Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 547
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Trump alitangaza kwa mshangao jana, Jumamosi, katika chapisho kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Kijamii (Truth Social platform), kwamba "Baada ya usiku mrefu wa mazungumzo yaliyopatanishwa na Marekani, ninafurahi kutangaza kwamba India na Pakistan zimekubali kusitishwa kwa mapigano kamili na mara moja, "na kuzisifu nchi zote mbili kwa kutumia busara na akili kubwa." (Al Jazeera, 11/5/2025) ... ni upi ukweli katika uhasama na mzozo huu? Je, Mkataba wa Maji wa Indus ni nini haswa ambao India imeusitisha kwa muda? Je, Marekani inahusika katika kuanzisha shambulizi hilo na pia kulisitisha?
Kisimamo cha Nusra Mbele ya Bunge la Lebanon kwa ajili ya Waislamu waliowekwa Kizuizini kilicho andaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon.
Vyanzo vya kimatibabu vimeandika kuuawa shahidi kwa Wapalestina wasiopungua 42 kutokana na ulipuaji mabomu wa umbile la Kiyahudi katika Ukanda wa Gaza tangu alfajiri ya Jumatatu, 12 Mei 2025. Uvamizi huo ulianza tena jioni baada ya kusimama kwa saa kadhaa, ambapo mwanajeshi mmoja aliyekamatwa wa umbile la Kiyahudi aliachiliwa huru.
Mabadilishano ya makombora kati ya Pakistan na India yanaendelea katika njia nyingi za kusitisha mapigano huko Kashmir baada ya India kushambulia kwa mabomu maeneo tisa ndani ya Pakistan usiku wa Mei 6, ambayo ilisema ni "miundombinu ya kigaidi iliyohusika na shambulizi la silaha huko Kashmir" mwezi uliopita. Suluhisho la kivitendo la kusonga mbele haliwezi kuwa mzozo mdogo, lakini lazima liwe ukombozi wa kina wa maeneo yanayokaliwa kimabavu.
Mnamo Mei 5, 2025, balozi wa umbile la Kiyahudi nchini India, Reuven Azar, akitoa maoni yake juu ya shambulizi la Bahalkam, lililotokea mnamo 22 Aprili, alisema, "Tumedhamiria kusonga mbele kutetea misingi yetu, kanuni zetu na maadili yetu, na nina hakika kwamba India itafanya vivyo hivyo."
Neno “dola ya kina” (deep state) limetumika sana miongoni mwa wanasiasa na katika vyombo vya habari. Hata hivyo, katika kuchunguza kauli hizi, inadhihirika kwamba ziko tofauti. Je, unaweza kufafanua zaidi uwezekano wa maana ya suala hili ili tuweze kuelewa uhalisia wa kisiasa kuhusiana na neno hili, na kutoa baadhi ya mifano kwa ufafanuzi zaidi?
Hizb ut Tahrir/Wilayat Uturuki inaandaa kongamano la halaiki lenye kichwa “Kongamano Kubwa la Gaza” jijini Ankara, ambapo suluhisho la kweli na la kudumu la kadhia ya Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) litajadiliwa.
Ufalme wa Oman, ambao unaendesha upatanishi katika mazungumzo ya Marekani na Iran, ulitangaza mnamo Alhamisi (kuakhirishwa kwa raundi ya nne ya mazungumzo ambayo yalipangwa kufanyika mnamo Jumamosi katika mji mkuu wa Italia, Roma, "kwa sababu za kiufundi," bila kutaja tarehe mpya. Al-Sharq, 1/5/2025). Mazungumzo ya awali yasiyo ya moja kwa moja kati ya Marekani na Iran yalianza mnamo tarehe 12 Aprili 2025 katika mji mkuu wa Oman, Muscat, kwa upatanishi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Badr Al-Busaidi.