Jumanne, 07 Ramadan 1447 | 2026/02/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jibu la Swali: Ruwaza ya Marekani ya Kutatua Kadhia ya Cyprus

“Afisi ya rais wa Uturuki ilitangaza mnamo Jumatatu kwamba Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini, Tufan Erhürman, atatembelea Ankara Alhamisi ijayo, 13/11/2025... Burhanettin Duran, mkuu wa idara ya mawasiliano ya rais wa Uturuki, alisema kwamba ziara ya Erhürman Ankara inakuja kutokana na mwaliko wa Rais Erdoğan, na Duran aliongeza kwamba ziara hiyo itakuwa kituo cha kwanza cha kigeni cha Erhurman... Na mnamo tarehe 19 Oktoba Bodi Kuu ya Uchaguzi ya Uturuki ya Cyprus ilitangaza ushindi wa kiongozi wa Chama cha Republican cha Kituruki, Tufan Erhürman, katika uchaguzi wa rais.” (Shirika la Anadolu, 10/11/2025). Kwa hivyo ni nini kimesababisha maridhiano haya? Ikifahamika kwamba Erhurman, wakati wa kampeni yake ya uchaguzi, alikuwa akitoa wito wa kuunganisha kisiwa hicho, huku Erdogan akitoa wito wa dola mbili? Na je, Amerika iko nyuma ya maridhiano hayo? Na Mwenyezi Mungu akulipe kheri.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Sudan Baada ya Vikosi vya Msaada wa Haraka Kuchukua Udhibiti wa El Fasher

“Massad Boulos, mshauri mkuu wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu masuala ya Mashariki ya Kati, alithibitisha kwamba jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka wamekubaliana kusitisha mapigano kwa miezi mitatu, kulingana na mpango wa Quartet, unaojumuisha Imarati, Marekani, Saudi Arabia, na Misri, uliotangazwa mnamo Septemba 12.” (Sky News Arabia, 3/11/2025).

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Indonesia: Matembezi Makubwa ya Kukumbusha Ulimwengu “Palestina ingali chini ya Uvamizi”

Maelfu ya Waislamu katika miji mbalimbali ya Indonesia walifanya matembezi yanayounga mkono Palestina mnamo Oktoba 18 na 19, 2025, chini ya kauli mbiu “Palestinaingali chini ya Uvamizi.” Huko Bandung, zaidi ya waandamanaji 15,000 walikusanyika mbele ya jengo la Gedung Sati, wakinyanyua bendera za Rayah zenye tamko la Tawhid na mabango yenye kauli mbiu kama vile “Tumeni majeshi ya Kiislamu, yakomboe Palestina!”, na “Suluhisho la mwisho kwa Palestina ni kupitia jihad na Khilafah,” na “Palestina itakombolewa kupitia Khilafah na Jihad.”

Soma zaidi...

Ni Dhambi Kubwa kwamba Gaza Haikukombolewa Au Umbile la Kiyahudi Halikutokomezwa kwa Juhudi za Wanajeshi wa Waislamu, Bali Iliangamizwa Kabisa na Kukombolewa Kidogo kwa Mpango Wa Trump na Usaliti wa Watawala wa Waislamu!!

Serikali ya Misri ilitangaza kusherehekea utekelezwaji wa mpango wa Trump mjini Gaza. Sisi alimwalika Rais wa Marekani kusherehekea kwa sababu yeye ndiye mwanzilishi wa mpango wa Gaza: [Rais Trump wa Marekani alisema mnamo Alhamisi kwamba mateka waliosalia wanaoshikiliwa na Hamas katika Ukanda wa Gaza wataachiliwa huru mnamo Jumatatu au Jumanne ya wiki ijayo, na kwamba bado analenga kuzuru eneo hilo kusherehekea hafla hii... “Ni muhimu kutaja kuwa Rais Sisi wa Misri alikuwa amemwalika Trump kushiriki katika sherehe ambazo zitafanywa nchini Misri ili kuadhimisha kutiwa saini kwa makubaliano, akiyachukulia kuwa makubaliano ya kihistoria ambayo yanazifisha taji juhudi za Misri, Marekani, na wapatanishi katika kipindi cha hivi karibuni.” (CNN Arabic, 9/10/2025)]

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Kikao cha Majadiliano “Mradi wa Ukombozi... Katika Mizani ya Hukmu za Sheria ya Kiislamu”

Mnamo Jumapili, 12 Oktoba 2025, Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Tunisia iliandaa kikao cha mazungumzo kwa kichwa “Mradi wa Ukombozi... Katika Mizani ya Hukmu za Sheria ya Kiislamu” katika eneo la Kairouan. Kikao hicho kilihudhuriwa na idadi kubwa ya wakaazi wa eneo hilo.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu