Hizb ut Tahrir Inatoa Salamu za Rambirambi kwa Kuondokewa na Mkurugenzi wa Radio Biladi
- Imepeperushwa katika Sudan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir Inatoa Salamu za Rambirambi kwa Kuondokewa na Mkurugenzi wa Radio Biladi.
Hizb ut Tahrir Inatoa Salamu za Rambirambi kwa Kuondokewa na Mkurugenzi wa Radio Biladi.
Mkutano baina ya Kiongozi wa Kabila la Al-Habab na Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Wilayah ya Sudan.
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan, na wanachama Ustadh Abdullah Hussein, Mratibu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, na Ustadh Muhammad Mukhtar, Mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alikutana na idadi ya viongozi wa Harakati ya Islamic Action katika afisi ya Hizb mjini Port Sudan, Jumapili, 26 Shawwal 1445 H sawia na 05/05/2024.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilimpokea afisini mwake adhuhuri mnamo siku ya Jumapili, 26 Shawwal 1445 H sawia na 05/05/2024 M, Al-Nazir Faisal Musa Shugar, Nazir wa makabila yote ya Darfur, na pamoja naye alikuwa Meya Babiker Harun Adam.
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan Wakutana na Ustadh Al-Taher Hassan Al-Mohami.
Mkutano huo ulijadili hali ya kisiasa nchini, vita vinavyoendelea, na hali ya mvutano kati ya vipote vya watu wa Sudan, kutoka kwa mapigano ya kikabila, migogoro kwa msingi wake, na maafa ambayo imeleta juu ya nchi na watu, na kwamba njia ya kutoka humo inawezekana tu kwa msingi wa hukmu za Uislamu mtukufu na sheria yake.
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Sheikh Nasser Ridha, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, na akiwemo Abdullah Hussein, Mratibu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, na Mohammed Mukhtar, Mwanachama wa Hizb ut Tahrir, ulikutana na Sheikh Othman Arefa, mjumbe wa Kamati ya Wanazuoni wa Jimbo la Bahari Nyekundu na Imam wa Msikiti wa Ibn Masoud, mnamo siku ya Jumamosi, 25 Shawwal 1445 H sawia na 4 Mei 2024 M, katika Afisi ya Hizb ut Tahrir Wilayah ya Sudan. katika mji wa Port Sudan.
Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ulioongozwa na Ustadh Yaqoub Ibrahim, na mwanachama: Ustadh Mwanasheria Ahmad Abkar, Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, na Ustadh Suleiman Al-Dasis, na Ustadh Daoud Abdullah, wanachama wa Hizb ut Tahrir, walimtembelea, Bw. Azraq Tilfone, Nazir (Kiongozi Mkuu) wa Makabila ya Nuba nchini Sudan, katika makaazi yake mjini Port Sudan mnamo siku ya Ijumaa, 24 Shawwal 1445 H sawia na 3/5/2024 M.
Mgogoro wa Sudan, vita vinavyoendelea na matokeo yake yalijadiliwa. Pande zote mbili zilisisitiza umuhimu wa suluhisho kuwa mbali na uingiliaji kati na ajenda za kutoka nje, na kwamba suluhisho lazima litokane na itikadi tukufu ya Uislamu.
Kwa msaada na muongozo wa Mwenyezi Mungu, leo, Jumapili, tarehe 7 Ramadhan 1445 H, sawia na tarehe 17 Machi, 2024, Afisi ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan imezinduliwa mjini Port Sudan (mtaa wa Al-Athmah), kusini-mashariki mwa uwanja. Itatumika kama nguzo ya kueneza fikra za Kiislamu, jukwaa la thaqafa ya Kiislamu, kitovu cha utambuzi wa kisiasa, na nukta kianzilishi cha ubebaji ulinganizi kuregesha maisha kamili ya Kiislamu kupitia kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya utume.