Jumatano, 09 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marekani Yaogopa Kuangamia kwa Tawala za Vibaraka katika Nchi za Waislamu na Kuibuka kwa Khilafah

Marekani haiachi kuonyesha hofu yake ya kuangamia kwa tawala vibaraka katika nchi za Waislamu mara kwa mara. Hofu hii inaonekana kwenye ndimi za viongozi wake; Mshauri wake wa Usalama wa Kitaifa Jake Sullivan anathibitisha kwamba itafanya kazi kuimarisha Jordan, umbile la Kiyahudi (Kizayuni), na Iraq ili mzozo wa Syria usihamia kwao. Siku chache zilizopita, Waziri wake wa Mambo ya Nje Antony Blinken alisisitiza katika hotuba yake kabla ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa NATO juu ya ulazima wa kuzuia kuregea kwa Dola ya Khilafah.

Soma zaidi...

Mumempindua Dhalimu wa ash-Sham, Basi Msikubali Chochote baada ya Dhalimu huyo Zaidi ya Utawala wa Uislamu na Dola yake, Khilafah

Baada ya miaka kumi na nne ya mihanga mikubwa ya watu wa Syria katika mapinduzi yao yaliyobarikiwa, Damascus ilikuwa kwenye miadi ya ushindi alfajiri ya leo, Jumapili 8 Disemba 2024, kwa Idhini ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) alitubariki kwa kupinduliwa kwa dhalimu Assad, baada ya zama za dhulma, uhalifu na udhalimu wa familia ya Assad katika utawala wake wa chuki, wa kimadhehebu kwa muda wa miaka 54. Katika zama zao, walipiga vita Dini, Shariah na waja wa Mwenyezi Mungu (swt). Waliwatia watu kila aina ya mateso. Hakuna ushahidi bora zaidi wa hili kuliko idadi ya kutisha ya wafungwa ambao waliachiliwa huru kutoka kwa magereza yake ya dhulma, maovu.

Soma zaidi...

Hongera Ash-Sham na Watu wake kwa Kumpindua Mtawala dhalimu na Utawala wake, Sasa ni Mbele Kuelekea Khilafah Rashida

Asubuhi ya leo, Jumapili tarehe 8/12/2024 M, na katika siku ya 12 ya operesheni ya “Kuzuia Uvamizi”, wapiganaji waliweza kuingia katika mji mkuu wa Syria, Damascus, na kupindua utawala wa Bashar al-Assad, ambaye Reuters iliripoti - ikiwanukuu maafisa wa Syria – kwamba aliuacha mji mkuu na kuelekea kusikojulikana. Hivyo, wapiganaji wa upinzani waliweza kuikomboa Idlib, Aleppo, Hama, Homs na Damascus, na kuwaachilia maelfu ya wafungwa waliokuwa wakizuiliwa na utawala wa kihalifu katika vyumba vya chini vya jela zake ovu kwa miaka na miongo kadhaa.

Soma zaidi...

Watawala wa Bara Arabu Wanashindana katika Ufisadi na Utiifu kwa Maadui wa Ummah!

Siku chache zilizopita, watawala wa Imarati walijigamba juu ya uhamasishaji wao mkubwa wa kuwafikia wauaji wa Rabbi wa Kiyahudi, Zvi Kogan, kwenye ardhi zao, na kupongeza umakini wa vyombo vya usalama na kasi ya taratibu zao zilizochangia kufichua tukio hilo, baada ya huduma hizi zote kufanya kwa muda wote, kulingana na yale yaliyoelezwa katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati huo huo, Imarati na Wizara yake ya Ulinzi haikujitolea kuwanusuru zaidi ya mashahidi elfu 44 na elfu 104 waliojeruhiwa huko Gaza, ingawa muuaji wao anajulikana na haihitaji uchunguzi au umakini wa vyombo vya usalama kumfikia.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas)

Kwa imani katika qadhaa ya Mwenyezi Mungu (swt) na kutaka malipo Yake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan inamuomboleza Mbebaji Da’wah katika safu zake: Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas) Aliyefariki kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu asubuhi ya leo, Jumanne, 3/12/2024, akiwa na umri wa miaka 80.

