Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 575
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
“China inamiliki hisia ya nguvu na mapambano, na kama lengo la China halikufungika tu na kudumisha eneo lake, na kukubali kukabiliana na Amerika kama jibu tu kwa harakati za Amerika kuelekea eneo lake, China haisubutu kupambana na Amerika katika maeneo yao ya ushawishi... na kama isingeanza kutumia ubepari katika nyanja nyingi, haswa katika uchumi... ingekuwa na sauti kubwa kimataifa, na athari yake kwa maslahi ya Amerika ingekuwa na nguvu zaidi. China kwa vyovyote vile ina hisia kali ya nguvu, na inafanya kazi ili kudumisha ubwana wa eneo lake, hata kama iko katika eneo lake...” — Kwa hivyo, je, kizuizi cha China cha mauzo ya nje ya madini adimu ya ardhini kwenda Amerika, kuyauza kwa dhamana za Hazina ya Marekani, kulisasisha jeshi lake, na kujenga jengo kubwa zaidi la kijeshi duniani kusini magharibi mwa Beijing... je, hiki si kiashiria cha ukombozi wa China kutoka kwa mtazamo wake wa kisiasa uliofungika katika eneo lake na upanuzi wa mtazamo huu kushindana na Amerika duniani kote?
“Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha alfajiri ya Jumanne mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Ukanda wa Gaza baada ya kuidhinisha rasimu ya azimio lililowasilishwa na Marekani na kuunga mkono mpango wa amani wa Trump katika sekta hiyo, na Rais Trump aliisifu kura ya Baraza la Usalama kuhusu azimio la Gaza kama wakati wa kihistoria...” (BBC, 18/11/2025). Kuhusu Azimio Nambari 2803, lilichapishwa na vyombo vya habari na lilikuwa ni idhini ya mpango wa pointi 20 wa Rais Donald Trump wa kukomesha mzozo mjini Gaza, lililotolewa mnamo tarehe 29 Septemba 2025.
“Afisi ya rais wa Uturuki ilitangaza mnamo Jumatatu kwamba Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini, Tufan Erhürman, atatembelea Ankara Alhamisi ijayo, 13/11/2025... Burhanettin Duran, mkuu wa idara ya mawasiliano ya rais wa Uturuki, alisema kwamba ziara ya Erhürman Ankara inakuja kutokana na mwaliko wa Rais Erdoğan, na Duran aliongeza kwamba ziara hiyo itakuwa kituo cha kwanza cha kigeni cha Erhurman... Na mnamo tarehe 19 Oktoba Bodi Kuu ya Uchaguzi ya Uturuki ya Cyprus ilitangaza ushindi wa kiongozi wa Chama cha Republican cha Kituruki, Tufan Erhürman, katika uchaguzi wa rais.” (Shirika la Anadolu, 10/11/2025). Kwa hivyo ni nini kimesababisha maridhiano haya? Ikifahamika kwamba Erhurman, wakati wa kampeni yake ya uchaguzi, alikuwa akitoa wito wa kuunganisha kisiwa hicho, huku Erdogan akitoa wito wa dola mbili? Na je, Amerika iko nyuma ya maridhiano hayo? Na Mwenyezi Mungu akulipe kheri.
“Massad Boulos, mshauri mkuu wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu masuala ya Mashariki ya Kati, alithibitisha kwamba jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka wamekubaliana kusitisha mapigano kwa miezi mitatu, kulingana na mpango wa Quartet, unaojumuisha Imarati, Marekani, Saudi Arabia, na Misri, uliotangazwa mnamo Septemba 12.” (Sky News Arabia, 3/11/2025).
Maelfu ya Waislamu katika miji mbalimbali ya Indonesia walifanya matembezi yanayounga mkono Palestina mnamo Oktoba 18 na 19, 2025, chini ya kauli mbiu “Palestinaingali chini ya Uvamizi.” Huko Bandung, zaidi ya waandamanaji 15,000 walikusanyika mbele ya jengo la Gedung Sati, wakinyanyua bendera za Rayah zenye tamko la Tawhid na mabango yenye kauli mbiu kama vile “Tumeni majeshi ya Kiislamu, yakomboe Palestina!”, na “Suluhisho la mwisho kwa Palestina ni kupitia jihad na Khilafah,” na “Palestina itakombolewa kupitia Khilafah na Jihad.”