislamu katika Kashmir Inayokaliwa Kimabavu

Katika onyesho la wazi la ukosefu wa usalama na unafiki, serikali inayoitwa ya “kidemokrasia” ya India, chini ya utawala wake wa kibaniani wa BJP, imetoa amri ya kupiga marufuku vitabu 25 vinavyoandika uhalisia wa kihistoria wa ukaliaji wake wa kimabavu wa Kashmir. Hatua hii, ya tarehe 5 Agosti 2025, inatoka kwa Idara ya Mambo ya Ndani ya idara wa Jammu na Kashmir, ikitangaza kwamba kazi hizi “feki” chini ya Kifungu cha 98 cha Bhartiya Nyaya Sanhita 2023, ikizituhumu kwa kueneza “simulizi za uwongo”, kupigia debe kujitenga, na kutukuza “ugaidi”.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu