Marekani Yaogopa Kuangamia kwa Tawala za Vibaraka katika Nchi za Waislamu na Kuibuka kwa Khilafah
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Marekani haiachi kuonyesha hofu yake ya kuangamia kwa tawala vibaraka katika nchi za Waislamu mara kwa mara. Hofu hii inaonekana kwenye ndimi za viongozi wake; Mshauri wake wa Usalama wa Kitaifa Jake Sullivan anathibitisha kwamba itafanya kazi kuimarisha Jordan, umbile la Kiyahudi (Kizayuni), na Iraq ili mzozo wa Syria usihamia kwao. Siku chache zilizopita, Waziri wake wa Mambo ya Nje Antony Blinken alisisitiza katika hotuba yake kabla ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa NATO juu ya ulazima wa kuzuia kuregea kwa Dola ya Khilafah.