Logo
Chapisha ukurasa huu

Afisi ya Habari
Wilayah Bangladesh

H.  26 Muharram 1447 Na: H 1447 / 04
M.  Jumatatu, 21 Julai 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Taasisi zote za Kikoloni, ikiwemo Tume Kuu ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu, ni Ala za kufikia Maslahi ya Marekani; Khilafah pekee kupitia kung'oa Misingi ya Taasisi zote hizi ndio itakayolinda Uislamu, Maslahi ya Watu na Ubwana wa Nchi hii

(Imetafsiriwa)

Licha ya maandamano na wasi wasi wa ngazi zote za wananchi na vyama vya kisiasa, hatimaye serikali ya mpito ya Bangladesh imetia saini makubaliano ya kuanzisha afisi ya taasisi ya Kikoloni yenye ushawishi wa Marekani, Tume Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa. Uamuzi huu wa serikali umekaribishwa na mashirika ya wanawake yenye chuki dhidi ya Uislamu, ambayo yanashiriki kikamilifu katika usawa wa kijinsia wa Magharibi, utambuzi wa kijamii wa "taaluma" ya kuchukiza ya ukahaba, na kile kinachoitwa haki za binadamu za LGBTQ ikiwa ni pamoja na ushoga unaoangamiza jamii; ilhali wana utata na kukosolewa na ngazi zote za watu kwa sababu hawana sauti katika kuweka haki adilifu na utu wa wanawake, uhuru kutokana na kazi za kikatili, na uboreshaji wa hali ya maisha. Aidha, hatua hii imekaribishwa na uongozi wenye utata nchini ambao ni wachochezi wa jumuiya na kutaka Marekani na India kuingilia kati nchini humo kwa kuibua moshi wa ukandamizaji wa watu walio wachache. Ijapokuwa serikali ya mpito haijachukua hatua na mipango yoyote madhubuti ya kulinda maisha na mali za wananchi na kutatua mgogoro wa kisiasa uliopo nchini humu, lakini hatua zao mbalimbali za kulinda maslahi ya Wamarekani zimewakasirisha na kuwavunja moyo wananchi. Hata wameweka mfano mmoja baada ya mwengine usio na aibu wa utiifu wao kwa Wamarekani kwa muda mfupi mno.

Enyi Watu, ni lazima mjue kwamba ripoti ya hivi majuzi iliyochapishwa na Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa katika utekelezaji wa ajenda mbovu ya kisiasa ya Marekani imewasilisha vikosi vyetu vya kijeshi kama wakiukaji wa haki za binadamu, na hivyo kuwafanya kuwa na utata duniani kote na kupanga njama ya kuwavunjia heshima; bado hawajazungumza dhidi ya njama ya India ya mauaji ya Pilkhana na mateso ya kinyama kwa familia za maafisa wa jeshi. Marekani imetoa mafunzo, teknolojia na silaha kwa baadhi ya vikosi vyetu vya kijeshi na vya usalama, kikiwemo RAB, ili kuwakandamiza wanasiasa mashuhuri wanaobeba da’wah ya Uislamu na walio imara katika kuipendelea nchi, na wamezitumia kwa malengo yasiyo ya kibinadamu. Madai mazito dhidi ya shirika hili ambalo limejifanya kuwa shirika la kutetea haki za binadamu, ni kwamba lina uwezo wa kufikia taasisi muhimu za muundo wa Serikali, zikiwemo mahakama, na limekusanya taarifa nyeti, na limeunda data za viongozi waaminifu wa kisiasa wanaofanya kazi dhidi ya dhalimu na kisha kushiriki habari hizo na washirika wao kwa manufaa ya kisiasa. Shirika hili lina afisi nchini Syria ambako limekabidhi taarifa za wanaharakati wa kisiasa na waasi wanaopigana dhidi ya dhalimu Bashar kwa kibaraka wa Marekani Bashar al-Assad na mshirika wao Urusi, na limeshirikiana kuwakandamiza. Vile vile, shirika hili lina afisi nchini Palestina, ambapo limekabidhi habari za siri kwa umbile haramu la Kiyahudi ili kuwakandamiza na kuwaua Waislamu, mfano ambao sasa uko wazi kwa walimwengu. Katika mahojiano na chombo kimoja cha habari cha Uingereza, Emma Reilly, mwanasheria wa haki za binadamu katika Tume ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (UNHRC), alisema, "Wanachama wa ngazi za juu wa UNHRC wanakabidhi kwa serikali ya Uyghur majina ya wapinzani wa Uyghur ili kupata manufaa ya kisiasa kutoka kwa China. Hili linatokea licha ya sera ya China ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Uyghur wa Turkestan Mashariki.” Sambamba na hili, hapana shaka kuwa Wamarekani watatumia taasisi hii kuwatumia ndugu zetu Waislamu, Waislamu wa Rohingya, kwa maslahi yao ya kijiografia na kisiasa na kuwasaliti chini ya kivuli cha haki za binadamu, kutekeleza ‘korido za kibinadamu’ au ‘chaneli za kibinadamu’. Kwa hakika, hili ‘Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa’, ambalo lina ushawishi wa Marekani, ni taasisi ya kitapeli iliyopakwa sukari. Kwa hiyo, maafisa na wafanyikazi wa taasisi hii huongeza masharti ya ‘msamaha wa dhima’ kwenye mikataba na nchi wanamofanyia kazi. Mwenyezi Mungu (swt) asema,

[وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ قَالُوا إِنَّمَا نَحْنُ مُصْلِحُونَ، أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ الْمُفْسِدُونَ وَلَٰكِن لَا يَشْعُرُونَ]

“Na wanapo ambiwa:Msifanye uharibifu ulimwenguni. Husema: Bali sisi ni watengenezaji. Hakika wao ndio waharibifu, lakini hawatambui.” [Surah Al-Baqarah: 11-12].

Enyi Watu, shirika hili linapiga vita Uislamu katika ulimwengu wa Kiislamu na linatoa kila aina ya msaada, ikiwa ni pamoja na fedha, kwa vibaraka wao ili kutekeleza ajenda ya kuangamiza maadili ya Uislamu. Ni wazi mithili ya mwangaza wa mchana kwamba jamii yao leo iko katika msukosuko kutokana fikra na maadili yao potovu. Hata hivyo, nchi za Magharibi zinalazimisha usawa wa kijinsia, ukahaba unaochukiza, ushoga, na LGBTQ katika jamii ya Kiislamu kupitia sura hii ya haki za binadamu na inaendelea na mradi wake wa kuangamiza maadili ya Kiislamu kwa jina la maadili huria. Inauita msimamo ulio kinyume na hili kuwa ni msimamo mkali na inawaunga mkono katika ukandamizaji wao. Mwenyezi Mungu (swt) asema,

[وَلَنْ تَرْضَى عَنكَ الْيَهُودُ وَلَا النَّصَارَى حَتَّى تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمْ قُلْ إِنَّ هُدَى اللَّهِ هُوَ الْهُدَى]

“Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uwongofu.” [Surah Al-Baqarah: 120].

Enyi Maafisa Wanyoofu katika Jeshi, mnashuhudia kwamba tabaka la watawala watiifu kwa Marekani, wakipuuza hisia na maandamano ya wananchi, wanachukua hatua moja baada ya nyingine kutekeleza ajenda ya Marekani. Wanachukua msimamo dhidi ya wananchi katika kutekeleza miradi ya Marekani dhidi ya Uislamu, Waislamu na nchi. Wakati maandamano na hasira za watu hazifanyi kazi, kimbilio la mwisho la watu ni wana wenye nguvu wanaofanya kazi katika jeshi. Kama mulivyo ilazimisha serikali hii kujiondoa kwenye 'korido ya kibinadamu' na mukapata sifa za watu. Vivyo hivyo, shirikini katika kupinga miradi yote ya mkoloni kafiri Marekani, ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa afisi ya Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu, mazoezi ya kijeshi ya pamoja na Wamarekani, na kumakinisha udhibiti wao. Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema, «إِنَّمَا الْإِمَامُ جُنَّةٌ يُقَاتَلُ مِنْ وَرَائِهِ وَيُتَّقَى بِهِ» “Hakika Imam (Khalifa) ni ngao, Waislamu hupigana nyuma ya na kujihami kwaye” [Sahih Muslim]. Ni wazi kutokana na hadith hii ya Mtume wetu kipenzi, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) kwamba mfumo wa Khilafah pekee ndio mlinzi wa kweli wa Umma wa Kiislamu. Taasisi zote za Kikoloni, likiwemo Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa, ni ala za kufikia maslahi ya Marekani; Khilafah pekee ndiyo itakayong'oa kabisa misingi ya taasisi zote hizi, na itaulinda Uislamu, maslahi ya watu na ubwana wa nchi. Kwa hiyo, badala ya kuwatazama watawala na wanasiasa hawa wapumbavu watiifu kwa Wamarekani - changamkeni kusimamisha Khilafah ili kuulinda Uislamu, maslahi ya watu na ubwana wa nchi; na kwa hili toeni nusrah (msaada wa kimada) kwa chama cha kisiasa chenye ikhlasi na kipaji cha Hizb ut Tahrir.

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ يَحُولُ بَيْنَ الْمَرْءِ وَقَلْبِهِ وَأَنَّهُ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ]

“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu huingia kati ya mtu na moyo wake, na kwamba hakika kwake Yeye tu mtakusanywa.” [Surah Al-Anfal: 24]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir

katika Wilayah Bangladesh

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Bangladesh
Address & Website
Tel: ‎+88 01798 367 640‎
www.ht-bangladesh.info
E-Mail: contact@ht-bangladesh.info, htmedia.bd@outlook.com Skype: htmedia.bd

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.