Alhamisi, 28 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  23 Jumada II 1447 Na: HTS 1447 / 66
M.  Jumapili, 14 Disemba 2025

Ripoti ya Habari
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Wamzuru Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Mji wa Wad Madani
(Imetafsiriwa)

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ulitembelea Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Jimbo la Al-Jazirah jana, Jumamosi, 13/12/2025. Ujumbe huo uliongozwa na Ustadh Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Abdulaziz Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na mhandisi Walid Kamil.

Ujumbe huo ulielezea madhumuni ya ziara hiyo, ukisema kwamba inakuja ndani ya muundo wa kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ili kuzuia mpango wa Amerika wa kutenganisha Darfur.

Sheikh Al-Fatih Abdulrahman Shatout alikaribisha ujumbe huo na ziara hiyo, akisema kwamba anajua mengi kuhusu Hizb, na kwamba Hizb ut Tahrir ndiyo pekee inayotoa masuluhisho yaliyo wazi. Kisha akasema kwamba anathamini kujitolea kwa kusimamisha Khilafah, na kwamba yuko tayari kwa kazi yoyote inayofanywa na Hizb kwa ajili ya kuzuia kukatwa kwa Darfur, na kwamba misikiti yao inawakaribisha Mashababu wa Hizb wakati wowote.

Mwishoni mwa ziara hiyo, ujumbe ulimshukuru Sheikh Al-Fatih kwa mapokezi ya dhati na ukarimu.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir

katika Wilayah Sudan

 

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 0912240143- 0912377707
http://www.hizb-sudan.org/
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu