Logo
Chapisha ukurasa huu

Afisi ya Habari
Wilayah Misri

H.  13 Rabi' II 1447 Na: 1447/17
M.  Jumapili, 05 Oktoba 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Kauli za Uhalalishaji Mahusiano ni Tangazo la Wazi la Kuoanishwa na Adui na Kujitenga na Ummah

(Imetafsiriwa)

Siku za hivi karibuni zimeshuhudia msururu wa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty wakati wa ushiriki wake katika makongamano ya kimataifa. Maarufu zaidi kati ya kauli hizi ni msisitizo wake juu ya “umuhimu wa 'Israel' kuishi kwa amani na kuoanishwa ndani ya eneo hili,” na “utayari kamili wa kuhalalisha mahusiano na ‘Israel’" pamoja na Saudi Arabia na nchi zengine, na kauli yake kwamba “suluhisho pekee kwa mustakbali ni kuanzishwa kwa dola ya Palestina isiyo na kijeshi inayoishi kwa amani na ‘Israel’.” Kauli hizi waziwazi zinaakisi mwelekeo unaofuatwa na tawala zilizoko katika nchi za Kiislamu: njia iliyojaa uhalalishaji mahusiano na umbile nyakuzi, na hata juhudi za kulilinda na kulioanisha ndani ya eneo hili, kuhudumia mradi wa kikoloni wa Magharibi.

Wakati waziri wa mambo ya nje wa nchi moja ya Kiislamu anaposema kwamba “ni muhimu kwa 'Israeli' kuishi kwa amani na kujumuika ndani ya eneo hili,” hasemi juu ya haja ya kukomesha uvamizi wa kupita kiasi, bali kuhusu kukiri uwepo wa umbile hili na kulichukulia kuwa ni sehemu ya kimaumbile ya eneo hili. Uoanishwaji katika eneo unaweza kupatikana tu kwa kutambua uwepo wake kisiasa na kisheria, na kwa kuichukulia kama dola ya kimaumbile yenye haki ya kuwepo, na si kama umbile ngeni lililopandikizwa ndani ya moyo wa Umma. Msimamo huu kimsingi unagongana na hukmu wazi ya Kiislamu juu ya suala hili: Palestina ni ardhi ya Kiislamu iliyokombolewa na Waislamu, na ni wakfu kwa Umma wa Kiislamu. Haijuzu kuiacha, hata shubiri moja. Umbile la Kiyahudi ni umbile nyakuzi lililoanzishwa na mkoloni kafiri Magharibi baada ya kuivunja Dola ya Khilafah.

Wito wa uhalalishaji kamili wa mahusiano ni tafsiri ya kivitendo ya utiifu, badala yake ni usaliti wa wazi kwa Ummah. Hii ni kwa sababu uhalalishaji mahusiano na adui anayeikalia kimabavu humpa nguvu, huimarisha uwepo wake, na hudhoofisha msimamo wa Umma wa Kiislamu, ambao unakataa kumtambua. Kulikubali umbile linalokalia kimabavu na kujaribu kuutuliza kwa amani na uhalalishaji mahusiano hakutabadili uhalisia wake, wala hakutalazimisha watu kulikubali na kuhalalisha mahusiano nalo.

Kauli hizi zinadhihirisha pengo kubwa kati ya serikali zinazotawala na Ummah. Umma bado unaichukulia Palestina kadhia yake kuu na unakataa kutambua au kuhalalisha mahusiano na umbile la Kiyahudi, msimamo wanaouonyesha katika kila fursa. Ama kuhusu tawala hizi, zimejishughulisha na miradi ya kuhalalisha mahusiano na usaidizi wa kisiasa na usalama kwa umbile hilo. Wameshiriki hata katika kuzingirwa kwake Gaza, na kuzuia hatua zozote halisi za kusaidia watu wake.

Kauli za Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty, iwe kuhusu “uoanishaji,” “uhalalishaji kamili wa mahusiano,” au “dola isiyo na jeshi,” sio misimamo ya kibinafsi. Bali ni kielelezo cha wazi cha sera za tawala za Kiarabu zenye fungamano na nchi za Magharibi, ambazo zinafanya kazi ya kufilisi kadhia ya Palestina. Vile vile inaakisi kujitenga kwa tawala hizi kutoka kwenye imani na hisia za Umma. Umbile nyakuzi ni mwili wenye saratani uliowekwa ndani ya mwili wa Ummah. Haijuzu kuishi nalo au kujioanisha nalo; badala yake, ni lazima ling'olewe.

Enyi Askari wa Kinanah: Kauli hizi za kudhalilisha zinazotolewa na viongozi, zinazotambua uhalali wa umbile nyakuzi na wanaona kuwepo kwake na usalama wake kuwa ni jambo la kimaumbile, hazitokani na Ummah na wala haziuwakilishi. Badala yake, hutolewa na serikali zilizounganishwa na mkoloni, zinazokuza miradi yake na kufanya kazi kulilinda. Ummah ambao nnyinyi ni miongoni mwake, na ambao ardhi na adhama yake mliapa kuilinda, unalikataa kabisa umbile hili na kuliona kuwa ni adui mnyakuzi ambaye si wa kuishi pamoja naye wala kufanya naye mapatano, bali ni kupigana na kung'olewa... Wajibu wenu wa Shariah leo ni kukusanyika kwa ajili ya kuinusuru Dini yenu, Ummah wenu, na matukufu yenu, kuukana utiifu wenu kwa watawala vibaraka wanaosalimu amri, na zielekezeni silaha zenu kwa adui wa kweli wa Ummah, ili mpate kuandika hadithi za ushindi kama walivyofanya babu zenu.

[وَمَا لَكُمْ لَا تُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْ هَذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا]

Na mna nini msipigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu na ya wale wanao onewa, wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola Mlezi wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhaalimu!” [An-Nisa: 75]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Misri

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Misri
Address & Website
Tel: 
http://hizb.net/
E-Mail:  info@hizb.net

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.