Migogoro Inayosababishwa na Utawala Fisadi Haiwezi Kutatuliwa Kupitia Nao
- Imepeperushwa katika Iraq
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tangu Marekani ilipoikalia kwa mabavu Iraq mwaka 2003, na kwa miaka 22 sasa, imekuwa ikikumbwa na mzozo wa kifedha na umaskini na uchochole ulioenea. Licha ya mapato ya mafuta yanayofikia mamia ya mabilioni kila mwaka, wanasiasa na wataalamu wake hujitokeza kila mwaka kutoa tahadhari kuhusu mgogoro wa kifedha unaoweza kusababisha serikali kukosa uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyikazi.