Je, Kura ya Kutokuwa na Imani ni Mchakato wa Kisiasa au wa Kimahakama?
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Wabunge nchini Kenya wameanza mchakato wa kumwondoa naibu rais wa nchi hii afisini. Wale wanaounga mkono juhudi hizo wanamshutumu Rigathi Gachagua kwa kuhusika katika maandamano ya Juni ya kupinga serikali - ambayo yaligeuka kuwa mabaya - pamoja na kuhusika katika ufisadi, kuhujumu serikali na kuendeleza siasa za mgawanyiko wa kikabila. Naibu rais amepuuzilia mbali madai hayo.