Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Hakika Makafiri wa Dunia Wamekusanyika dhidi yYetu!
- Imepeperushwa katika Pakistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Hakika Makafiri wa Dunia Wamekusanyika dhidi yYetu!
Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Hakika Makafiri wa Dunia Wamekusanyika dhidi yYetu!
Marekani, Kupitia Usitishwa Vita, inafikia Mambo Mawili Makuu kwa Uadui wa Kiyahudi...
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Ijapokuwa Ulimwengu wa Kiislamu Unatawaliwa na Mfumo wa Kikoloni!
Kwa mnasaba wa miaka 103 H ya mkoloni kafiri, kwa msaada wa wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, kuivunja dola ya Uislamu (Khilafah Uthmani) na kukomeshwa kwa mfumo wa utawala katika Uislamu (Khilafah) kutoka katika maisha ya Umma wa Kiislamu, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Uturuki ilitoa filamu ya makala yenye kichwa: “Mustakabali wenye Matumaini kutoka Karne Iliyopotea!”
Mnamo Jumapili, tarehe 1 Disemba 2024, katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na kikao cha 45 cha Baraza Kuu la Baraza la Ushirikiano wa Ghuba iliyoandaliwa na Serikali ya Kuwait, viongozi wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC) na wawakilishi wao walitoa wito wa kumalizwa kwa uhalifu wa mauaji na adhabu ya pamoja huko Gaza, uhamishaji wa wakaazi, uharibifu wa vifaa na miundombinu ya raia. Walitoa wito wa kuingilia kati kulinda raia, kusitisha vita, na kufadhili mazungumzo mazito ili kufikia suluhu endelevu, wakisisitiza misimamo yao madhubuti kuhusu kadhia ya Palestina, kukomesha uvamizi huo, na uungaji mkono wao kwa uhuru wa watu wa Palestina juu ya ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu tangu Juni 1967, na kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu wake, na kuhakikisha haki za wakimbizi, kwa mujibu wa Mpango wa Amani wa Kiarabu na maazimio ya uhalali wa kimataifa. Kuhusiana na Lebanon, viongozi hao walithibitisha mshikamano kamili na Lebanon.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Maafisa Hawa wa Kijeshi Hawaishi ndani kabisa ya Misitu yenye Giza!
Maoni ya habari yaliyotolewa na Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Pakistan.
Kwa imani katika qadhaa ya Mwenyezi Mungu (swt) na kutaka malipo Yake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan inamuomboleza Mbebaji Da’wah katika safu zake: Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas) Aliyefariki kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu asubuhi ya leo, Jumanne, 3/12/2024, akiwa na umri wa miaka 80.
Hizb ut Tahrir Wilayah ya Kenya imechapisha toleo jipya la Jarida la UQAB kwa ajili ya mwezi wa Disemba 2024 M.
Mnamo tarehe 27 Novemba 2024, usitishaji vita ulitangazwa katika upande wa Lebanon kati ya umbile la Kiyahudi na Hezbollah. Moja ya masharti yake ilikuwa kwamba umbile la Kiyahudi lingeondoa jeshi lake linalovamia kutoka kusini mwa Lebanon ndani ya miezi miwili, huku Hezbollah ingerudisha nyuma majeshi yake kaskazini mwa Mto Litani. Makubaliano hayo pia yalivipa vikosi vya Kiyahudi uhuru wa kutembea kusini endapo chama hicho kitakiuka makubaliano hayo, sambamba na kuendelea na safari za ndege za adui katika anga ya Lebanon kwa ajili ya uchunguzi na ujasusi.