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mkutano wa GCC ni Ushirikiano katika Dhambi na Udanganyifu

Mnamo Jumapili, tarehe 1 Disemba 2024, katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na kikao cha 45 cha Baraza Kuu la Baraza la Ushirikiano wa Ghuba iliyoandaliwa na Serikali ya Kuwait, viongozi wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC) na wawakilishi wao walitoa wito wa kumalizwa kwa uhalifu wa mauaji na adhabu ya pamoja huko Gaza, uhamishaji wa wakaazi, uharibifu wa vifaa na miundombinu ya raia. Walitoa wito wa kuingilia kati kulinda raia, kusitisha vita, na kufadhili mazungumzo mazito ili kufikia suluhu endelevu, wakisisitiza misimamo yao madhubuti kuhusu kadhia ya Palestina, kukomesha uvamizi huo, na uungaji mkono wao kwa uhuru wa watu wa Palestina juu ya ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu tangu Juni 1967, na kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu wake, na kuhakikisha haki za wakimbizi, kwa mujibu wa Mpango wa Amani wa Kiarabu na maazimio ya uhalali wa kimataifa. Kuhusiana na Lebanon, viongozi hao walithibitisha mshikamano kamili na Lebanon.

Soma zaidi...

Ghasia za Hivi Karibuni za Kisiasa ni Mapambano ya Madaraka Kati ya Makundi ya Kisiasa yanayoshindana juu ya Kiti Utawala cha Udhalilifu, Khiyana na Ubaraka kwa Amerika

Maandamano ya hivi majuzi yaliyoitwa “Wito wa Mwisho”, yalianza mnamo tarehe 24 Novemba 2024 na kuhitimishwa katika uwanja wa D-Chowk jijini Islamabad mnamo Novemba 27. Mbali na kufungwa kwa barabara, shule na mitandao ya intaneti, karibu makumi ya watu, vikiwemo vyombo vya utekelezaji sheria na raia, waliuawa na makumi kadhaa kujeruhiwa. Hata hivyo, vyovyote itakavyokuwa kwa matokeo ya ghasia hizo kali, masaibu ya watu wa Pakistan yatabaki yale yale. Machafuko haya ya kisiasa ni mapambano ya madaraka kati ya vikundi tofauti  vibaraka wa Amerika. Mabadiliko ya kweli kwa watu yatakuja pale tu majeshi yatakapotoa Nusrah yao kwa ajili ya kusimamisha Khilafah Rashida.

Soma zaidi...

Miaka Miwili ya Utawala bila Uislamu: Kupuuza Amana ya Mwenyezi Mungu

Katika hafla ya kuadhimisha mwaka wake wa pili afisini, Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim, aliandaa Mpango wa Miaka Miwili wa Serikali ya Madani (2TM) na Kongamano la Kitaifa la 2024 la Marekebisho ya Utumishi wa Umma mnamo Novemba 23-24, 2024 katika Jumba la Mikutano la Kuala Lumpur (KLCC). Hafla hilo ilionyesha huduma mbalimbali za serikali chini ya paa moja, na zaidi ya vibanda 30 vinavyotoa huduma na bidhaa kwa umma. Ripoti zilisifu hafla hiyo kuwa ya mafanikio, ikiwa na zaidi ya wageni 200,000. Zaidi ya hayo, Anwar aliendesha kikao cha ukumbi wa jiji kuangazia mafanikio na mipango yake chini ya serikali ya Madani huku akishughulikia ukosoaji, haswa kuhusu mahojiano yake ya CNN yenye utata kuhusu uwepo wa umbile la Kiyahudi na ufadhili wa makampuni ya kibinafsi wa safari zake na ujumbe wake nje ya nchi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu