Jumatatu, 24 Safar 1447 | 2025/08/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jaribio la ATU la Kuwabandika Majina Wanachama wa Hizb ut Tahrir waliokuwa Wazungumzaji wa Makongamano ya Kisiasa ya Mtandaoni kuwa ni Wanamgambo ni Kitendo cha Ugaidi na Ukandamizaji

Serikali ya Hasina ilifanya jaribio jengine lililofeli la kusitisha dawah ya Hizb ut Tahrir katika kurudisha Mfumo kamili wa Maisha wa Kiislamu kupitia kusimamisha tena Khilafah Rashida kwa kuwahangaisha na kuwakandamiza wanachama wake kupitia kikosi chake maarufu cha kigaidi kinachojulikana kama "Kitengo cha Kupambana na Ugaidi (ATU)”.

Soma zaidi...

Demokrasia na Mfumo wake wa Kiulimwengu ni Minyororo ya Utumwa wa Kimarekani Simamisheni Tena Khilafah kwa Ajili ya Mabadiliko Halisi

Mnamo tarehe 27 Machi 2022, Imran Khan alifichua operesheni ya mabadiliko ya serikali kupitia njama ya Marekani kwenye mkutano wa hadhara, na akatangaza mapambano ya umma dhidi ya udhibiti wa Marekani juu ya Pakistan. Hata hivyo, katika muda wa miezi saba na nusu tu, Imran Khan alimaliza rasmi kampeni hii.

Soma zaidi...

Kongamano la Nchi Zinazozungumza Kifaransa Lililofanyika nchini Tunisia ni Kongamano la Kufeli na Usaliti

Kongamano la 18 la marais wa nchi na serikali zinazoshirikiana matumizi ya lugha ya Kifaransa, linaloitwa Kongamano la Nchi Zinazozungumza Kifaransa (Francophone), litafanyika katika kisiwa cha Djerba mnamo Novemba 19 na 20, 2022, baada ya vikwazo vya mara kwa mara tangu ilipotangazwa mnamo 2020 kwamba litafanyika katika nchi yetu.

Soma zaidi...

Mkataba wa Maelewano (MoU) wa Umeme kwa Maji ni Mwezeshaji Waziwazi wa umbile la Kiyahudi Kwa Gharama ya Watu wa Jordan na Ummah na Dhidi ya Chaguo lake la Kuikomboa Palestina

Mnamo tarehe 8/11/2022, juu ya kadhia za ziada za Mkutano wa Kilele wa Tabianchi huko Sharm El-Sheikh, Jordan, Imarati na umbile la Kiyahudi zilitia saini mkataba wa maelewano (MoU) ili kuendeleza upembuzi yakinifu na "kushiriki katika kutengeneza ala muhimu katika zilizopangwa kwa wakati kwa ajili ya mkutano wa COP28” utakaofanyika Imarati mnamo Novemba 2023, kuanzisha miradi miwili tofauti, inayotegemeana na kuhusiana; kwa lengo la kuasisi kiwanda cha kusafisha maji katika Bahari ya Mediterania kwa badali ya kuanzishwa kwa kiwanda cha kuazalisha umeme safi nchini Jordan.

Soma zaidi...

Majibu ya Habari

Mada: Hizb ut Tahrir ni Chama cha Kisiasa Kisichofanya Vitendo vya Kisilaha

Sio kwa Kumuogopa Yeyote, lakini kwa Kufuata Mfano wa Mtume (saw)

Tulipitia ripoti yenye kichwa: “Wahubiri, Watu Wenye Msimamo Mkali, na Makundi ya Kidini Watuma Barua za Vitisho kwa Balozi wa Marekani jijini Khartoum...

Soma zaidi...

Daraa kwa Mara Nyengine Tena iko katikati ya Chuma cha Utawala wa Kihalifu na Nyundo ya Makundi ya Maridhiano

Mji wa Jasim ulizingirwa mwezi Agosti mwaka wa 2022. Kisingizio cha hilo kilikuwa uwepo wa chembechembe za ISIS katika mji huo. Mji huo baadaye ulivamiwa mnamo Oktoba; wengi waliuawa wakati wa uvamizi huo. Kabla ya hapo, mji wa Tafas ulishuhudia mandhari hiyo hiyo, na utawala wa kihalifu ulijaribu kuuvamia na kuzua mifarakano miongoni mwa wakaazi wake.

Soma zaidi...

Shambulizi juu ya Khimar (Kitambaa cha kichwa) barani Ulaya ni Vita vya Hadhara Dhidi ya Hadhara "Jibu kwa Makala ya Jean Chichizola"

Mnamo tarehe 11/09/2022, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kiliwasilisha mjadala kuhusu "Shambulizi dhidi ya Hijabu barani Ulaya", ambapo washiriki walizungumza kuhusu vikwazo ambavyo wanawake wa Kiislamu katika nchi za Magharibi wanakumbana navyo, ambao ulimkasirisha mwandishi wa habari Jean Chichizola kiasi kwamba aliandika makala yaliyochapishwa mnamo tarehe 19/10/2022 kwenye Gazeti la Le Figaro, yenye kichwa "Ufaransa inatuhumiwa kutaka "kuuondoa Uislamu" kwa vijana wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu