Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
| H. 26 Jumada I 1447 | Na: HTS 1447 / 56 |
| M. Jumatatu, 17 Novemba 2025 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Ni Khilafah Rashida pekee kwa Njia ya Utume ndiyo itakayong'oa Mizizi ya Ukoloni wa Magharibi kutoka Ardhi Zetu
(Imetafsiriwa)
Kwa mwaliko wa Balozi wa Uingereza, Kumar Iyer, pamoja na Ujerumani, Ireland, Uholanzi, na Norway, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lilifanya kikao mnamo Ijumaa, 14/11/2025, kuhusu ukiukaji katika mji wa El-Fasher. Baraza hilo lilipitisha kwa kauli moja azimio linaloiamuru Misheni Huru ya Kutafuta Ukweli, ambayo Baraza lilikuwa limeianzisha mnamo 11/10/2023, kuchunguza ukiukaji uliofanywa katika mji huo, ambapo Baraza liliamuru kuwatambua wote waliohusika, ili kusaidia kuwafikisha mbele ya sheria. Na kama mwendelezo wa mbinu yake ya kukataa misheni hii tangu kuanzishwa kwake, Waziri wa Sheria, Abdullah Darf, alitangaza katika mahojiano na tovuti ya habari ya uchunguzi jana, Jumapili 16/11/2025, kwamba “Sudan inakataa kupeleka uchunguzi kuhusu uhalifu wa Vikosi vya Msaada wa Haraka huko Al-Fashir kwa Kamati ya Kutafuta Ukweli.”
Mzozo unaoendelea nchini Sudan ni mojawapo ya matukio ya mzozo wa kikoloni wa Magharibi, kati ya mkoloni kafiri wa zamani, Uingereza pamoja na Ulaya upande mmoja, na mkoloni mpya, Amerika, upande mwengine, kila mmoja akiwa na zana zake za ndani, kikanda, na kimataifa. Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Turk, aliregelea mzozo huu, ambapo alisema katika kikao cha Baraza kilichotajwa: “Sudan iko chini ya uzito wa mzozo wa wakala kuhusu maliasili na bidhaa zake, ambazo zinajumuisha dola nyingi ndani ya kanda hii na nje yake.”
Dhidi ya mazingira ya kuanguka kwa El-Fasher, ambayo ilisababisha pigo kubwa kwa ushawishi wa kijeshi wa Uingereza unaowakilishwa katika vikosi vya pamoja, vibaraka wa Uingereza walianza kufanya kazi, wakitumia mashini kubwa ya vyombo vya habari inayoungwa mkono na njia maarufu za setilaiti, katika kukuza propaganda dhidi ya uhalifu wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), ikiambatana na uamshaji wa vibaraka wote wa Uingereza na Ulaya katika mashirika ya kimataifa, haswa mashirika ya Umoja wa Mataifa. Wote walianza kufanya kazi katika faili la kile kinachoitwa haki za binadamu, wakisisitiza uhalifu wa RSF ambao ndio chombo muhimu zaidi kinachotegemewa na sera ya Marekani huko Darfur, ili kuwafanya kuwa wahalifu, kuwadhoofisha, na kuwaondoa katika mlinganyo wa migogoro ya kimataifa. Kwa hivyo, harakati ya Baraza la Haki za Binadamu, ambalo ni chombo halisi cha sera ya Ulaya, haswa Uingereza, katika uwanja wa migogoro ya kimataifa, ilikuja haswa baada ya Rais wa Amerika Donald Trump kutia saini, jioni ya Jumanne 04/02/2025, amri ya rais inayoamuru nchi yake ijiondoe kutoka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa. Na ili kuzuia harakati za vibaraka wa Uingereza na wale walio pamoja nao, Amerika iliiagiza serikali ya Sudan kukataa Kamati ya Kutafuta Ukweli, na kuiagiza RSF kukubali kamati hiyo ili waimarishe msimamo wao katika kukabiliana na tuhma, ili dhoruba ipite bila hasara kubwa kwa Amerika.
Kisha Amerika haikusimama hapo, lakini Waziri wake wa Mambo ya Nje, Marco Rubio, alitoa taarifa kali dhidi ya RSF, ambayo iliifanya Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan kushangilia. Rubio alisema katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Hamilton nchini Canada mnamo 12/11/2025, na kulingana na tafsiri ya tovuti rasmi ya serikali ya Marekani, maandishi ya hotuba yake ni: “Na unapoibua suala la ukatili huu, wao RSF—hutumia kisingizio kwamba hawa ni wahalifu. Ukweli ni, wao si wahalifu. Wanafanya hivi kwa utaratibu, na hili ni jambo tunalolichukulia kwa uzito, na tunafanya tuwezavyo kuwashawishi nchi husika kukaa kwenye meza ya mazungumzo ili kulizuia.” Ingawa alielezea uhalifu unaofanywa na Vikosi vya Msaada wa Haraka dhidi ya raia kama wa kimfumo, na sio tu upotovu unaofanywa na watu wahalifu, hakuelekea upande wa kuwafanya kuwa wahalifu; badala yake aliziomba nchi zinazowaunga mkono kusitisha! Hii ndiyo tabia ya Amerika, hifadhi ya maovu: wakati uhalifu wa vibaraka wake unapofichuliwa, hupitisha hukumu ya uhalifu wao ili kuchukua faili ya uhalifu, kisha kuitupa kwenye pipa la takataka. Na vivyo hivyo makafiri wakoloni: faili za uhalifu wa Sisi huko Rabaa ziko wapi?! Na faili ya matumizi ya silaha za kemikali ya Bashar iko wapi huko Ghouta ya Damascus na miji mengine?! Na uhalifu wa Muhammad bin Salman wa kumkata mwandishi wa habari Khashoggi katika ubalozi nchini Uturuki uko wapi?!
Hakika inasikitisha sana kwamba nchi yetu imekuwa uwanja wa mizozo ya kimataifa kuhusu ushawishi kati ya Amerika na Ulaya, hasa Uingereza. Wanafanya biashara na damu ya watu wetu na heshima yao. Wao ni taifa moja katika uadui, hawawatakii kheri Waislamu mahali popote au wakati wowote. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema:
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا بِطَانَةً مِّن دُونِكُمْ لَا يَأْلُونَكُمْ خَبَالاً وَدُّوا مَا عَنِتُّمْ قَدْ بَدَتِ الْبَغْضَاءُ مِنْ أَفْوَاهِهِمْ وَمَا تُخْفِي صُدُورُهُمْ أَكْبَرُ قَدْ بَيَّنَّا لَكُمُ الْآيَاتِ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ]
“Enyi mlio amini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini.” [Surat Aal-i-Imran: 118].
Makafiri wakoloni hawajali kuhusu kuuawa kwa Waislamu, wala hawajali kuhusu kuvunjiwa heshima yao.
Waislamu wamepoteza mchungaji, kwa hivyo mbwa mwitu wa kibepari wamekiuka matukufu yao, na hakuna kitakachotuokoa kutokana na msiba huu isipokuwa kutoa nusrah kwa Hizb ut Tahrir ili kusimamisha Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume, ambayo itawakatilia mbali makafiri kutoka katika ardhi zetu, kuzuia kuingilia kwao mambo yetu, na kukomesha biashara yao kwa damu na heshima yetu.
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ يَحُولُ بَيْنَ الْمَرْءِ وَقَلْبِهِ وَأَنَّهُ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ]
“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu huingia kati ya mtu na moyo wake, na kwamba hakika kwake Yeye tu mtakusanywa.” [Surat Al-Anfal:24]
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb Ut Tahrir
katika Wilayah Sudan
| Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Sudan |
Address & Website Tel: 0912240143- 0912377707 http://www.hizb-sudan.org/ |
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com |