Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo (469)
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Maelezo yanayohusiana na ramani hayaishii tu katika kujua eneo la nchi ambayo tukio mahususi linalochunguzwa linahusiana. Badala yake, inapanuka hadi kuelewa eneo la nchi kwenye ramani, asili ya jiografia inayohusiana na nchi, asili ya mipaka yake, mafungamano yake na bahari, mafungamano yake na vipengee muhimu vya kijiografia, na kufahamu hali ya ya watu kulingana na idadi ya watu, msongamano wa watu, asili na sifa za idadi ya watu, na umiliki wake wa nishati na teknolojia.
Abu Ubaidah Aamir bin Abdullah bin Al-Jarrah Al-Fihri Al-Qurashi (40 Kabla ya Hijra/584 M hadi 18 Baada ya Hijrah/639 M) alikuwa Swahaba (ra) wa Mtume (saw), kamanda wa Kiislamu, na mmoja wa Maswahaba kumi (ra) waliopewa bishara njema ya Pepo. Alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kusilimu.
Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.